Yeremia 46:1-28
46 Hili ndilo neno la Yehova kwa Yeremia nabii kuhusu mataifa:+
2 Kwa ajili ya Misri,+ kuhusu jeshi la Farao Neko+ mufalme wa Misri, mwenye alikuwa pembeni ya Muto Efrati na mwenye alishindwa kule Karkemishi na Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni katika mwaka wa ine (4) wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda:
3 “Mutayarishe ngao zenu za kidogo* na ngao zenu za mukubwa,Na muende kwenye pigano.
4 Mufunge farasi lijamu* na mupande, ninyi wapanda-farasi.
Musimame na muvae kofia zenu za chuma.
Munoe mikuki na muvae makoti yenu ya chuma.
5 ‘Sababu gani ninawaona wakiwa na woga?
Wanarudia nyuma, wapiganaji-vita wao wamepondwa.
Wamekimbia kwa woga, wapiganaji-vita wao hawakugeuka.
Kuko woga kuzunguka pande zote,’ ni vile Yehova anasema.
6 ‘Wenye ni wepesi hawawezi kukimbia, na wapiganaji-vita hawawezi kuponyoka.
Kule kaskazini, kwenye sehemu ya pembeni ya Muto Efrati,Wamejikwaa na kuanguka.’+
7 Ni nani huyu mwenye anapanda kama Muto Nile,Kama mito yenye kujaa sana maji?
8 Misri inapanda kama vile Muto Nile,+Kama mito yenye kujaa sana maji,Na inasema, ‘Nitapanda na kufunika dunia.
Nitaharibu muji na wale wenye kukaa ndani.’
9 Mupande, ninyi farasi!
Muende kiwazimu, ninyi magari!
Wapiganaji-vita waende,Kushi na Putu, wenye wanatumia ngao,+Na Ludimu,+ wenye wanatumia na kupinda* upinde.+
10 “Siku hiyo ni ya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi, siku ya kisasi ili kulipiza kisasi juu ya maadui wake. Na upanga utameza na kushiba na kujijaza damu yao, kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi, iko* na zabihu* katika inchi ya kaskazini pembeni ya Muto Efrati.+
11 Panda mupaka Gileadi uchukue zeri,+Ee binti bikira wa Misri.
Umeongeza bure tu matunzo yako,Kwa maana hakuna matunzo kwa ajili yako.+
12 Mataifa yamesikia juu ya haya yako,+Na kilio chako kimejaza inchi.
Kwa maana mupiganaji-vita anajikwaa juu ya mupiganaji-vita,Na wote wawili wanaanguka pamoja.”
13 Hili ndilo neno lenye Yehova alimuambia Yeremia nabii juu ya kuja kwa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni ili kupiga inchi ya Misri:+
14 “Muliseme katika Misri, mulitangaze katika Migdoli.+
Mulitangaze katika Nofu* na katika Tahpanhesi.+
Museme, ‘Musimame na mujitayarishe,Kwa maana upanga utameza kukuzunguka pande zote.
15 Sababu gani watu wako wenye nguvu wamefagiliwa mbali?
Walishindwa kusimama,Kwa maana Yehova amewasukuma chini.
16 Wanajikwaa na kuanguka kwa wingi.
Wanaambiana:
“Musimame! Turudie kwa watu wetu na kwenye inchi yetuKwa sababu ya upanga wenye kuua sana.”’
17 Kule wametangaza,‘Farao mufalme wa Misri ni makelele yenye hayana maanaMwenye ameacha nafasi ipite.’*+
18 ‘Kama vile hakika ninaishi,’ ni vile Mufalme anasema, mwenye jina lake ni Yehova wa majeshi,‘Yeye* ataingia kama Tabori+ kati ya milimaNa kama Karmeli+ pembeni ya bahari.
19 Tayarisha muzigo wako kwa ajili ya uhamisho,Ee binti mwenye kukaa Misri.
Kwa maana Nofu* itakuwa kitu cha kuogopesha;Itawashwa moto* na kuachwa bila mukaaji.+
20 Misri ni kama kitoto-dike cha ngombe chenye kupendeza,Lakini mainzi wenye kuuma watakuja kumushambulia kutoka kaskazini.
21 Hata maaskari wake wenye walikodiwa wenye kuwa katikati yake ni kama vitoto-dume vya ngombe vyenye kunenepa,Lakini wao pia wamegeuka na kukimbia pamoja.
Walishindwa kusimama,+Kwa maana siku ya musiba wao imekuja juu yao,Wakati wao wa kuombwa hesabu.’
22 ‘Sauti yake ni kama ya nyoka mwenye kukimbia,Kwa maana wanamufuata kwa nguvu, wakiwa na mashoka,Kama watu wenye kukata miti.*
23 Watakata pori lake,’ ni vile Yehova anasema, ‘hata kama lilionekana haliwezi kuingiwa ndani.
Kwa maana ni wengi kuliko nzige, hawana hesabu.
24 Binti ya Misri atapatishwa haya.
Atatiwa katika mukono wa watu wa kaskazini.’+
25 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema: ‘Sasa ninakaza uangalifu wangu juu ya Amoni+ kutoka No,*+ juu ya Farao, juu ya Misri, juu ya miungu yake,+ na juu ya wafalme wake—ndiyo, juu ya Farao na wote wenye wanamutegemea.’+
26 “‘Na nitawatia katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wao,* katika mukono wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni+ na watumishi wake. Lakini kisha ataikaliwa kama zamani,’ ni vile Yehova anasema.+
27 ‘Na wewe, mutumishi wangu Yakobo, usiogope,Na usiogopeshwe, Ee Israeli.+
Kwa maana, nitakuokoa kutoka mbaliNa uzao wako* kutoka inchi yao ya utekwa.+
Yakobo atarudia na kuwa na utulivu bila usumbufu,Bila mutu wa kuwaogopesha.+
28 Basi wewe mutumishi wangu Yakobo, usiogope,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwa maana niko pamoja na wewe.
Nitafanya uharibifu mukubwa kati ya mataifa yote kwenye nilikutawanya,+Lakini wewe sitakuharibu kabisa.+
Nitakutia nizamu* kwa kiasi chenye kufaa,+Lakini sitakuacha hata kidogo bila kukupatia azabu.’”
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Mara nyingi zilibebwa na wapiga-mishale.
^ Lijamu ni kipande cha chuma chenye kinawekwa kwenye kinywa cha munyama ili kumuongoza na kumuzuia.
^ Tnn., “kukanyanga.”
^ Ao “mauaji.”
^ Ao “eko.”
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Ao “Memfisi.”
^ Ao “wakati wenye uliwekwa upite.”
^ Ni kusema, ule mwenye anashinda Misri.
^ Ao “Memfisi.”
^ Ao pengine, “itakuwa inchi yenye imeachwa.”
^ Ao “wenye kukusanya kuni.”
^ Ni kusema, Tebesi.
^ Ao “wenye wanatafuta nafsi yao.”
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Tnn., “mbegu yako.”
^ Ao “Nitakurekebisha.”