Yeremia 43:1-13

  • Watu wanakataa kutii na wanaenda Misri (1-7)

  • Neno la Yehova kwa Yeremia katika Misri (8-13)

43  Wakati Yeremia alikuwa amemaliza kuambia watu wote maneno haya yote kutoka kwa Yehova Mungu wao, kila neno lenye Yehova Mungu wao alikuwa amemutuma awaambie, 2  Azaria mwana wa Hoshaya, Yohanani+ mwana wa Karea, na watu wote wenye kimbelembele wakamuambia Yeremia: “Mambo yenye unasema ni ya uongo! Yehova Mungu wetu hakukutuma useme, ‘Musiende Misri kukaa kule.’ 3  Lakini Baruku+ mwana wa Neria anakuchochea juu yetu ili kututia katika mukono wa Wakaldayo, ili kutuua ao kutupeleka katika uhamisho Babiloni.”+ 4  Basi Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi na watu wote hawakutii sauti ya Yehova kwamba wabakie katika inchi ya Yuda. 5  Tofauti na hilo, Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wakakamata pamoja nao mabaki wote wa Yuda wenye walikuwa wamerudia kukaa katika inchi ya Yuda kutoka katika mataifa yote kwenye walikuwa wametawanywa.+ 6  Wakakamata wanaume, wanamuke, watoto, mabinti wa mufalme, na kila mutu mwenye* Nebuzaradani+ mukubwa wa walinzi alikuwa ameacha pamoja na Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani,+ na pia Yeremia nabii na Baruku mwana wa Neria. 7  Na wakaingia katika inchi ya Misri, kwa maana hawakutii sauti ya Yehova, na wakaenda mupaka Tahpanhesi.+ 8  Kisha neno la Yehova likakuja kwa Yeremia katika Tahpanhesi, na kusema: 9  “Kamata katika mukono wako majiwe makubwa, na uyafiche katika saruji* kwenye ngazi ya matofali yenye kuwa kwenye muingilio wa nyumba ya Farao katika Tahpanhesi, na wanaume Wayahudi wakiangalia. 10  Kisha uwaambie, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Angalia, ninaita Nebukadneza* mufalme wa Babiloni, mutumishi wangu,+ na nitaweka kiti chake cha ufalme juu ya majiwe haya yenye nimeficha, na atanyoosha hema yake ya kifalme juu yake.+ 11  Na ataingia na kupiga inchi ya Misri.+ Mutu yeyote mwenye alikusudiwa pigo lenye kuua atapigwa kwa pigo lenye kuua, na mutu yeyote mwenye alikusudiwa kuenda katika utekwa ataenda katika utekwa, na mutu yeyote mwenye alikusudiwa upanga atapigwa kwa upanga.+ 12  Na nitawasha moto nyumba za* miungu ya Misri,+ na ataiteketeza na kuipeleka ikiwa imetekwa. Atajifunika inchi ya Misri kumuzunguka kama vile muchungaji anajifunika mwenyewe nguo yake, na ataondoka kule kwa amani.* 13  Na atavunja vipande-vipande nguzo za* Bet-shemeshi* katika inchi ya Misri, na atateketeza kwa moto nyumba za* miungu ya Misri.”’”

Maelezo ya Chini

Ao “kila nafsi yenye.”
Ao “mortier.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
Ao “mahekalu ya.”
Ao “bila kuumizwa.”
Ao “minara ya.”
Ao “Nyumba (Hekalu la) ya Jua,” ni kusema, Heliopolisi.
Ao “mahekalu ya.”