Yeremia 32:1-44
32 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova katika mwaka wa kumi (10) wa Mufalme Sedekia wa Yuda, ni kusema, mwaka wa kumi na munane (18) wa Nebukadneza.*+
2 Wakati huo majeshi ya mufalme wa Babiloni yalikuwa yanazunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita, na Yeremia nabii alikuwa amefungwa katika Kiwanja cha Walinzi+ katika nyumba ya mufalme wa Yuda.
3 Kwa maana Mufalme Sedekia wa Yuda alikuwa amemufunga,+ akisema, “Sababu gani unatoa unabii kama huu? Unasema, ‘Yehova anasema hivi: “Nitatia muji huu katika mukono wa mufalme wa Babiloni, na ataukamata,+
4 na Mufalme Sedekia wa Yuda hataponyoka kutoka kwa Wakaldayo, kwa maana hakika atatiwa katika mukono wa mufalme wa Babiloni, na atasema naye uso kwa uso na kumuona macho kwa macho.”+
5 ‘Atamupeleka Sedekia Babiloni, na atabakia kule mupaka wakati nitamukazia uangalifu,’ ni vile Yehova anasema. ‘Hata kama munaendelea kupigana vita na Wakaldayo, hamutafanikiwa.’”+
6 Yeremia akasema: “Neno la Yehova limekuja kwangu, na kusema,
7 ‘Angalia, Hanameli mwana wa Shalumu ndugu ya baba yako atakuja kwako na kusema: “Ujinunulie shamba langu lenye kuwa katika Anatoti,+ kwa sababu uko na haki ya kwanza ya kulikomboa.”’”+
8 Hanameli mwana wa ndugu ya baba yangu akakuja kwangu, kama vile Yehova alikuwa amesema, katika Kiwanja cha Walinzi, na akaniambia: “Tafazali nunua shamba langu lenye kuwa kule Anatoti, katika inchi ya Benyamini, kwa maana uko na haki ya kuliriti na kulikomboa. Ujinunulie shamba hilo.” Halafu nikajua kwamba jambo hilo lilikuwa kupitia neno la Yehova.
9 Basi nikanunua shamba lenye lilikuwa Anatoti kutoka kwa Hanameli mwana wa ndugu ya baba yangu. Nikamupimia feza,+ shekeli* saba (7) na vipande kumi (10) vya feza.
10 Kisha nikaandika kwenye karatasi ya mapatano,+ nikaitia muhuri, nikaita mashahidi,+ na nikapima feza katika mizani.*
11 Nikakamata ile karatasi ya mapatano ya kununua, yenye ilitiwa muhuri kulingana na amri na masharti ya kisheria, na pia karatasi ya mapatano yenye iliachwa bila kutiwa muhuri,
12 na nikapana karatasi ya mapatano ya kununua kwa Baruku+ mwana wa Neria+ mwana wa Mahseya mbele ya Hanameli mwana wa ndugu ya baba yangu, wale mashahidi wenye waliandika katika karatasi ya mapatano ya kununua, na Wayahudi wote wenye walikuwa wamekaa katika Kiwanja cha Walinzi.+
13 Sasa nikamuamuru Baruku mbele yao, kwa kusema:
14 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kamata karatasi hizi za mapatano, karatasi hii ya mapatano ya kununua, yenye ilitiwa muhuri na ile karatasi ingine ya mapatano yenye iliachwa bila kutiwa muhuri, na uzitie katika chombo cha udongo, ili zichungwe kwa wakati murefu.’
15 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Nyumba na mashamba na mashamba ya mizabibu vitanunuliwa tena katika inchi hii.’”+
16 Halafu nikasali kwa Yehova kisha kumupatia Baruku mwana wa Neria ile karatasi ya mapatano ya kununua, kwa kusema:
17 “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova! Angalia! Uliumba mbingu na dunia kwa nguvu zako kubwa+ na kwa mukono wako wenye kunyooshwa. Hakuna jambo lenye kuwa la ajabu sana kwako,
18 wewe Mwenye kuonyesha upendo mushikamanifu kwa maelfu, lakini mwenye kulipa kosa la baba kwa* wana wao kisha wao,+ Mungu wa kweli, mwenye kuwa mukubwa na Mwenye nguvu, wewe mwenye jina lako ni Yehova wa majeshi.
19 Wewe ni mukubwa katika shauri* na mwenye nguvu katika matendo,+ wewe mwenye macho yako yanachunguza njia zote za wanadamu,+ ili kumupatia kila mutu kulingana na njia zake na kulingana na mambo yenye anafanya.+
20 Umefanya katika inchi ya Misri alama na miujiza yenye inajulikana mupaka leo, na hivyo umejifanyia jina katika Israeli na kati ya wanadamu,+ kama leo hii.
21 Na ukatosha watu wako Israeli katika inchi ya Misri, kwa alama, kwa miujiza, kwa mukono wenye nguvu, kwa mukono wenye kunyooshwa, na kwa matendo yenye kuogopesha.+
22 “Kisha wakati fulani ukawapatia inchi hii yenye uliapa kwamba utapatia mababu zao,+ inchi yenye kutiririka maziwa na asali.+
23 Na wakaingia na kuiriti, lakini hawakutii sauti yako ao kutembea katika sheria yako. Hawakufanya jambo lolote lenye uliwaamuru wafanye, na hivyo ukafanya musiba huu wote uwaangukie.+
24 Angalia! Watu wamekuja na maboma ya kuzunguka ili kukamata muji,+ na kwa sababu ya upanga,+ njaa, na ugonjwa wa kuambukiza,+ hakika muji utaanguka katika mikono ya Wakaldayo wenye wanaupiga vita; mambo yenye ulisema yametimia yote, kama vile unaona sasa.
