Isaya 27:1-13

  • Yehova anaua Leviatani (1)

  • Wimbo kuhusu Israeli akiwa shamba la mizabibu (2-13)

27  Siku hiyo Yehova, akiwa na upanga wake mukali na mukubwa na wenye nguvu,+Atamuelekezea uangalifu Leviatani,* ule nyoka mwenye kuenda mbio kwa kutereza,Leviatani, ule nyoka mwenye kujiviringa-viringa,Na ataua munyama mukubwa mwenye kuwa katika bahari.  2  Siku hiyo mumuimbie ule mwanamuke:* “Shamba la mizabibu la divai yenye kutoa pofu!+  3  Mimi, Yehova, ninamulinda.+ Kila wakati ninamumwangilia maji.+ Ninamulinda usiku na muchana,Ili mutu yeyote asimuumize.+  4  Hakuna kasirani kali ndani yangu.+ Ni nani atapambana na mimi katika vita kwa kutumia miti midogo-midogo ya miiba na magugu? Nitavikanyanga-kanyanga na kuvichoma moto vyote pamoja.  5  Kama haiko vile, acha ashike kwa nguvu ngome yangu,Afanye amani pamoja na mimi;Amani aifanye pamoja na mimi.”  6  Katika siku zenye kuja Yakobo atatia mizizi,Israeli atatoa maua na kuchipuka,+Na watajaza mazao katika inchi.+  7  Je, lazima apigwe kwa pigo la ule mwenye kumupiga? Ao, je, lazima auawe kwa mauaji kama ya watu wake wenye waliuawa?  8  Utashindana naye kwa mulio wa kushitua wakati utakuwa unamufukuza. Atamufukuza kwa mulipuko wake mukali katika siku ya upepo wa mashariki.+  9  Basi kwa njia hii kosa la Yakobo litafunikwa,+Na mazao kamili wakati zambi yake itaondolewa yatakuwa haya: Atafanya majiwe yote ya mazabahuYakuwe kama majiwe ya chokaa yenye imepondwa,Na hakuna miti mitakatifu* ao vinara vya uvumba vyenye vitabakia.+ 10  Kwa maana muji wenye ngome utaachwa,Malisho yataachwa na kubakia kama jangwa.+ Kitoto-dume cha ngombe kitakulia majani pale na kulala paleNa kitakula matawi yake.+ 11  Wakati matawi yake yatakuwa yamekauka,Wanamuke watakuja kuyavunja,Na kuwasha nayo moto. Kwa maana watu hawa hawana uelewaji.+ Ndiyo sababu Mutengenezaji wao hatawaonyesha rehema,Na Ule mwenye aliwafanya hatawaonyesha wema.+ 12  Siku hiyo Yehova atapiga-piga matunda kuanzia muto mudogo wenye kutiririka wa ule Muto* mupaka kwenye Bonde la Muto* la Misri,+ na ninyi mutakusanywa mumoja kisha mwingine, Enyi watu wa Israeli.+ 13  Siku hiyo baragumu kubwa itapigwa,+ na wale wenye kuangamia katika inchi ya Ashuru+ na wale wenye walitawanyika katika inchi ya Misri+ watakuja na kumuinamia Yehova kwenye mulima mutakatifu katika Yerusalemu.+

Maelezo ya Chini

Inaonekana ni Israeli, hapa inazungumuziwa kama mwanamuke na kufananishwa na shamba la mizabibu.
Ni kusema, Efrati.