Isaya 56:1-12
56 Yehova anasema hivi:
“Mushike haki,+ na mutende uadilifu,*Kwa maana wokovu wangu utakuja hivi karibuniNa haki yangu itafunuliwa.+
2 Mwenye furaha ni mutu mwenye anafanya jambo hiliNa mwana wa binadamu mwenye anaendelea kulishika,Mwenye anashika Sabato na haichafue,+Na mwenye anazuia mukono wake usitende namna yoyote ya uovu.
3 Mugeni mwenye anajiunga na Yehova+ hapaswe kusema,‘Hakika Yehova atanitenga na watu wake.’
Na towashi hapaswe kusema, ‘Angalia! Niko muti wenye kukauka.’”
4 Kwa maana Yehova anaambia hivi matowashi wenye kushika sabato zangu na wenye kuchagua mambo yenye kunipendeza na wenye kushika agano langu:
5 “Nitawapatia munara na jina katika nyumba yangu na katika kuta zangu,Jambo la muzuri kuliko watoto wanaume na watoto wanamuke.
Nitawapatia jina lenye kudumu,Lenye halitaangamia.
6 Kuhusu wageni wenye kujiunga na Yehova ili kumutolea utumishiIli kupenda jina la Yehova+Na kuwa watumishi wake,Wale wote wenye kushika Sabato na hawaichafueNa wenye kushika agano langu,
7 Pia nitawaleta kwenye mulima wangu mutakatifu+Na kuwafanya washangilie ndani ya nyumba yangu ya sala.
Matoleo yao mazima ya kuteketezwa na zabihu zao zitakubaliwa kwenye mazabahu yangu.
Kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya vikundi vyote vya watu.”+
8 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, mwenye anakusanya wenye walisambazwa wa Israeli,+ anasema:
“Nitakusanya wengine kwake zaidi ya wale wenye tayari wamekusanywa.”+
9 Ninyi wote wanyama wa pori, mukuje mukule,Ninyi wote wanyama wa pori wenye kuwa katika pori.+
10 Walinzi wake ni vipofu,+ hakuna hata mumoja mwenye ameona.+
Wote ni imbwa wenye kuwa bubu, hawawezi kufoka.+
Wanapumua haraka-haraka na kulala chini; wanapenda kusinzia.
11 Wao ni imbwa wenye hamu kubwa ya kula;*Hawashibe hata kidogo.
Wao ni wachungaji wenye hawana uelewaji.+
Wote wamefuata njia yao wenyewe;Kila mumoja wao anatafuta faida yenye haiko ya haki na kusema:
12 “Mukuje, nikamate divai,Na tukunywe pombe nyingi.+
Na kesho itakuwa kama leo, hata muzuri zaidi!”

