Isaya 29:1-24
29 “Ole wake Arieli,* Arieli, muji kwenye Daudi alipiga kambi!+
Endelea mwaka kwa mwaka;Muzunguko wa sikukuu+ uendelee.
2 Lakini nitaleta taabu juu ya Arieli,+Na kutakuwa kilio na maombolezo,+Na atakuwa kwangu kama jiko la mazabahu ya Mungu.+
3 Nitapiga kambi pande zote juu yako,Na nitakuzunguka kwa ajili ya vita kupitia lupango ya mitiNa kusimamisha juu yako vitu vya kutumia ili kuzunguka kwa ajili ya vita.+
4 Utashushwa;Utazungumuza ukiwa katika udongo,Na mavumbi yatafanya mambo yenye utasema yasisikike muzuri.
Sauti yako itatoka katika udongo+Kama sauti ya mutu mwenye kupashana habari na pepo wachafu,Na maneno yako yatatoka katika mavumbi kama sauti ya ndege.
5 Kikundi cha maadui* wako kitakuwa kama unga laini,+Kikundi cha watu wenye kuonea kama vile maganda ya mbegu yenye kupeperuka.+
Na itatokea mara moja, bila kutazamia.+
6 Yehova wa majeshi atawakazia uangalifuKwa mungurumo na tetemeko la inchi na makelele makubwa,Kwa upepo wa zoruba na zoruba kali na miali ya moto wenye kuteketeza.”+
7 Kisha kikundi cha watu wa mataifa yote yenye kupigana vita na Arieli,+—Wale wote wenye kupigana vita naye,Minara ya kumuzunguka kwa ajili ya vitaNa wale wenye kumuletea taabu—Watakuwa kama ndoto, maono ya usiku.
8 Ndiyo, itakuwa kama vile wakati mutu mwenye njaa anaota ndoto kwamba anakula,Lakini anaamuka akiwa na njaa,*Na kama vile wakati mutu mwenye kiu anaota ndoto kwamba anakunywa,Lakini anaamuka akiwa amechoka na akiwa na kiu.*
Ni vile itakuwa kwa kikundi cha watu wa mataifa yoteYenye kupigana vita na Mulima Sayuni.+
9 Mushituke na kushangaa sana;+Mujifanye kuwa vipofu na mukuwe vipofu.+
Wamelewa, lakini haiko kwa sababu ya divai;Wanayumba-yumba, lakini haiko kwa sababu ya pombe.
10 Kwa maana Yehova amemwanga juu yenu roho ya usingizi muzito;+Na amefunga macho yenu, manabii,+Na amefunika vichwa vyenu, waonaji.+
11 Maono yote yamekuwa kwenu kama maneno ya kitabu chenye kimefungwa kwa muhuri.+ Wakati wanakipatia mutu mwenye anajua kusoma, na kusema: “Tafazali, soma kitabu hiki kwa sauti,” atasema: “Siwezi, kwa maana kimefungwa kwa muhuri.”
12 Na wakati wanamupatia kile kitabu mutu mwenye hajue kusoma, na kusema: “Tafazali, soma kitabu hiki kwa sauti,” atasema: “Sijue kusoma hata kidogo.”
13 Yehova anasema: “Watu hawa wananikaribia kwa vinywa vyao,Na wananiheshimia kwa midomo yao,+Lakini moyo wao uko mbali sana na mimi,Na wananiogopa kwa kutegemea amri za wanadamu zenye wamefundishwa.+
14 Kwa hiyo, mimi ndiye nitatendea tena watu hawa mambo ya ajabu,+Kwa jambo la ajabu juu ya jambo la ajabu;Na hekima ya watu wao wenye hekima itaangamia,Na uelewaji wa watu wao wenye busara utafichwa.”+
15 Ole wao wale wenye wanafanya yao yote ili kumuficha Yehova mipango yao.*+
Matendo yao yanafanywa mahali kwenye giza,Wakati huohuo wanasema: “Ni nani anatuona?
Ni nani anajua habari juu yetu?”+
16 Munageuza mambo kabisa!*
Je, mufinyanzi* anapaswa kuonwa kuwa sawa na udongo?+
Je, kitu chenye kilitengenezwa kinapaswa kusema kuhusu ule mwenye alikitengeneza:
“Hakunitengeneza”?+
Na je, kitu chenye kilitengenezwa kitasema hivi kuhusu ule mwenye alikitengeneza:
“Hana uelewaji”?+
17 Kwa wakati mufupi tu Lebanoni itageuzwa kuwa shamba la matunda,+Na shamba hilo la matunda litaonwa kuwa pori.+
18 Siku hiyo viziwi watasikia maneno ya kitabu,Na kutoka katika weusi na giza macho ya vipofu yataona.+
19 Wapole watashangilia sana katika Yehova,Na maskini kati ya watu watafurahi katika Mutakatifu wa Israeli.+
20 Kwa maana mutu mwenye kuonea hatakuwa tena,Mwenye kujisifu atafikia mwisho wake,Na wale wote wenye kukaa macho ili kuumiza wengine wataharibiwa,+
21 Wale wenye kwa neno la uongo wanafanya wengine wakuwe na hatia,Wenye wanatega mutego kwa ajili ya ule muteteaji* kwenye mulango mukubwa wa muji,+Na wale wenye wanaima haki mwenye haki kwa kutumia sababu zenye hazina musingi.+
22 Basi Yehova, mwenye alimukomboa Abrahamu,+ anaambia nyumba ya Yakobo hivi:
“Yakobo hatapata haya tena,Na uso wake hautabadilika rangi tena.*+
23 Kwa maana wakati ataona watoto wake,Wenye ni kazi ya mikono yake, katikati yake,+Watatakasa jina langu;Ndiyo, watamutakasa Mutakatifu wa Yakobo,Na watamuogopa sana Mungu wa Israeli.+
24 Wale wenye kupotoka katika roho watapata uelewaji,Na wale wenye kunungunika watakubali mafundisho.”
Maelezo ya Chini
^ Pengine inamaanisha “Jiko la Mazabahu ya Mungu,” inaonekana ni Yerusalemu.
^ Tnn., “wageni.”
^ Ao “na nafsi yake haina kitu.”
^ Ao “na nafsi yake imekauka.”
^ Ao “shauri lao.”
^ Ao “Muko waovu kabisa!”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Tnn., “mwenye kukaripia.”
^ Ni kusema, kwa sababu ya haya na kuvunjika moyo.