Isaya 16:1-14

  • Ujumbe juu ya Moabu unaendelea (1-14)

16  Mutume kondoo-dume kwa mutawala wa inchi,Kutoka Sela kupitia jangwa,Mupaka kwenye mulima wa binti ya Sayuni.  2  Kama ndege mwenye alifukuzwa katika chicha yake,*+Ni vile mabinti wa Moabu watakuwa kwenye nafasi za kuvukia za Arnoni.+  3  “Mutoe shauri, mutimize uamuzi. Fanya kivuli chako cha katikati ya muchana kikuwe kama usiku. Ficha wenye walisambazwa na usitoe wale wenye kukimbia.  4  Acha watu wangu wenye walisambazwa wakae ndani yako, Ee Moabu. Ukuwe mahali pao pa kujificha kwa sababu ya mwenye kuharibu.+ Mukandamizaji atafikia mwisho wake,Uharibifu utafikia mwisho,Na wale wenye kukanyanga-kanyanga wengine wataharibiwa kutoka katika dunia.  5  Kisha kiti cha ufalme kitafanywa kuwa imara kabisa katika upendo mushikamanifu. Ule mwenye kukiikalia katika hema ya Daudi atakuwa muaminifu;+Atahukumu kwa haki na atatenda haraka uadilifu.”*+  6  Tumesikia kuhusu kiburi cha Moabu⁠—​iko* na kiburi sana+⁠—Majivuno yake na kiburi chake na kasirani yake kali;+Lakini maneno yake yenye hayana maana yataisha.  7  Basi Moabu atamuombolezea Moabu;Wote wataomboleza.+ Wale wenye walipigwa wataomboleza kwa sababu ya keki za zabibu za Kir-hareseti.+  8  Kwa maana matuta ya Heshboni+ yamekauka. Muzabibu wa Sibma,+Watawala wa mataifa wamekanyanga-kanyanga matawi yake mekundu yenye kungaa;*Walikuwa wamefika mupaka Yazeri;+Walikuwa wameenea mupaka katika jangwa. Machipukizi yake yalikuwa yameenea na kufika mupaka katika bahari.  9  Ndiyo sababu nitalilia muzabibu wa Sibma kama vile ninalilia Yazeri. Machozi yangu yatakulowanisha, Ee Heshboni na Eleale,+Kwa kuwa kupiga vigelegele kwa sababu ya matunda yako ya kipindi cha joto na mavuno yako kumeisha.* 10  Shangwe na furaha zimeondolewa katika shamba la matunda,Na hakuna nyimbo za furaha ao kupiga vigelegele katika mashamba ya mizabibu.+ Mwenye kukanyanga hakanyange tena divai katika chombo cha kukamulia divai. Kwa maana nimefanya vigelegele vimalizike.+ 11  Ndiyo sababu niko na musukosuko ndani yangu kuhusu Moabu,+Kama wakati kinubi kinapigwa,Na utu wangu wa ndani sana kuhusu Kir-hareseti.+ 12  Hata kama Moabu anajichokesha kwenye mahali pa juu na kuenda kusali katika patakatifu pake, hatatimiza kitu chochote.+ 13  Hili ndilo neno lenye Yehova alisema zamani kuhusu Moabu. 14  Na sasa Yehova anasema: “Katika kipindi cha miaka tatu (3), kama miaka ya mufanyakazi wa kulipwa,* utukufu wa Moabu utapatishwa haya kwa muvurugo mwingi wa kila namna, na wale wenye watabakia watakuwa kidogo sana na wa hali ya chini.”+

Maelezo ya Chini

Ao “nyumba yake; kiota chake.”
Ao “eko.”
Ao “matawi yake yenye kujaa zabibu nyekundu.”
Ao pengine, “Kwa sababu mulio wa vita umekuja juu ya matunda yako ya kipindi cha joto na juu ya mavuno yako.”
Ao “yenye kuhesabiwa kwa uangalifu kama vile mufanyakazi wa kulipwa anafanya”; ni kusema, kwa miaka 3 kamili.