Isaya 28:1-29
28 Ole wake taji* lenye kujionyesha* la walevi wa Efraimu+Na ua lenye kufifia la uzuri wake wenye utukufu,Lenye kuwa kwenye kichwa cha bonde lenye mbolea la wale wenye wamelemewa na divai!
2 Angalia! Yehova iko* na mutu mwenye nguvu na mwenye uwezo.
Kama upepo wa mvua ya majiwe wenye mungurumo wa radi, zoruba yenye upepo mukali yenye kuharibu,Kama zoruba yenye mungurumo wa maji ya garika yenye nguvu,Atalitupa katika dunia kwa nguvu.
3 Mataji yenye kujionyesha* ya walevi wa EfraimuYatakanyangiwa chini kwa miguu.+
4 Na ua lenye kufifia la uzuri wake wenye utukufuLenye kuwa juu ya kichwa cha bonde lenye mbolea,Litakuwa kama tini ya kwanza-kwanza mbele ya kipindi cha joto.
Wakati mutu anaiona, anaimeza wakati tu inakuwa katika mukono wake.
5 Siku hiyo Yehova wa majeshi atakuwa taji la utukufu na taji la muzuri la maua kwa watu wake wenye walibakia.+
6 Na atakuwa roho ya haki kwa ule mwenye kukaa katika hukumu na chanzo cha nguvu kwa wale wenye kuzuia mashambulizi kwenye mulango mukubwa.+
7 Na hawa pia wanapotea kwa sababu ya divai;Wanayumba-yumba kwa sababu ya vinywaji vyao vyenye kulewesha.
Kuhani na nabii wanapotea kwa sababu ya pombe;Divai inawavuruga,Na wanayumba-yumba kwa sababu ya pombe yao;Maono yao yanafanya wapotee,Na wanajikwaa katika hukumu.+
8 Kwa maana meza zao zimejaa matapiko machafu—Yamejaa kila mahali.
9 Mutu atamufundisha nani ujuzi,Na mutu atamufasiria nani ujumbe?
Je, ni wale wenye wametoka tu kuachishwa kunyonya,Wale wenye wametoka tu kuondolewa kwenye maziwa?
10 Kwa maana ni “amri kisha amri, amri kisha amri,Mustari kwa mustari, mustari kwa mustari,*+Hapa kidogo, pale kidogo.”
11 Kwa hiyo atasema na watu hawa kupitia wale wenye kigugumizi* na kupitia luga ya kigeni.+
12 Alikuwa amewaambia: “Hapa ndipo mahali pa kupumuzikia. Mwenye kuchoka apumuzike; hapa ndipo mahali pa kujiburudishia,” lakini walikataa kusikiliza.+
13 Basi neno la Yehova litakuwa kwao:
“Amri kisha amri, amri kisha amri,Mustari kwa mustari, mustari kwa mustari,*+Hapa kidogo, pale kidogo,”Ili wakati wanatembea,Wajikwae na kuangukia nyumaNa wavunjike na kunaswa na kukamatwa.+
14 Basi musikie neno la Yehova, ninyi wenye kujisifuNinyi watawala wa watu hawa wenye kuwa katika Yerusalemu,
15 Kwa maana munasema:
“Tumefanya agano pamoja na Kifo,+Na tumefanya mapatano* pamoja na Kaburi.*
Wakati mafuriko yenye nguvu na ya kushitukia yatapita,Hayatatufikia,Kwa maana tumefanya uongo kuwa kimbilio letuNa tumejificha katika udanganyifu.”+
16 Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
“Angalia, ninaweka katika Sayuni jiwe lenye limejaribiwa ili likuwe musingi,+Jiwe la pembe lenye samani+ la musingi imara.+
Kila mutu mwenye anaonyesha imani hataogopa.+
17 Na nitafanya haki kuwa kamba ya kupimia+Na uadilifu* kuwa kifaa cha kusawazisha;*+Na mvua ya majiwe itaharibu kimbilio la uongo,Na maji yatazamisha mahali pa kujificha.
18 Agano lenu pamoja na Kifo litavunjwa,Na mapatano yenu pamoja na Kaburi* hayatasimama.+
Wakati mafuriko yenye nguvu na ya kushitukia yatapita,Yatawaponda ninyi.
19 Kila mara wakati yatapita,Yatawafagilia ninyi mbali;+Kwa maana yatapita asubui kisha asubui,Muchana na usiku.
Woga mukubwa ndio utawafanya waelewe kile chenye kilisikiwa.”*
20 Kwa maana kitanda ni kifupi sana, mutu hawezi kujinyoosha juu yake,Na kitu cha kujifunika chenye kusukwa ni chembamba, hakiwezi kumufunika mutu.
21 Kwa maana Yehova atasimama kama kwenye Mulima Perasimu,Atainuka kama katika bonde* lenye kuwa karibu na Gibeoni,+Ili afanye tendo lake—tendo lake la ajabu—Na ili afanye kazi yake—kazi yake yenye haiko ya kawaida.+
22 Sasa musifanye zihaka,+Ili vifungo vyenu visikazwe zaidi,Kwa maana nimesikia kutoka kwa Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi,Kwamba uharibifu umeamuliwa kwa ajili ya inchi yote.*+
23 Mutege sikio na musikilize sauti yangu;Mukaze uangalifu na musikilize kile ninasema.
24 Je, mulimaji anaendelea kulima muchana wote mbele ya kupanda mbegu?
Je, anaendelea kuchimbua na kuvunja udongo wake?+
25 Wakati amesawazisha udongo,Je, hatawanye bizari nyeusi na kupanda bizari,Na je, hapande ngano, mutama, na shayiri mahali pake,Na ngano ya kusemeti+ kwenye mipaka?
26 Kwa maana Yeye anamufundisha* njia yenye kufaa;Mungu wake anamufundisha.+
27 Kwa maana bizari nyeusi haisagwe kwa kifaa cha kupiga-piga nafaka;+Na gurudumu* la gari la kukokotwa halizungushwe juu ya bizari.
Lakini, bizari nyeusi inapigwa-pigwa kwa fimbo,Na bizari kwa fimbo.
28 Je, mutu anaponda nafaka ili apate mukate?
Hapana, haendelee kuipiga-piga.+
Na wakati anazungusha gurudumu* la gari lake la kukokotwa juu yake akiwa na farasi zake,Yeye haiponde.+
29 Na mambo hayo pia yanatoka kwa Yehova wa majeshi,Mwenye shauri* lake ni la ajabu,Na mwenye ametimiza mambo makubwa.*+
Maelezo ya Chini
^ Inaonekana ni muji mukubwa, Samaria.
^ Ao “lenye majivuno; lenye kiburi.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “yenye majivuno; yenye kiburi.”
^ Ao “Kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia.”
^ Tnn., “wale wenye mudomo wenye kugugumiza.”
^ Ao “Kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia.”
^ Ao pengine “Tumetimiza maono.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “timazi.” Timazi ni kamba yenye kufungiwa kitu kizito ambayo ilitumiwa ili kupima usawa.
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao pengine, “Wakati wataelewa, watasikia woga mukubwa sana.”
^ Ao “eneo tambarare la chini.”
^ Ao “kwa ajili ya dunia yote.”
^ Ao “anamutia nizamu; anamupatia azabu.”
^ Ao “mupeto; pneu.”
^ Ao “mupeto; pneu.”
^ Ao “kusudi.”
^ Ao “mwenye hekima yake yenye kutumika ni kubwa.”