Isaya 29:1-24

  • Ole wake Arieli! (1-16)

    • Heshima ya midomo tu inalaumiwa (13)

  • Viziwi watasikia; na vipofu wataona (17-24)

29  “Ole wake Arieli,* Arieli, muji kwenye Daudi alipiga kambi!+ Endelea mwaka kwa mwaka;Muzunguko wa sikukuu+ uendelee.  2  Lakini nitaleta taabu juu ya Arieli,+Na kutakuwa kilio na maombolezo,+Na atakuwa kwangu kama jiko la mazabahu ya Mungu.+  3  Nitapiga kambi pande zote juu yako,Na nitakuzunguka kwa ajili ya vita kupitia lupango ya mitiNa kusimamisha juu yako vitu vya kutumia ili kuzunguka kwa ajili ya vita.+  4  Utashushwa;Utazungumuza ukiwa katika udongo,Na mavumbi yatafanya mambo yenye utasema yasisikike muzuri. Sauti yako itatoka katika udongo+Kama sauti ya mutu mwenye kupashana habari na pepo wachafu,Na maneno yako yatatoka katika mavumbi kama sauti ya ndege.  5  Kikundi cha maadui* wako kitakuwa kama unga laini,+Kikundi cha watu wenye kuonea kama vile maganda ya mbegu yenye kupeperuka.+ Na itatokea mara moja, bila kutazamia.+  6  Yehova wa majeshi atawakazia uangalifuKwa mungurumo na tetemeko la inchi na makelele makubwa,Kwa upepo wa zoruba na zoruba kali na miali ya moto wenye kuteketeza.”+  7  Kisha kikundi cha watu wa mataifa yote yenye kupigana vita na Arieli,+⁠—​Wale wote wenye kupigana vita naye,Minara ya kumuzunguka kwa ajili ya vitaNa wale wenye kumuletea taabu⁠—Watakuwa kama ndoto, maono ya usiku.  8  Ndiyo, itakuwa kama vile wakati mutu mwenye njaa anaota ndoto kwamba anakula,Lakini anaamuka akiwa na njaa,*Na kama vile wakati mutu mwenye kiu anaota ndoto kwamba anakunywa,Lakini anaamuka akiwa amechoka na akiwa na kiu.* Ni vile itakuwa kwa kikundi cha watu wa mataifa yoteYenye kupigana vita na Mulima Sayuni.+  9  Mushituke na kushangaa sana;+Mujifanye kuwa vipofu na mukuwe vipofu.+ Wamelewa, lakini haiko kwa sababu ya divai;Wanayumba-yumba, lakini haiko kwa sababu ya pombe. 10  Kwa maana Yehova amemwanga juu yenu roho ya usingizi muzito;+Na amefunga macho yenu, manabii,+Na amefunika vichwa vyenu, waonaji.+ 11  Maono yote yamekuwa kwenu kama maneno ya kitabu chenye kimefungwa kwa muhuri.+ Wakati wanakipatia mutu mwenye anajua kusoma, na kusema: “Tafazali, soma kitabu hiki kwa sauti,” atasema: “Siwezi, kwa maana kimefungwa kwa muhuri.” 12  Na wakati wanamupatia kile kitabu mutu mwenye hajue kusoma, na kusema: “Tafazali, soma kitabu hiki kwa sauti,” atasema: “Sijue kusoma hata kidogo.” 13  Yehova anasema: “Watu hawa wananikaribia kwa vinywa vyao,Na wananiheshimia kwa midomo yao,+Lakini moyo wao uko mbali sana na mimi,Na wananiogopa kwa kutegemea amri za wanadamu zenye wamefundishwa.+ 14  Kwa hiyo, mimi ndiye nitatendea tena watu hawa mambo ya ajabu,+Kwa jambo la ajabu juu ya jambo la ajabu;Na hekima ya watu wao wenye hekima itaangamia,Na uelewaji wa watu wao wenye busara utafichwa.”+ 15  Ole wao wale wenye wanafanya yao yote ili kumuficha Yehova mipango yao.*+ Matendo yao yanafanywa mahali kwenye giza,Wakati huohuo wanasema: “Ni nani anatuona? Ni nani anajua habari juu yetu?”+ 16  Munageuza mambo kabisa!* Je, mufinyanzi* anapaswa kuonwa kuwa sawa na udongo?+ Je, kitu chenye kilitengenezwa kinapaswa kusema kuhusu ule mwenye alikitengeneza: “Hakunitengeneza”?+ Na je, kitu chenye kilitengenezwa kitasema hivi kuhusu ule mwenye alikitengeneza: “Hana uelewaji”?+ 17  Kwa wakati mufupi tu Lebanoni itageuzwa kuwa shamba la matunda,+Na shamba hilo la matunda litaonwa kuwa pori.+ 18  Siku hiyo viziwi watasikia maneno ya kitabu,Na kutoka katika weusi na giza macho ya vipofu yataona.+ 19  Wapole watashangilia sana katika Yehova,Na maskini kati ya watu watafurahi katika Mutakatifu wa Israeli.+ 20  Kwa maana mutu mwenye kuonea hatakuwa tena,Mwenye kujisifu atafikia mwisho wake,Na wale wote wenye kukaa macho ili kuumiza wengine wataharibiwa,+ 21  Wale wenye kwa neno la uongo wanafanya wengine wakuwe na hatia,Wenye wanatega mutego kwa ajili ya ule muteteaji* kwenye mulango mukubwa wa muji,+Na wale wenye wanaima haki mwenye haki kwa kutumia sababu zenye hazina musingi.+ 22  Basi Yehova, mwenye alimukomboa Abrahamu,+ anaambia nyumba ya Yakobo hivi: “Yakobo hatapata haya tena,Na uso wake hautabadilika rangi tena.*+ 23  Kwa maana wakati ataona watoto wake,Wenye ni kazi ya mikono yake, katikati yake,+Watatakasa jina langu;Ndiyo, watamutakasa Mutakatifu wa Yakobo,Na watamuogopa sana Mungu wa Israeli.+ 24  Wale wenye kupotoka katika roho watapata uelewaji,Na wale wenye kunungunika watakubali mafundisho.”

Maelezo ya Chini

Pengine inamaanisha “Jiko la Mazabahu ya Mungu,” inaonekana ni Yerusalemu.
Tnn., “wageni.”
Ao “na nafsi yake haina kitu.”
Ao “na nafsi yake imekauka.”
Ao “shauri lao.”
Ao “Muko waovu kabisa!”
Tnn., “mwenye kukaripia.”
Ni kusema, kwa sababu ya haya na kuvunjika moyo.