Yeremia 18:1-23
18 Hili ndilo neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova:
2 “Simama na ushuke mupaka kwenye nyumba ya mufinyanzi,*+ na pale nitakufanya usikie maneno yangu.”
3 Basi nikashuka mupaka kwenye nyumba ya mufinyanzi,* na alikuwa anafanya kazi kwenye magurudumu* ya mufinyanzi.
4 Lakini chombo chenye mufinyanzi* alikuwa anatengeneza kwa udongo kikaharibika katika mukono wake. Basi mufinyanzi akakitengeneza upya kuwa chombo kingine, kama vile aliona inafaa.*
5 Kisha neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema:
6 “‘Je, siwezi kuwatendea ninyi kama vile mufinyanzi* huyu alitenda, Ee nyumba ya Israeli?’ ni vile Yehova anasema. ‘Muangalie! Kama udongo katika mukono wa mufinyanzi, ni vile ninyi muko katika mukono wangu, Ee nyumba ya Israeli.+
7 Wakati wowote nikisema juu ya kungoa na kubomoa na kuharibu taifa ao ufalme,+
8 na taifa hilo liache uovu wake wenye nilisema juu yake, mimi pia nitabadilisha mawazo yangu* juu ya musiba wenye nilikusudia kuleta juu yake.+
9 Lakini wakati wowote nikisema juu ya kujenga na kupanda taifa ao ufalme,
10 na linafanya mambo ya mubaya mbele ya macho yangu na halitii sauti yangu, nitabadilisha mawazo yangu* juu ya mema yenye nilikusudia kulitendea.’
11 “Sasa, tafazali, ambia watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, ‘Yehova anasema hivi: “Angalia, ninatayarisha* musiba na kufanya mupango mubaya juu yenu. Mugeuke, tafazali, kutoka kwenye njia zenu za mubaya, na murekebishe njia zenu na mazoea yenu.”’”+
12 Lakini wakasema: “Hakuna tumaini!+ Kwa maana tutafuata mawazo yetu wenyewe, na kila mumoja wetu atatenda kulingana na ugumu wa moyo wake muovu.”+
13 Kwa hiyo Yehova anasema hivi:
“Muulize ninyi wenyewe, tafazali, kati ya mataifa.
Ni nani amesikia jambo kama hili?
Bikira wa Israeli amefanya jambo lenye kuchukiza sana.+
14 Je, teluji* ya Lebanoni inapotea kutoka kwenye miamba yenye kuwa kwenye miteremuko yake?
Ao, je, maji baridi yenye kutiririka kutoka mbali yatakauka?
15 Lakini watu wangu wamenisahau.+
Kwa maana wanatoa zabihu kwa* kitu chenye hakina mafaa yoyote,+Na wanafanya watu wajikwae katika njia zao, njia za zamani,+Ili wapite kwenye barabara za kidogo-kidogo zenye haziko laini na zenye hazinyooke,*
16 Ili kufanya inchi yao kuwa kitu cha kuogopesha+Na kitu cha kupigiwa muluzi milele.+
Kila mutu mwenye anapita pembeni yake ataangalia kwa mushangao na kutikisa kichwa chake.+
17 Kama upepo wa mashariki, nitawatawanya mbele ya adui.
Nitawaonyesha mugongo wangu, hapana uso wangu, katika siku ya musiba wao.”+
18 Na wakasema: “Mukuje, tufanye mupango mubaya juu ya Yeremia,+ kwa maana sheria haitaangamia* kutoka kwa makuhani wetu ao shauri kutoka kwa watu wenye hekima ao neno kutoka kwa manabii. Mukuje tuseme juu yake,* na tusisikilize mambo yenye anasema.”
19 Unitegee sikio, Ee Yehova,Na usikilize mambo yenye wapinzani wangu wanasema.
20 Je, wema unapaswa kulipwa kwa ubaya?
Kwa maana wamechimbia uzima wangu* shimo.+
Kumbuka namna nilisimama mbele yako ili kusema mambo ya muzuri juu yao,Ili kugeuza kasirani yako kali kutoka kwao.
21 Basi toa wana wao wapate njaa,Na uwatoe kwenye nguvu za upanga.+
Bibi zao wafiwe na watoto na kuwa wajane.+
Wanaume wao wauawe kwa pigo lenye kuua,Vijana wao wapigwe na kuuawa kwa upanga katika pigano.+
22 Kilio kisikike kutoka kwenye nyumba zaoWakati utaleta juu yao wanyanganyi kwa kushitukia.
Kwa maana wamechimba shimo ili kunikamataNa wameweka mitego kwa ajili ya miguu yangu.+
23 Lakini wewe, Ee Yehova,Unajua muzuri mipango yao yote juu yangu ili waniue.+
Usifunike kosa lao,Na usifute zambi yao kutoka mbele yako.
Uwaache wakwazike mbele yako+Wakati utakamata hatua juu yao katika kasirani yako.+
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “mipeto; pneus.”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Tnn., “kama vile ilikuwa sawa katika macho ya mufinyanzi kutengeneza.”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “nitasikitika.”
^ Ao “nitasikitika.”
^ Tnn., “ninafanya.”
^ Ao “neige.”
^ Ao “wanachoma zabihu ili zitoe moshi kwa ajili ya.”
^ Ao “zenye hazikutengenezwa.”
^ Ao “agizo halitaangamia.”
^ Tnn., “tumupige kwa ulimi.”
^ Ao “nafsi yangu.”