Yeremia 36:1-32
36 Sasa katika mwaka wa ine (4) wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, neno hili lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema:
2 “Kamata kitabu cha kukunjwa na uandike ndani yake maneno yote yenye nimekuambia juu ya Israeli na Yuda+ na mataifa yote,+ tangu siku ya kwanza yenye nilisema na wewe katika siku za Yosia mupaka leo.+
3 Pengine wakati wale wa nyumba ya Yuda watasikia juu ya musiba wote wenye ninakusudia kuleta juu yao, watageuka na kuacha njia zao zenye uovu, ili nisamehe kosa lao na zambi yao.”+
4 Kisha Yeremia akaita Baruku+ mwana wa Neria, na Yeremia akasema maneno yote yenye Yehova alikuwa amemuambia, na Baruku akayaandika katika kile kitabu cha kukunjwa.+
5 Kisha Yeremia akamuamuru Baruku: “Nimefungwa na siwezi kuingia katika nyumba ya Yehova.
6 Basi wewe ndiye unapaswa kuingia na kusoma kwa sauti kubwa maneno ya Yehova katika kitabu cha kukunjwa chenye uliandika wakati nilikuwa ninasema. Uyasome katika masikio ya watu kwenye nyumba ya Yehova katika siku ya kufunga; basi utayasomea watu wote wa Yuda wenye wanaingia kutoka katika miji yao.
7 Pengine ombi lao la kuomba rehema litamufikia Yehova, na watageuka, kila mumoja kutoka katika njia zake zenye uovu, kwa maana hasira na kasirani kali yenye Yehova ametangaza juu ya watu hawa ni kubwa.”
8 Basi Baruku mwana wa Neria akafanya mambo yote yenye Yeremia nabii alikuwa amemuamuru; akasoma kwa sauti kubwa katika kile kitabu cha kukunjwa maneno ya Yehova kwenye nyumba ya Yehova.+
9 Sasa katika mwaka wa tano (5) wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, katika mwezi wa kenda (9), watu wote katika Yerusalemu na watu wote wenye walikuja katika Yerusalemu kutoka katika miji ya Yuda wakatangaza kufunga mbele ya Yehova.+
10 Kisha Baruku akasoma kwa sauti kubwa katika kile kitabu cha kukunjwa maneno ya Yeremia kwenye nyumba ya Yehova, katika chumba* cha Gemaria+ mwana wa Shafani+ mwandikaji,* katika kiwanja cha juu, kwenye muingilio wa mulango mukubwa mupya wa nyumba ya Yehova,+ katika masikio ya watu wote.
11 Wakati Mikaya mwana wa Gemaria mwana wa Shafani alisikia maneno yote ya Yehova katika kile kitabu cha kukunjwa,
12 akashuka kuenda kwenye nyumba ya mufalme, kwenye chumba cha mwandishi. Wakubwa* wote walikuwa wamekaa pale: Elishama+ mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnatani+ mwana wa Akbori,+ Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na wakubwa wengine wote.
13 Mikaya akawaambia maneno yote yenye alikuwa amesikia wakati Baruku alisoma katika kile kitabu cha kukunjwa katika masikio ya watu.
14 Kisha wakubwa wote wakamutuma Yehudi mwana wa Netania mwana wa Shelemia mwana wa Kushi kwa Baruku, na kusema: “Kuja na ulete kitabu cha kukunjwa chenye ulisoma katika masikio ya watu.” Baruku mwana wa Neria akakamata kile kitabu cha kukunjwa katika mukono wake na akaingia kwao.
15 Wakamuambia: “Kaa, tafazali, na utusomee kwa sauti kubwa kitabu hicho cha kukunjwa.” Basi Baruku akawasomea kitabu hicho cha kukunjwa.
16 Sasa wakati tu walisikia maneno hayo yote, wakaangaliana kwa woga, na wakamuambia Baruku: “Hakika tunapaswa kumuambia mufalme maneno haya yote.”
