Yeremia 40:1-16
40 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova kisha Nebuzaradani+ mukubwa wa walinzi kumuachilia huru kutoka Rama.+ Alikuwa amemupeleka kule akiwa amefungwa pingu za mikono, na alikuwa kati ya wale wote wenye walihamishwa wa Yerusalemu na wa Yuda wenye walikuwa wanapelekwa Babiloni.
2 Kisha mukubwa wa walinzi akamukamata Yeremia na kumuambia: “Yehova Mungu wako alitabiri musiba huu juu ya mahali hapa,
3 na Yehova ametimiza hilo kama vile alisema, kwa sababu mulimutendea Yehova zambi na hamukutii sauti yake. Ndiyo sababu jambo hili limewapata ninyi.+
4 Sasa ninakuachilia huru leo kutoka kwa pingu za mikono zenye zilikuwa kwenye mikono yako. Kama inaonekana muzuri kwako kuja pamoja na mimi Babiloni, kuja, na nitakuhangaikia. Lakini kama hautaki kuja pamoja na mimi Babiloni, usikuje. Angalia, inchi yote iko mbele yako. Uende mahali popote kwenye unachagua.”+
5 Wakati Yeremia alikuwa bado hajageuka, Nebuzaradani akasema: “Rudia kwa Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani,+ mwenye mufalme wa Babiloni ameweka juu ya miji ya Yuda, na ukae pamoja naye kati ya watu; ao uende mahali popote kwenye unachagua.”
Kisha mukubwa wa walinzi akamupatia posho la chakula na zawadi na akamuacha aende.
6 Basi Yeremia akaenda kwa Gedalia mwana wa Ahikamu kule Mispa+ na akakaa pamoja naye kati ya watu wenye walibakia katika inchi.
7 Kisha wakati fulani wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa katika eneo la mashamba pamoja na watu wao wakasikia kwamba mufalme wa Babiloni alikuwa amemuweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu ya inchi na kwamba alikuwa amemuweka juu ya wanaume, wanamuke, na watoto kati ya watu maskini wa inchi wenye hawakukuwa wamepelekwa Babiloni.+
8 Basi wakaenda kwa Gedalia kule Mispa.+ Walikuwa Ishmaeli+ mwana wa Netania, Yohanani+ na Yonatani wana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumeti, wana wa Efai Munetofa, na Yezania+ mwana wa Mumaakati, pamoja na watu wao.
9 Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani akawaapia kiapo, wao pamoja na watu wao, na kusema: “Musiogope kutumikia Wakaldayo. Mukae katika inchi na mumutumikie mufalme wa Babiloni, na mambo yatakuwa muzuri kwenu.+
10 Lakini mimi, nitakaa katika Mispa ili niwawakilishe ninyi kwa* Wakaldayo wenye wanakuja kwetu. Lakini ninyi munapaswa kukusanya divai, matunda ya kipindi cha joto, na mafuta na kuviweka katika vyombo vyenu vya kuwekea na kukaa katika miji yenye ninyi mulichukua.”+
11 Na Wayahudi wote wenye walikuwa katika Moabu, Amoni, na Edomu, na pia wale wenye walikuwa katika inchi zingine zote, wakasikia pia kama mufalme wa Babiloni alikuwa ameacha mabaki katika Yuda na kama alikuwa ameweka juu yao Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani.
12 Basi Wayahudi wote wakaanza kurudia kutoka kila mahali kwenye walikuwa wametawanywa, na wakakuja katika inchi ya Yuda, kwa Gedalia kule Mispa. Na wakakusanya divai na matunda ya kipindi cha joto kwa wingi sana.
13 Yohanani mwana wa Karea na wakubwa wote wa jeshi wenye walikuwa katika eneo la mashamba wakakuja kwa Gedalia kule Mispa.
14 Wakamuambia: “Je, haujue kama Baalisi, mufalme wa Waamoni,+ amemutuma Ishmaeli mwana wa Netania ili akuue?”*+ Lakini Gedalia mwana wa Ahikamu hakuwaamini.
15 Kisha Yohanani mwana wa Karea akamuambia kwa uficho Gedalia katika Mispa: “Ninataka kuenda na kumupiga na kumuua Ishmaeli mwana wa Netania, na hakuna mutu mwenye atajua. Sababu gani akuue,* na sababu gani watu wote wa Yuda wenye walikusanyika kwako watawanyike na mabaki ya Yuda waangamie?”
16 Lakini Gedalia+ mwana wa Ahikamu akamuambia Yohanani mwana wa Karea: “Usifanye vile, kwa maana mambo yenye unasema juu ya Ishmaeli ni uongo.”