Yeremia 7:1-34

  • Tumaini la uongo katika hekalu la Yehova (1-11)

  • Hekalu litakuwa kama Shilo (12-15)

  • Ibada ya kidesturi inahukumiwa (16-34)

    • “Malkia wa Mbinguni” anaabudiwa (18)

    • Kutoa watoto kuwa zabihu katika Hinomu (31)

7  Hili ndilo neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema: 2  “Simama katika mulango mukubwa wa nyumba ya Yehova na utangaze pale ujumbe huu, ‘Musikie neno la Yehova, ninyi wote watu wa Yuda wenye munaingia katika milango hii mikubwa ili kumuinamia Yehova. 3  Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Mubadilishe njia zenu na matendo yenu, na nitawaruhusu muendelee kukaa mahali hapa.+ 4  Musiweke tegemeo lenu katika maneno ya udanganyifu na kusema, ‘Hili ni* hekalu la Yehova, hekalu la Yehova, hekalu la Yehova!’+ 5  Kwa maana kama kwa kweli munabadilisha njia zenu na matendo yenu; kama kwa kweli munatenda haki kati ya mutu na jirani yake;+ 6  kama hamukandamize wakaaji wageni, mayatima,* na wajane;+ kama hamumwange damu yenye haina kosa mahali hapa; na kama hamufuate miungu mingine na kujiletea maumivu ninyi wenyewe;+ 7  basi nitawaruhusu muendelee kukaa mahali hapa, katika inchi yenye nilipatia mababu zenu kwa wakati wote.”’”* 8  “Lakini munaweka tegemeo lenu katika maneno ya udanganyifu+⁠—​jambo hilo halitaleta faida yoyote hata kidogo. 9  Je, munaweza kuiba,+ kuua, kufanya uzinifu, kuapa kwa uongo,+ kumutolea Baali zabihu,*+ na kufuata miungu yenye hamukujua, 10  na kisha mukuje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii yenye kubeba jina langu na kusema, ‘Tutaokolewa,’ hata kama munafanya mambo haya yote yenye kuchukiza? 11  Je, nyumba hii yenye kubeba jina langu imekuwa pango la wanyanganyi mbele ya macho yenu?+ Muangalie, nimejionea jambo hilo,” ni vile Yehova anasema. 12  “‘Hata hivyo, sasa muende mahali pangu katika Shilo,+ kwenye pale mwanzo nilifanya jina langu likae,+ na muone kile nilipafanyia kwa sababu ya ubaya wa watu wangu Israeli.+ 13  Lakini muliendelea kufanya mambo hayo yote,’ ni vile Yehova anasema, ‘na hata kama nilisema na ninyi tena na tena,* hamukusikiliza.+ Niliendelea kuwaita ninyi, lakini hamukujibu.+ 14  Ni vile nitatendea nyumba yenye kubeba jina langu,+ yenye munategemea,+ na mahali hapa kwenye niliwapatia ninyi na mababu zenu, kama vile nilitendea Shilo.+ 15  Nitawatupa ninyi kutoka mbele ya macho yangu, kama vile nilitupa ndugu zenu wote, wazao wote wa Efraimu.’+ 16  “Na wewe, usisali kwa ajili ya watu hawa. Usilie kwa sauti kubwa ao kutoa sala ao kuniomba kwa ajili yao,+ kwa maana sitakusikiliza.+ 17  Je, hauone mambo yenye wanafanya katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu? 18  Wana wanakusanya kuni, baba wanawasha moto, na bibi wanaponda unga ili kumutengenezea Malkia wa Mbinguni* keki za zabihu,+ na wanamwangia miungu mingine matoleo ya kinywaji ili kunikasirisha.+ 19  ‘Lakini je, ni mimi ndiye wanaumiza?’* ni vile Yehova anasema. ‘Je, hawajiumize wao wenyewe, kwa haya yao wenyewe?’+ 20  Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘Angalia! Hasira yangu na kasirani yangu kali zitamwangwa juu ya mahali hapa,+ juu ya mwanadamu na munyama, juu ya miti ya shamba na mazao ya udongo; itateketeza na haitazimishwa.’