17 Na wakamuuliza Baruku: “Tafazali, utuambie namna uliandika maneno haya yote. Je, yeye ndiye alikuwa anasema?”
18 Baruku akawajibu: “Aliniambia maneno haya yote, na nikayaandika kwa wino katika kitabu hiki cha kukunjwa.”
19 Wakubwa wakamuambia Baruku: “Uende na mujifiche, wewe pamoja na Yeremia, na musiache mutu yeyote ajue kwenye muko.”+
20 Kisha wakaingia kwa mufalme, kwenye kiwanja, na wakaweka kile kitabu katika chumba cha Elishama mwandishi, na wakamuambia mufalme kila kitu chenye walikuwa wamesikia.
21 Basi mufalme akamutuma Yehudi+ akamate kile kitabu cha kukunjwa, na akakileta kutoka katika chumba cha Elishama mwandishi. Yehudi akaanza kukisoma katika masikio ya mufalme na ya wakubwa wote wenye walikuwa wamesimama pembeni ya mufalme.
22 Mufalme alikuwa amekaa katika nyumba ya kipindi cha baridi, katika mwezi wa kenda (9),* na kulikuwa moto wenye kuwaka katika jiko la makaa mbele yake.
23 Kisha Yehudi kusoma mafungu tatu (3) ao ine (4), mufalme alikuwa anakata sehemu hiyo kwa kisu cha mwandishi na kuitupa katika moto wenye ulikuwa unawaka katika jiko, mupaka kitabu chote cha kukunjwa kikaishia katika moto wenye ulikuwa katika jiko.
24 Na hawakusikia woga wowote; mufalme wala watumishi wake wote wenye walisikia maneno hayo yote hawakupasua nguo zao.
25 Hata kama Elnatani,+ Delaya,+ na Gemaria+ walimuomba mufalme asiteketeze kwa moto kile kitabu cha kukunjwa, hakuwasikiliza.
26 Zaidi ya hayo, mufalme akaamuru Yerahmeeli mwana wa mufalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli wakamate Baruku mwandishi na Yeremia nabii, lakini Yehova akaendelea kuwaficha.+
27 Na neno la Yehova likakuja tena kwa Yeremia kisha mufalme kuteketeza kile kitabu cha kukunjwa chenye kilikuwa na maneno yenye Baruku alikuwa ameandika wakati aliambiwa na Yeremia,+ na kusema:
28 “Kamata kitabu kingine cha kukunjwa na uandike juu yake maneno yote yaleyale yenye yalikuwa kwenye kile kitabu cha kukunjwa cha kwanza, chenye Mufalme Yehoyakimu wa Yuda aliteketeza kwa moto.+
29 Na unapaswa kusema hivi juu ya Mufalme Yehoyakimu wa Yuda, ‘Yehova anasema hivi: “Umeteketeza kwa moto kitabu hiki cha kukunjwa na kusema, ‘Sababu gani umeandika juu yake: “Mufalme wa Babiloni atakuja hakika na kuharibu inchi hii na kuondoa kabisa mwanadamu na munyama kutoka ndani yake”?’+
30 Kwa hiyo Yehova anasema hivi juu ya Mufalme Yehoyakimu wa Yuda: ‘Hatakuwa na mutu yeyote mwenye atakaa kwenye kiti cha ufalme cha Daudi,+ na maiti yake itaachwa inje kwenye joto wakati wa muchana na baridi kali wakati wa usiku.+
31 Nitamuomba yeye na wazao wake* na watumishi wake watoe hesabu kwa sababu ya kosa lao, na nitaleta juu yao na juu ya wakaaji wa Yerusalemu na juu ya watu wa Yuda musiba wote wenye nilisema juu yao,+ lakini hawakusikiliza.’”’”+
32 Kisha Yeremia akakamata kitabu kingine cha kukunjwa na kukipatia Baruku mwana wa Neria, mwandishi,+ na akiambiwa na Yeremia, akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu cha kukunjwa chenye Mufalme Yehoyakimu wa Yuda alikuwa ameteketeza katika moto.+ Na maneno mengine mengi kama hayo yakaongezwa.
Maelezo ya Chini
^ Ao “chumba cha kukulia chakula.”
^ Ao “mwandishi.”
^ Ao “maofisa wa makao ya mufalme.”
^ Nusu ya pili ya Mwezi wa 11 na nusu ya kwanza ya Mwezi wa 12 kulingana na kalendari yetu. Angalia Nyongeza B15.
^ Tnn., “mbegu yake.”