Yeremia 37:1-21

  • Wakaldayo wataondoka kwa wakati kidogo tu (1-10)

  • Yeremia anafungwa katika gereza (11-16)

  • Sedekia anakutana na Yeremia (17-21)

    • Yeremia anapewa mukate (21)

37  Na Mufalme Sedekia+ mwana wa Yosia akaanza kutawala pa nafasi ya Konia*+ mwana wa Yehoyakimu, kwa maana Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni alimufanya kuwa mufalme katika inchi ya Yuda.+ 2  Lakini yeye na watumishi wake na watu wa inchi hawakusikiliza maneno ya Yehova yenye yalisemwa kupitia Yeremia nabii. 3  Na Mufalme Sedekia akatuma Yehukali+ mwana wa Shelemia na Sefania+ mwana wa Maaseya kuhani kwa Yeremia nabii, na kusema: “Tafazali sali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wetu.” 4  Yeremia alikuwa anatembea huku na huku kwa uhuru kati ya watu, kwa maana walikuwa hawajamutia katika gereza.+ 5  Sasa jeshi la Farao lilikuwa limeondoka Misri,+ na Wakaldayo wenye walikuwa wanazunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita wakasikia habari juu yao. Basi wakaondoka mbele ya Yerusalemu.+ 6  Kisha neno la Yehova likakuja kwa Yeremia nabii, na kusema: 7  “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Mumuambie hivi mufalme wa Yuda, mwenye aliwatuma ninyi kwangu ili kuniuliza: “Angalia! Jeshi la Farao lenye linakuja kuwasaidia ninyi litarudia katika inchi yake, Misri.+ 8  Na Wakaldayo watarudia tena na kupiga vita juu ya muji huu na kuukamata na kuuteketeza kwa moto.”+ 9  Yehova anasema hivi: “Musijidanganye* kwa kusema, ‘Hakika Wakaldayo wataenda kutoka kwetu,’ kwa sababu hawataenda. 10  Hata kama mungepiga na kuua jeshi lote la Wakaldayo wenye wanapigana na ninyi kisha kubakie tu watu wao wenye waliumizwa, bado wangesimama kutoka kwenye mahema yao na kuteketeza muji huu kwa moto.”’”+ 11  Wakati jeshi la Wakaldayo lilikuwa limeondoka mbele ya Yerusalemu kwa sababu ya jeshi la Farao,+ 12  Yeremia akaondoka Yerusalemu na kuenda kwenye inchi ya Benyamini+ ili apokee fungu lake kule kati ya watu wake. 13  Lakini wakati alifika kwenye Mulango Mukubwa wa Benyamini, ofisa mwenye alikuwa juu ya walinzi, mwenye jina lake lilikuwa Iriya mwana wa Shelemia mwana wa Hanania, akamukamata Yeremia nabii na kusema: “Unakimbia kuenda kwa Wakaldayo!” 14  Lakini Yeremia akasema: “Haiko kweli! Mimi sikimbie kuenda kwa Wakaldayo.” Lakini hakumusikiliza. Basi Iriya akamukamata Yeremia na kumuingiza kwa wakubwa. 15  Wakubwa wakamukasirikia Yeremia,+ na wakamupiga na kumufunga*+ katika nyumba ya Yehonatani mwandishi, yenye ilikuwa imefanywa kuwa gereza. 16  Yeremia alitiwa katika gereza la chini ya udongo,* katika vyumba vyenye ngome, na akakaa kule siku nyingi. 17  Kisha Mufalme Sedekia akatuma aletwe, na mufalme akamuuliza maulizo kwa siri katika nyumba yake.*+ Akauliza, “Je, kuko neno lolote kutoka kwa Yehova?” Yeremia akasema, “Liko!” na akaendelea, “Utatiwa katika mukono wa mufalme wa Babiloni!”+ 18  Pia Yeremia akamuambia Mufalme Sedekia: “Namna gani nimekutendea zambi wewe na watumishi wako na watu hawa, na hivyo mumenitia katika gereza? 19  Wako wapi, sasa, manabii wenu wenye waliwatolea ninyi unabii, ‘Mufalme wa Babiloni hatakuja juu yenu ninyi na juu ya inchi hii’?+ 20  Sasa sikiliza, tafazali, Ee bwana wangu mufalme. Tafazali, kubali ombi langu la kuomba rehema. Usinirudishe katika nyumba ya Yehonatani+ mwandishi, ili nisikufie kule.”+ 21  Basi Mufalme Sedekia akaamuru kwamba Yeremia awekwe katika kifungo katika Kiwanja cha Walinzi,+ na alipewa mukate wa muviringo kila siku kutoka kwenye barabara ya watengenezaji wa mikate+ mupaka wakati mikate yote iliisha katika muji.+ Na Yeremia akaendelea kukaa katika Kiwanja cha Walinzi.

Maelezo ya Chini

Anaitwa pia Yehoyakini na Yekonia.
Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
Ao “Musidanganye nafsi zenu.”
Tnn., “wakamutia katika nyumba ya pingu.”
Tnn., “nyumba ya tangi la maji.”
Ao “nyumba yake ya kifalme.”