Isaya 27:1-13
27 Siku hiyo Yehova, akiwa na upanga wake mukali na mukubwa na wenye nguvu,+Atamuelekezea uangalifu Leviatani,* ule nyoka mwenye kuenda mbio kwa kutereza,Leviatani, ule nyoka mwenye kujiviringa-viringa,Na ataua munyama mukubwa mwenye kuwa katika bahari.
2 Siku hiyo mumuimbie ule mwanamuke:*
“Shamba la mizabibu la divai yenye kutoa pofu!+
3 Mimi, Yehova, ninamulinda.+
Kila wakati ninamumwangilia maji.+
Ninamulinda usiku na muchana,Ili mutu yeyote asimuumize.+
4 Hakuna kasirani kali ndani yangu.+
Ni nani atapambana na mimi katika vita kwa kutumia miti midogo-midogo ya miiba na magugu?
Nitavikanyanga-kanyanga na kuvichoma moto vyote pamoja.
5 Kama haiko vile, acha ashike kwa nguvu ngome yangu,Afanye amani pamoja na mimi;Amani aifanye pamoja na mimi.”
6 Katika siku zenye kuja Yakobo atatia mizizi,Israeli atatoa maua na kuchipuka,+Na watajaza mazao katika inchi.+
7 Je, lazima apigwe kwa pigo la ule mwenye kumupiga?
Ao, je, lazima auawe kwa mauaji kama ya watu wake wenye waliuawa?
8 Utashindana naye kwa mulio wa kushitua wakati utakuwa unamufukuza.
Atamufukuza kwa mulipuko wake mukali katika siku ya upepo wa mashariki.+
9 Basi kwa njia hii kosa la Yakobo litafunikwa,+Na mazao kamili wakati zambi yake itaondolewa yatakuwa haya:
Atafanya majiwe yote ya mazabahuYakuwe kama majiwe ya chokaa yenye imepondwa,Na hakuna miti mitakatifu* ao vinara vya uvumba vyenye vitabakia.+
10 Kwa maana muji wenye ngome utaachwa,Malisho yataachwa na kubakia kama jangwa.+
Kitoto-dume cha ngombe kitakulia majani pale na kulala paleNa kitakula matawi yake.+
11 Wakati matawi yake yatakuwa yamekauka,Wanamuke watakuja kuyavunja,Na kuwasha nayo moto.
Kwa maana watu hawa hawana uelewaji.+
Ndiyo sababu Mutengenezaji wao hatawaonyesha rehema,Na Ule mwenye aliwafanya hatawaonyesha wema.+
12 Siku hiyo Yehova atapiga-piga matunda kuanzia muto mudogo wenye kutiririka wa ule Muto* mupaka kwenye Bonde la Muto* la Misri,+ na ninyi mutakusanywa mumoja kisha mwingine, Enyi watu wa Israeli.+
13 Siku hiyo baragumu kubwa itapigwa,+ na wale wenye kuangamia katika inchi ya Ashuru+ na wale wenye walitawanyika katika inchi ya Misri+ watakuja na kumuinamia Yehova kwenye mulima mutakatifu katika Yerusalemu.+
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Inaonekana ni Israeli, hapa inazungumuziwa kama mwanamuke na kufananishwa na shamba la mizabibu.
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ni kusema, Efrati.
^ Angalia Maana ya Maneno.