25 Lakini umeniambia, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, ‘Ujinunulie shamba kwa feza na uite mashahidi,’ hata kama hakika muji utatiwa katika mukono wa Wakaldayo.”
26 Halafu neno la Yehova likakuja kwa Yeremia, na kusema:
27 “Mimi huyu, Yehova, Mungu wa wanadamu wote.* Je, kuko jambo lolote lenye ni la ajabu sana kwangu?
28 Basi Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninatia muji huu katika mukono wa Wakaldayo na katika mukono wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni, na ataukamata.+
29 Na Wakaldayo wenye wanapigana vita na muji huu wataingia na kuchoma muji huu kwa moto na kuuteketeza+ pamoja na nyumba zenye juu ya sehemu zake za juu watu walitoa zabihu kwa Baali na kutolea miungu mingine matoleo ya kinywaji ili kunikasirisha.’+
30 “‘Kwa maana watu wa Israeli na wa Yuda wamefanya mambo ya mubaya tu mbele ya macho yangu, tangu ujana wao na kuendelea;+ watu wa Israeli wanaendelea kunikasirisha kwa kazi ya mikono yao,’ ni vile Yehova anasema.
31 ‘Kwa maana muji huu, tangu siku waliujenga mupaka leo, umekuwa kwangu tu kitu cha kuchochea hasira na kasirani kali,+ na hivyo lazima uondolewe mbele ya uso wangu,+
32 kwa sababu ya uovu wote wenye watu wa Israeli na wa Yuda wamefanya ili kunikasirisha—wao, wafalme wao,+ wakubwa wao,+ makuhani wao, manabii wao,+ na watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu.
33 Waliendelea kunigeuzia migongo yao, hapana nyuso zao;+ hata kama nilijaribu kuwafundisha tena na tena,* hakuna hata mumoja wao mwenye alisikiliza ili kupokea nizamu.+
34 Na waliweka sanamu zao zenye kuchukiza katika nyumba yenye kubeba jina langu, ili kuichafua.+
35 Zaidi ya hayo, walijenga mahali pa juu pa Baali katika Bonde la Mwana wa Hinomu,*+ ili kupitisha watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke katika moto kwa ajili ya Moleki,+ jambo lenye sikukuwa nimewaamuru+ na lenye halijaingia katika moyo wangu* hata kidogo ili kufanya jambo kama hilo lenye kuchukiza, na kufanya Yuda watende zambi.’
36 “Kwa hiyo Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi juu ya muji huu wenye munasema utatiwa katika mukono wa mufalme wa Babiloni kwa upanga, njaa, na ugonjwa wa kuambukiza,
37 ‘Angalia, nitawakusanya pamoja kutoka katika inchi zote kwenye niliwatawanya katika hasira yangu na katika kasirani yangu kali na katika kasirani kubwa,+ na nitawarudisha mahali hapa na kufanya wakae katika usalama.+
38 Na watakuwa watu wangu, na mimi nitakuwa Mungu wao.+
39 Na nitawapatia moyo mumoja+ na njia moja ili waniogope sikuzote, kwa faida yao wenyewe na kwa faida ya watoto wao kisha wao.+
40 Na nitafanya agano la milele pamoja nao,+ kwamba sitageuka na kuacha kuwatendea mema;+ na nitatia woga wangu katika mioyo yao, na hivyo hawatageuka na kuniacha.+
41 Nitafurahi juu yao ili kuwatendea mema,+ na nitawapanda imara katika inchi hii,+ kwa moyo wangu wote na kwa nafsi* yangu yote.’”
42 “Kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Kama vile nimeletea watu hawa musiba huu wote mukubwa, ni vile nitawaletea mema yote* yenye ninawaahidi.+
43 Na mashamba yatanunuliwa tena katika inchi hii,+ hata kama munasema: “Ni inchi yenye imeachwa yenye haina mwanadamu na munyama, na imetiwa katika mukono wa Wakaldayo.”’
44 “‘Mashamba yatanunuliwa kwa feza, karatasi za mapatano ya kununua zitaandikwa na kutiwa muhuri, na mashahidi wataitwa katika inchi ya Benyamini,+ katika maeneo yenye kuzunguka Yerusalemu, katika miji ya Yuda,+ katika miji ya eneo lenye milima, na katika miji ya inchi tambarare ya chini,+ na katika miji ya kusini, kwa sababu nitarudisha watu wao wenye walikamatwa mateka,’+ ni vile Yehova anasema.”
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.
^ Ao “kilo.”
^ Tnn., “katika kifua cha.”
^ Ao “mukubwa kuhusiana na makusudi yako.”
^ Tnn., “kila mwili.”
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Tnn., “nikiamuka asubui sana na kufundisha.”
^ Angalia Maana ya Maneno, “Gehena.”
^ Ao “halijaingia katika mawazo yangu.”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “vitu vyote vya muzuri vyenye.”