Isaya 16:1-14
-
Ujumbe juu ya Moabu unaendelea (1-14)
16 Mutume kondoo-dume kwa mutawala wa inchi,Kutoka Sela kupitia jangwa,Mupaka kwenye mulima wa binti ya Sayuni.
2 Kama ndege mwenye alifukuzwa katika chicha yake,*+Ni vile mabinti wa Moabu watakuwa kwenye nafasi za kuvukia za Arnoni.+
3 “Mutoe shauri, mutimize uamuzi.
Fanya kivuli chako cha katikati ya muchana kikuwe kama usiku.
Ficha wenye walisambazwa na usitoe wale wenye kukimbia.
4 Acha watu wangu wenye walisambazwa wakae ndani yako, Ee Moabu.
Ukuwe mahali pao pa kujificha kwa sababu ya mwenye kuharibu.+
Mukandamizaji atafikia mwisho wake,Uharibifu utafikia mwisho,Na wale wenye kukanyanga-kanyanga wengine wataharibiwa kutoka katika dunia.
5 Kisha kiti cha ufalme kitafanywa kuwa imara kabisa katika upendo mushikamanifu.
Ule mwenye kukiikalia katika hema ya Daudi atakuwa muaminifu;+Atahukumu kwa haki na atatenda haraka uadilifu.”*+
6 Tumesikia kuhusu kiburi cha Moabu—iko* na kiburi sana+—Majivuno yake na kiburi chake na kasirani yake kali;+Lakini maneno yake yenye hayana maana yataisha.
7 Basi Moabu atamuombolezea Moabu;Wote wataomboleza.+
Wale wenye walipigwa wataomboleza kwa sababu ya keki za zabibu za Kir-hareseti.+
8 Kwa maana matuta ya Heshboni+ yamekauka.
Muzabibu wa Sibma,+Watawala wa mataifa wamekanyanga-kanyanga matawi yake mekundu yenye kungaa;*Walikuwa wamefika mupaka Yazeri;+Walikuwa wameenea mupaka katika jangwa.
Machipukizi yake yalikuwa yameenea na kufika mupaka katika bahari.
9 Ndiyo sababu nitalilia muzabibu wa Sibma kama vile ninalilia Yazeri.
Machozi yangu yatakulowanisha, Ee Heshboni na Eleale,+Kwa kuwa kupiga vigelegele kwa sababu ya matunda yako ya kipindi cha joto na mavuno yako kumeisha.*
10 Shangwe na furaha zimeondolewa katika shamba la matunda,Na hakuna nyimbo za furaha ao kupiga vigelegele katika mashamba ya mizabibu.+
Mwenye kukanyanga hakanyange tena divai katika chombo cha kukamulia divai.
Kwa maana nimefanya vigelegele vimalizike.+
11 Ndiyo sababu niko na musukosuko ndani yangu kuhusu Moabu,+Kama wakati kinubi kinapigwa,Na utu wangu wa ndani sana kuhusu Kir-hareseti.+
12 Hata kama Moabu anajichokesha kwenye mahali pa juu na kuenda kusali katika patakatifu pake, hatatimiza kitu chochote.+
13 Hili ndilo neno lenye Yehova alisema zamani kuhusu Moabu.
14 Na sasa Yehova anasema: “Katika kipindi cha miaka tatu (3), kama miaka ya mufanyakazi wa kulipwa,* utukufu wa Moabu utapatishwa haya kwa muvurugo mwingi wa kila namna, na wale wenye watabakia watakuwa kidogo sana na wa hali ya chini.”+
Maelezo ya Chini
^ Ao “nyumba yake; kiota chake.”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “eko.”
^ Ao “matawi yake yenye kujaa zabibu nyekundu.”
^ Ao pengine, “Kwa sababu mulio wa vita umekuja juu ya matunda yako ya kipindi cha joto na juu ya mavuno yako.”
^ Ao “yenye kuhesabiwa kwa uangalifu kama vile mufanyakazi wa kulipwa anafanya”; ni kusema, kwa miaka 3 kamili.

