Yeremia 49:1-39
49 Kwa ajili ya Waamoni,+ Yehova anasema hivi:
“Je, Israeli hana wana:
Je, hana muriti?
Sababu gani Malkamu+ ameriti Gadi?+
Na sababu gani watu wake wanakaa katika miji ya Israeli?”
2 “‘Kwa hiyo muangalie! siku zinakuja,’ ni vile Yehova anasema,‘Wakati nitafanya mulio wa vita usikiwe* juu ya Raba+ ya Waamoni.+
Atakuwa kilima chenye kimeachwa ukiwa,Na miji yake ya pembeni-pembeni* itawashwa moto.’
‘Na Israeli atachukua wale wenye walimuchukua,’+ ni vile Yehova anasema.
3 ‘Omboleza, Ee Heshboni, kwa maana Ai ameharibiwa!
Mulie kwa sauti kubwa, Enyi miji ya pembeni-pembeni ya Raba.
Muvae nguo za magunia.
Muomboleze na muende huku na huku kati ya mazizi ya majiwe,*Kwa maana Malkamu ataenda katika uhamisho,Pamoja na makuhani wake na wakubwa wake.+
4 Sababu gani unajisifu juu ya mabonde,*Juu ya eneo lako tambarare lenye kutiririka, Ee binti mwenye kukosa uaminifu,Mwenye kutegemea hazina zake,Na mwenye kusema: “Ni nani atanishambulia?”’”
5 “‘Angalia, ninaleta jambo la kuogopesha juu yako,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi anasema,‘Kutoka kwa wale wote wenye kukuzunguka.
Utatawanywa kila upande,Na hakuna mwenye atakusanya wale wenye kukimbia.’”
6 “‘Lakini kisha nitakusanya watu wa Waamoni wenye walikamatwa mateka,’ ni vile Yehova anasema.”
7 Kwa ajili ya Edomu, Yehova wa majeshi anasema hivi:
“Je, hakuna tena hekima yoyote katika Temani?+
Je, shauri la muzuri limeangamia kutoka kwa wale wenye kuwa na uelewaji?
Je, hekima yao imeoza?
8 Mukimbie, mugeuke!
Muende mukae katika sehemu za chini kabisa, Enyi wakaaji wa Dedani!+
Kwa maana nitaleta musiba juu ya EsauWakati muda wangu wa kumukazia uangalifu utafika.
9 Kama wakusanya-zabibu wangeingia kwako,Je, hawangeacha zabibu fulani nyuma kwa ajili ya kukusanywa?
Kama wezi wangeingia usiku,Wangetokeza uharibifu kwa kiasi tu chenye wanataka.+
10 Lakini nitamuvua Esau akuwe uchi.
Nitafunua mahali pake pa kujificha,Ili asiweze kujificha.
Watoto wake na ndugu zake na majirani wake wataharibiwa,+Na hatakuwa tena.+
11 Acha watoto wako wenye hawana baba,Na nitawalinda wazima,Na wajane wako watanitegemea.”
12 Kwa maana Yehova anasema hivi: “Angalia! Kama wale wenye hawakuhukumiwa kunywa kikombe wanapaswa kukikunywa, je, wewe utaachwa bila kupewa azabu kabisa? Hautaachwa bila kupewa azabu, kwa maana unapaswa kukikunywa.”+
13 “Kwa maana nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe,” ni vile Yehova anasema, “kwamba Bosra itakuwa kitu cha kuogopesha,+ kitu cha haya, uharibifu, na laana; na miji yake yote itakuwa mabomoko ya kudumu.”+
14 Nimesikia habari kutoka kwa Yehova,Mujumbe ametumwa kati ya mataifa, akisema:
“Mujikusanye pamoja na mumushambulie;Mujitayarishe kwa ajili ya pigano.”+
15 “Kwa maana angalia! Nimekufanya kuwa mudogo sana kati ya mataifa,Mwenye kuzarauliwa kati ya wanadamu.+
16 Mutetemeko wenye ulitokeza umekudanganya,Kimbelembele cha moyo wako,Ee wewe mwenye kukaa katika makimbilio ya mwamba,Mwenye kukaa kwenye kilima kirefu zaidi.
Hata kama unajenga chicha yako* juu kama tai,Nitakushusha kutoka pale,” ni vile Yehova anasema.
17 “Na Edomu anapaswa kuwa kitu cha kuogopesha.+ Kila mutu mwenye kupita pembeni yake ataangalia kwa woga na kupiga muluzi kwa sababu ya mapigo yake yote.
18 Kama vile katika uharibifu wa Sodoma na Gomora na wa miji yake jirani,”+ Yehova anasema, “hakuna mutu mwenye ataishi pale, na hakuna mutu mwenye atakaa pale.+
19 “Angalia! Mutu fulani atapanda ili kushambulia malisho yenye kuwa salama kama simba+ kutoka kwenye miti mingi midogo-midogo* pembeni ya Yordani, lakini kwa wakati kidogo nitamufanya akimbie kutoka kwake. Na nitaweka juu yake ule mwenye kuchaguliwa. Kwa maana ni nani mwenye kuwa kama mimi, na ni nani mwenye atanipinga? Ni muchungaji gani mwenye anaweza kusimama mbele yangu?+
20 Kwa hiyo musikie, Enyi watu, uamuzi wenye* Yehova amefanya juu ya Edomu na mambo yenye amefikiria juu ya wakaaji wa Temani:+
Hakika wenye kuwa wadogo wa kundi watakokotwa.