+ 21  “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Muendelee, muongeze matoleo yenu mazima ya kuteketezwa kwenye zabihu zenu zingine, na mukule nyama ninyi wenyewe.+ 22  Kwa maana katika siku yenye nilitosha mababu zenu katika inchi ya Misri, sikusema nao ao kuwaamuru juu ya matoleo mazima ya kuteketezwa na zabihu.+ 23  Lakini niliwapatia amri hii: “Mutii sauti yangu, na nitakuwa Mungu wenu, na ninyi mutakuwa watu wangu.+ Munapaswa kutembea katika njia yote yenye ninaamuru, ili mambo yakuwe muzuri kwenu.”’+ 24  Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao;+ tofauti na hilo, walitembea katika mipango yao ya mubaya,* na kwa kichwa-nguvu walifuata moyo wao muovu,+ na wakarudia nyuma, hawakuenda mbele, 25  tangu siku yenye mababu zenu walitoka katika inchi ya Misri mupaka leo hii.+ Basi nikaendelea kutuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nikiwatuma kila siku, tena na tena.*+ 26  Lakini walikataa kunisikiliza, na hawakutega sikio lao.+ Tofauti na hilo, walikuwa kichwa-nguvu,* na wakatenda mubaya zaidi kuliko mababu zao! 27  “Utawaambia maneno haya yote,+ lakini hawatakusikiliza; utawaita, lakini hawatakujibu. 28  Na utawaambia, ‘Hili ndilo taifa lenye halikutii sauti ya Yehova Mungu wao na walikataa kukubali nizamu. Uaminifu umeangamia na hata hautajwe kati yao.’*+ 29  “Nyoa nywele zako zenye hazijakatwa* na kuzitupa mbali, na uimbe wimbo wa huzuni* juu ya vilima vyenye kuwa wazi, kwa maana Yehova amekataa na ataacha kizazi hiki chenye kimemukasirisha sana. 30  ‘Kwa maana watu wa Yuda wamefanya mambo ya mubaya mbele ya macho yangu,’ ni vile Yehova anasema. ‘Wameweka sanamu zao zenye kuchukiza katika nyumba yenye inabeba jina langu, ili kuichafua.+ 31  Wamejenga mahali pa juu pa Tofeti, kwenye kuwa katika Bonde la Mwana wa Hinomu,*+ ili kuteketeza watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke katika moto,+ jambo lenye sikukuwa nimeamuru na halijaingia katika moyo wangu* hata kidogo.’+ 32  “‘Kwa hiyo angalia! siku zinakuja,’ ni vile Yehova anasema, ‘wakati halitaitwa tena Tofeti ao Bonde la Mwana wa Hinomu* lakini Bonde la Mauaji. Watazika katika Tofeti mupaka kusikuwe nafasi yenye kubakia.+ 33  Na maiti za watu hawa zitakuwa chakula cha ndege wa mbinguni na cha wanyama wa dunia, bila mutu wa kuwaogopesha.+ 34  Nitamaliza sauti ya kufurahi na sauti ya kushangilia, sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi,+ katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu, kwa maana inchi itafanywa kuwa mabomoko.’”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Haya ni,” ikizungumuzia majengo yote ya hekalu.
Ao “watoto wenye hawana baba.”
Ao “tangu milele mupaka milele.”
Ao “kuchoma zabihu ili zitoe moshi kwa ajili ya Baali.”
Tnn., “nilikuwa ninaamuka asubui sana na kusema.”
Jina la cheo la mungu mwanamuke mwenye aliabudiwa na Waisraeli waasi-imani; pengine ni mungu mwanamuke wa uzazi.
Ao “wanakasirisha; wanachokoza.”
Ao “shauri lao.”
Tnn., “kila siku nikiamuka asubui sana na kuwatuma.”
Tnn., “walifanya shingo yao kuwa ngumu.”
Tnn., “umeondolewa katika kinywa chao.”
Ao “zimetolewa kwa Mungu.”
Ao “wimbo wa maombolezo.”
Angalia Maana ya Maneno, “Gehena.”
Ao “halijaingia katika mawazo yangu.”
Angalia Maana ya Maneno, “Gehena.”