Yeremia 52:1-34

  • Sedekia anaasi Babiloni (1-3)

  • Nebukadneza anazunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita (4-11)

  • Kuharibiwa kwa muji na hekalu (12-23)

  • Watu wanapelekwa katika uhamisho Babiloni (24-30)

  • Yehoyakini anaachiliwa huru kutoka katika gereza (31-34)

52  Sedekia+ alikuwa na miaka makumi mbili na moja (21) wakati alikuwa mufalme, na alitawala kwa miaka kumi na moja (11) katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Hamutali+ binti ya Yeremia wa Libna. 2  Aliendelea kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova, kulingana na mambo yote yenye Yehoyakimu alikuwa amefanya.+ 3  Ni kwa sababu ya kasirani ya Yehova kwamba mambo hayo yalitokea katika Yerusalemu na katika Yuda, mupaka akawatupa kutoka mbele ya macho yake.+ Na Sedekia akamuasi mufalme wa Babiloni.+ 4  Katika mwaka wa kenda (9) wa utawala wa Mufalme Sedekia, katika mwezi wa kumi (10), katika siku ya kumi ya mwezi huo, Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni alikuja pamoja na jeshi lake lote ili kupigana na Yerusalemu. Wakapiga kambi juu yake na kujenga ukuta wa kuzunguka kwa ajili ya vita kuizunguka pande zote.+ 5  Na muji ukazungukwa kwa ajili ya vita mupaka mwaka wa kumi na moja (11) wa Mufalme Sedekia. 6  Katika mwezi wa ine (4), katika siku ya kenda (9) ya mwezi huo,+ njaa ikakuwa kali katika muji, na hapakukuwa chakula kwa ajili ya watu wa inchi.+ 7  Mwishowe ukuta wa muji ukatobolewa tundu kubwa, na maaskari wote wakakimbia kutoka katika muji usiku kupitia mulango mukubwa wenye kuwa kati ya zile kuta mbili karibu na bustani ya mufalme, wakati Wakaldayo walikuwa wanazunguka muji; na wakaendelea kupitia njia ya Araba.+ 8  Lakini jeshi la Wakaldayo likamufuatilia mufalme, na wakamufikia Sedekia+ katika maeneo tambarare ya jangwa la Yeriko, na maaskari wake wote wakatawanyika kutoka pembeni yake. 9  Kisha wakamukamata mufalme na kumuleta mupaka kwa mufalme wa Babiloni kule Ribla katika inchi ya Hamati, na akamuhukumu. 10  Na mufalme wa Babiloni akaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake, na pia akaua wakubwa wote wa Yuda kule Ribla. 11  Kisha mufalme wa Babiloni akapofusha macho ya Sedekia,+ akamufunga kwa pingu za shaba, akamupeleka Babiloni, na kumufunga katika gereza mupaka siku ya kifo chake. 12  Katika mwezi wa tano (5), katika siku ya kumi (10) ya mwezi huo, ni kusema, katika mwaka wa kumi na kenda (19) wa Mufalme Nebukadneza* mufalme wa Babiloni, Nebuzaradani mukubwa wa walinzi, mwenye alikuwa mutumishi wa mufalme wa Babiloni, akaingia ndani ya Yerusalemu.+ 13  Akateketeza kwa moto nyumba ya Yehova,+ nyumba ya mufalme, na nyumba zote za Yerusalemu; akateketeza pia kwa moto kila nyumba kubwa. 14  Na kuta zenye kuzunguka Yerusalemu zilibomolewa na jeshi lote la Wakaldayo lenye lilikuwa pamoja na mukubwa wa walinzi.+ 15  Nebuzaradani mukubwa wa walinzi akapeleka katika uhamisho wamoja kati ya watu wa hali ya chini na wale watu wengine wenye walibakia wenye waliachwa katika muji. Akakamata pia wale wenye walikimbia wenye walikuwa wamekimbia na kujiunga na mufalme wa Babiloni na pia wenye walibakia kati ya wafanyakazi wenye ufundi.+ 16  Lakini Nebuzaradani mukubwa wa walinzi akaacha wamoja kati ya watu maskini zaidi wa inchi watumike wakiwa watunza-mizabibu na wafanyakazi wa kulazimishwa.+ 17  Na Wakaldayo wakavunja vipande-vipande zile nguzo za shaba+ za nyumba ya Yehova na yale magari+ na ile Bahari ya shaba+ vyenye vilikuwa katika nyumba ya Yehova, na wakapeleka shaba yote kule Babiloni.+ 18  Walikamata pia makopo, vipao,* vizimisha-moto, mabakuli,+ vikombe,+ na vyombo vyote vya shaba vyenye vilitumiwa katika utumishi wa hekalu. 