Atafanya makao yao yakuwe ukiwa kwa sababu yao.+
21 Kwa sauti ya kuanguka kwao, dunia imetetemeka.
Kuko kilio!
Sauti imesikiwa mupaka kwenye Bahari Nyekundu.+
22 Angalia! Atapanda na kushuka kama vile tai,+Na atanyoosha mabawa yake juu ya Bosra.+
Katika siku hiyo moyo wa wapiganaji-vita wa EdomuUtakuwa kama moyo wa mwanamuke mwenye kuzaa.”
23 Kwa ajili ya Damasko:+
“Hamati+ na Arpadi wamepatishwa haya,Kwa maana wamesikia habari ya mubaya.
Wanayeyuka kwa woga.
Kuko musukosuko katika bahari wenye hauwezi kutulizwa.
24 Damasko amepoteza bidii.
Amegeuka ili kukimbia, lakini ameshikwa na woga.
Taabu na maumivu vimemushika,Kama mwanamuke mwenye kuzaa.
25 Namna gani muji wenye sifa haukuachwa,Muji wa furaha?
26 Kwa maana vijana wake wataanguka katika viwanja vyake vya watu wote,Na maaskari wote wataangamia katika siku hiyo,” ni vile Yehova wa majeshi anasema.
27 “Nitawasha moto ukuta wa Damasko,Na utateketeza minara yenye ngome ya Ben-hadadi.”+
28 Kwa ajili ya Kedari+ na falme za Hasori, zenye Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni alipiga, Yehova anasema hivi:
“Musimame, mupande kuenda Kedari,Na muharibu wana wa Mashariki.
29 Mahema yao na makundi yao yatachukuliwa,Vitambaa vyao vya mahema na mali zao zote.
Ngamia wao watachukuliwa,Na watawalalamikia, ‘Kuko woga pande zote!’”
30 “Mukimbie, muende mbali!
Muende na mukae katika sehemu za chini kabisa, Enyi wakaaji wa Hasori,” ni vile Yehova anasema.
“Kwa maana Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni ametunga mbinu juu yenu,Na amefanya mupango juu yenu.”
31 “Musimame, mupande ili kushambulia taifa lenye kuwa na amani,Lenye kukaa kwa usalama!” ni vile Yehova anasema.
“Halina milango wala mapingo; wanaishi peke yao.
32 Ngamia wao watanyanganywa,Na mifugo yao mingi itakuwa vitu vyenye vinachukuliwa katika vita.
Nitawatawanya kwenye kila upepo,*Wale wenye wanakata nywele zao kwenye vipaji vya nyuso,+Na nitaleta musiba wao kutoka kila upande,” ni vile Yehova anasema.
33 “Na Hasori atakuwa pango la mbweha,Mahali kwenye kumeachwa ukiwa sikuzote.
Hakuna mutu mwenye ataishi kule,Na hakuna mutu mwenye atakaa ndani yake.”
34 Hili ndilo neno la Yehova lenye lilikuja kwa Yeremia nabii kuhusu Elamu+ kwenye mwanzo wa utawala wa Mufalme Sedekia+ wa Yuda:
35 “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Angalia, ninavunja upinde wa Elamu,+ chanzo cha* nguvu zao.
36 Nitaleta juu ya Elamu zile pepo ine (4) kutoka kwenye miisho ine ya mbingu, na nitawatawanya kwenye pepo hizi zote. Hakutakuwa taifa kwenye watu wa Elamu wenye walitawanywa hawataenda.’”
37 “Nitavunja-vunja Waelamu mbele ya maadui wao na mbele ya wale wenye wanatafuta kuchukua uzima wao;* na nitaleta musiba juu yao, kasirani yangu yenye kuwaka,” ni vile Yehova anasema. “Na nitatuma upanga uwafuate mupaka wakati nitakuwa nimewaharibu.”
38 “Na nitaweka kiti changu cha ufalme katika Elamu,+ na nitaharibu kutoka pale mufalme na wakubwa,” ni vile Yehova anasema.
39 “Lakini katika kipindi cha mwisho cha zile siku, nitakusanya watu wa Elamu wenye walikamatwa mateka,” ni vile Yehova anasema.
Maelezo ya Chini
^ Ao pengine, “sauti ya kilio cha pigano isikiwe.”
^ Ao “miji yenye kumuzunguka.”
^ Ao “mazizi ya kondoo.” Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.
^ Ao “maeneo tambarare ya chini.”
^ Ao “nyumba yako; kiota chako.”
^ Ao “vichaka vikubwa.”
^ Ao “shauri lenye.”
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Ao “kila upande.”
^ Tnn., “mwanzo wa.”
^ Ao “wale wenye wanatafuta nafsi yao.”