Yeremia 34:1-22
34 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, wakati Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni na jeshi lake lote na falme zote za dunia zenye kuwa chini ya mamlaka yake na watu wote walikuwa wanapigana vita juu ya Yerusalemu na miji yake yote:+
2 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Uende na useme na Mufalme Sedekia+ wa Yuda na umuambie: “Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninatia muji huu katika mukono wa mufalme wa Babiloni, na atauteketeza kwa moto.+
3 Na hautaponyoka kutoka katika mukono wake, kwa maana hakika utakamatwa na kutiwa katika mukono wake.+ Na utamuona Mufalme wa Babiloni macho kwa macho, na atasema na wewe uso kwa uso, na utaenda Babiloni.’+
4 Hata hivyo, sikia neno la Yehova, Ee Mufalme Sedekia wa Yuda, ‘Yehova anasema hivi juu yako wewe: “Hautakufa kwa upanga.
5 Utakufa kwa amani,+ na watakufanyia sikukuu ya kuchoma manukato kama vile walifanyia baba zako, wafalme wa zamani wenye walikutangulia, na watakuombolezea, ‘Aa, Ee bwana!’ kwa maana ‘nimesema neno hilo,’ ni vile Yehova anasema.”’”’”
6 Kisha Yeremia nabii akamuambia maneno haya yote Mufalme Sedekia wa Yuda katika Yerusalemu,
7 wakati majeshi ya mufalme wa Babiloni yalikuwa yanapiga vita juu ya Yerusalemu na juu ya miji yote ya Yuda yenye ilibakia,+ juu ya Lakishi+ na juu ya Azeka;+ kwa maana hiyo ndiyo tu ilikuwa miji yenye ngome yenye ilibakia kati ya miji ya Yuda.
8 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova kisha Mufalme Sedekia kufanya agano pamoja na watu wote wenye walikuwa katika Yerusalemu ili kuwatangazia uhuru,+
9 kwamba kila mutu aachilie huru watumwa wake Waebrania, wanaume na wanamuke, ili mutu yeyote asiendelee kumufanya Muyahudi mwenzake kuwa mutumwa wake.
10 Basi wakubwa wote na watu wote wakatii. Walikuwa wameingia katika agano kwamba kila mutu aachilie huru watumwa wake wanaume na wanamuke na asiendelee tena kuwafanya kuwa watumwa. Wakatii na wakawaacha waende.
11 Hata hivyo, kisha wakati fulani walirudisha watumwa wao wanaume na wanamuke wenye walikuwa wameachilia huru, na wakawalazimisha kurudia katika utumwa.
12 Basi neno la Yehova likakuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema:
13 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Nilifanya agano pamoja na mababu zenu+ katika siku yenye niliwatosha katika inchi ya Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa,+ nikisema:
14 “Kwenye mwisho wa miaka saba (7), kila mumoja wenu anapaswa kumuachilia huru ndugu yake Mwebrania mwenye aliuzishwa kwako na amekutumikia miaka sita (6); unapaswa kumuachilia huru.”+ Lakini mababu zenu hawakunisikiliza wala kunitegea masikio yao.
15 Na hivi karibuni* ninyi wenyewe muligeuka na kufanya mambo yenye kuwa sawa mbele ya macho yangu kwa kutangazia wenzenu uhuru, na mukafanya agano mbele yangu katika nyumba yenye kubeba jina langu.
16 Lakini kisha, muligeuka na kuchafua jina langu+ kwa kurudisha watumwa wenu wanaume na wanamuke wenye mulikuwa mumeachilia huru kama vile walitaka,* na mukawalazimisha kurudia katika utumwa.’
17 “Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Hamukunitii katika kutangaza uhuru, kila mutu kwa ndugu yake na kwa mwenzake.+ Basi sasa nitawatangazia ninyi uhuru,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwa upanga, ugonjwa wa kuambukiza, na njaa,+ na nitawafanya ninyi kuwa kitu cha kuogopesha kwa falme zote za dunia.+
18 Na ni hivi itafanyika kwa watu wenye walivunja agano langu kwa kukosa kutenda maneno ya agano lenye walifanya mbele yangu wakati walikata kitoto-dume cha ngombe vipande mbili na kupita katikati ya vile vipande,+
19 ni kusema, wakubwa wa Yuda, wakubwa wa Yerusalemu, maofisa wa makao ya mufalme, makuhani, na watu wote wa inchi wenye walipita katikati ya vile vipande vya kitoto-dume cha ngombe:
20 Nitawatia katika mukono wa maadui wao na katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wao,* na maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa mbinguni na cha wanyama wa dunia.+
21 Na nitatia Mufalme Sedekia wa Yuda na wakubwa wake katika mukono wa maadui wao na katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wao* na katika mukono wa majeshi ya mufalme wa Babiloni,+ yenye yanaondoka kuwaacha ninyi.’+
22 “‘Angalia, nitatoa agizo,’ ni vile Yehova anasema, ‘na nitawarudisha katika muji huu, na wataupiga vita na kuukamata na kuuteketeza kwa moto;+ na nitafanya miji ya Yuda kuwa eneo lenye limeachwa, bila mukaaji.’”+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Tnn., “leo.”
^ Ao “kama vile nafsi yao ilitaka.”
^ Ao “wenye wanatafuta nafsi zao.”
^ Ao “wenye wanatafuta nafsi zao.”