19  Mukubwa wa walinzi alikamata beseni,+ vyetezo, mabakuli, makopo, vinara vya taa,+ vikombe, na mabakuli yenye yalikuwa ya zahabu na feza ya kweli.+ 20  Na zile nguzo mbili, ile Bahari, wale ngombe-dume kumi na mbili (12) wa shaba+ wenye walikuwa chini ya ile Bahari, na yale magari yenye Mufalme Sulemani alikuwa ametengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yehova, shaba ya vyombo hivyo vyote haingeweza kupimwa. 21  Kuhusu zile nguzo, kila nguzo ilikuwa na urefu kuenda juu wa mikono* kumi na munane (18), na kamba ya kupimia yenye urefu wa mikono kumi na mbili (12) ingeweza kuizunguka;+ unene wake ulikuwa na upana wa vidole* ine (4), na ilikuwa na tundu. 22  Na kifuniko cha nguzo chenye kilikuwa juu yake kilikuwa cha shaba; na urefu wa kifuniko kimoja ulikuwa wa mikono tano (5);+ na wavu* na makomamanga vyenye kuzunguka kifuniko pande zote, vyote vilitengenezwa kwa shaba. Nguzo ya pili ilikuwa vilevile, pia yale makomamanga. 23  Kulikuwa makomamanga makumi kenda na sita (96) pembeni-pembeni; kwa ujumla, kulikuwa makomamanga mia moja (100) kuzunguka wavu huo.*+ 24  Mukubwa wa walinzi alimukamata pia Seraya+ mukubwa wa makuhani, Sefania+ kuhani wa pili, na wale walinzi watatu (3) wa milango.+ 25  Na alikamata kutoka katika muji ofisa mumoja wa makao ya mufalme mwenye alikuwa musimamizi wa maaskari, watu saba (7) wenye walishirikiana kwa ukaribu na mufalme wenye walipatikana katika muji, na pia mwandishi wa mukubwa wa jeshi, mwenye kukusanya watu wa inchi, na watu makumi sita (60) kutoka kati ya watu wa kawaida wa inchi wenye walikuwa wangali katika muji. 26  Nebuzaradani mukubwa wa walinzi akawakamata na kuwapeleka kwa mufalme wa Babiloni kule Ribla. 27  Mufalme wa Babiloni akawapiga na kuwaua kule Ribla+ katika inchi ya Hamati. Basi Yuda wakaenda katika uhamisho kutoka katika inchi yao.+ 28  Hawa ndio watu wenye Nebukadneza* alipeleka katika uhamisho: katika mwaka wa saba (7), Wayahudi elfu tatu makumi mbili na tatu (3 023).+ 29  Katika mwaka wa kumi na munane (18) wa Nebukadneza,*+ watu* mia munane makumi tatu na mbili (832) walichukuliwa kutoka Yerusalemu. 30  Katika mwaka wa makumi mbili na tatu (23) wa Nebukadneza,* Nebuzaradani mukubwa wa walinzi alipeleka Wayahudi katika uhamisho, watu* mia saba makumi ine na tano (745).+ Kwa ujumla, watu* elfu ine mia sita (4 600) walipelekwa katika uhamisho. 31  Kisha katika mwaka wa makumi tatu na saba (37) wa uhamisho wa Mufalme Yehoyakini+ wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili (12), katika siku ya makumi mbili na tano (25) ya mwezi huo, Mufalme Evil-merodaki wa Babiloni, katika mwaka wenye alikuwa mufalme, akamuachilia huru* Mufalme Yehoyakini wa Yuda na kumutosha katika gereza.+ 32  Alisema naye kwa fazili na akaweka kiti chake cha ufalme juu kuliko viti vya wafalme wengine wenye walikuwa pamoja naye katika Babiloni. 33  Basi Yehoyakini akavua nguo zake za gereza, na alikuwa anakula kwa ukawaida mbele yake siku zote za maisha yake. 34  Alipewa kwa ukawaida posho ya chakula kutoka kwa mufalme wa Babiloni, siku kwa siku, mupaka siku ya kifo chake, siku zote za maisha yake.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
Ao “sepetu; bêches.”
Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Upana wa kidole ulikuwa sawa na santimetre 1.85 (inchi 0.73). Angalia Nyongeza B14.
Ao “makila.”
Ao “makila hiyo.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
Ao “nafsi.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
Ao “nafsi.”
Ao “nafsi.”
Tnn., “akainua kichwa cha.”