Yeremia 21:1-14
21 Yeremia alipokea neno kutoka kwa Yehova wakati Mufalme Sedekia+ alituma kwake Pashuri+ mwana wa Malkiya na Sefania+ mwana wa Maaseya, kuhani, ili kutoa ombi hili:
2 “Tafazali umuulize Yehova kwa ajili yetu, kwa sababu Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni anapigana vita na sisi.+ Pengine Yehova atatutendea moja ya matendo yake ya ajabu, na hivyo ataondoka kwetu.”+
3 Yeremia akawaambia: “Mumuambie Sedekia hivi:
4 ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Angalia, ninageuza juu yenu* silaha za vita zenye kuwa katika mikono yenu wenyewe, zenye munatumia ili kupigana na mufalme wa Babiloni+ na Wakaldayo wenye kuwa inje ya ukuta wenye wanawazunguka ninyi kwa ajili ya vita. Na nitawakusanya katikati ya muji huu.
5 Na mimi mwenyewe nitapigana na ninyi+ kwa mukono wenye kunyooshwa na kwa mukono wenye nguvu, kwa hasira na kasirani kali na ukali mukubwa.+
6 Nitapiga wakaaji wa muji huu, mwanadamu na munyama pia. Watakufa kwa ugonjwa mukubwa wa kuambukiza.”’+
7 “‘“Na kisha,” ni vile Yehova anasema, “Nitatia Mufalme Sedekia wa Yuda na watumishi wake na watu wa muji huu—wale wenye wataokoka ugonjwa wa kuambukiza, upanga, na njaa—nitawatia katika mukono wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni, katika mukono wa maadui wao, na katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wao.*+ Atawapiga na kuwaangusha kwa upanga. Hatawasikitikia, ao kuonyesha huruma ao kuwa na rehema yoyote.”’+
8 “Na utaambia watu hawa, ‘Yehova anasema hivi: “Angalia, ninaweka mbele yenu njia ya uzima na njia ya kifo.
9 Wale wenye watabakia katika muji huu watakufa kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza. Lakini mutu yeyote mwenye atatoka na kujitia katika mikono ya Wakaldayo wenye wanawazunguka ninyi kwa ajili ya vita ataendelea kuishi, na atapata uzima wake* kama kitu chenye kilichukuliwa katika vita.”’*+
10 “‘“Kwa maana nimekaza uso wangu juu ya muji huu kwa ajili ya musiba haiko kwa ajili ya mema,”+ ni vile Yehova anasema. “Utatiwa katika mukono wa mufalme wa Babiloni,+ na atauteketeza kwa moto.”+
11 “‘Kwa nyumba ya mufalme wa Yuda: Musikie neno la Yehova.
12 Enyi nyumba ya Daudi, Yehova anasema hivi:
“Mutende haki kila asubui,Na mumukomboe ule mwenye ananyanganywa kutoka katika mukono wa mupunjaji,+Ili kasirani yangu kali isiwake kama moto+Na kuteketeza bila mutu wa kuuzimishaKwa sababu ya matendo yenu maovu.”’+
13 ‘Angalia, nitapigana na wewe, Ee mukaaji wa bonde,*Ee mwamba wa inchi tambarare,’ ni vile Yehova anasema.
‘Na ninyi wenye kusema: “Ni nani atashuka kupigana na sisi?
Na ni nani mwenye atashambulia makao yetu?”
14 Nitawaomba ninyi mutoe hesabuKulingana na matendo yenu,’+ ni vile Yehova anasema.
‘Na nitawasha moto katika pori lake,Na utateketeza vitu vyote vyenye kumuzunguka.’”+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Ao “nitawageuzia.”
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Ao “wenye wanatafuta nafsi yao.”
^ Ao “nafsi yake.”
^ Ao “ataponyoka na uzima wake.”
^ Ao “eneo tambarare la chini.”