Yeremia 51:1-64
51 Yehova anasema hivi:
“Angalia, ninaamusha upepo wenye kuharibuJuu ya Babiloni+ na juu ya wakaaji wa Leb-kamai.*
2 Nitatuma wenye kupepua Babiloni,Na watamupepua na kufanya inchi yake kuwa wazi;Watakuja juu yake kwenye pande zote katika siku ya musiba.+
3 Mupiga-mishale asipinde* upinde wake.
Na mutu yeyote asisimame akiwa amevaa koti yake ya chuma.
Musionyeshe huruma yoyote kwa vijana wake.+
Muharibu jeshi lake lote.
4 Na wataanguka wakiwa wameuawa katika inchi ya Wakaldayo,Wakiwa wametobolewa kwa mukuki katika barabara zake.+
5 Kwa maana Israeli na Yuda hawakufanywa kuwa wajane na Mungu wao, na Yehova wa majeshi.+
Lakini inchi yao* imejaa hatia kwa maoni ya Mutakatifu wa Israeli.
6 Mukimbie kutoka katikati ya Babiloni,Na mukimbie ili kuokoa uzima wenu.*+
Musiangamie kwa sababu ya kosa lake.
Kwa maana ni wakati wa kisasi cha Yehova.
Anamulipa kulingana na yenye ametenda.+
7 Babiloni amekuwa kikombe cha zahabu katika mukono wa Yehova;Alilewesha dunia yote.
Mataifa yamekunywa kwenye divai yake;+Ndiyo sababu mataifa yamepatwa na wazimu.+
8 Babiloni ameanguka kwa kushitukia na amevunjika.+
Muomboleze kwa ajili yake!+
Mulete zeri kwa ajili ya maumivu yake; pengine anaweza kupona.”
9 “Tulijaribu kuponyesha Babiloni, lakini hakupona.
Mumuache na tuende, kila mumoja kwenye inchi yake.+
Kwa maana hukumu yake imefika mupaka mbinguni;Iko juu kama mawingu.+
10 Yehova ametutendea haki.+
Mukuje, tueleze katika Sayuni kazi ya Yehova Mungu wetu.”+
11 “Munoe mishale;+ muchukue ngao za muviringo.*
Yehova amechochea roho ya wafalme wa Wamedi,+Kwa sababu anakusudia kuharibu Babiloni.
Kwa maana hiki ndicho kisasi cha Yehova, kisasi kwa ajili ya hekalu lake.
12 Muinue alama*+ juu ya kuta za Babiloni.
Muimarishe ulinzi, muweke walinzi.
Mutayarishe wale wenye watavizia.
Kwa maana Yehova amefanya mupango,Na atatimiza kile chenye ameahidi juu ya wakaaji wa Babiloni.”+
13 “Ee mwanamuke mwenye kukaa juu ya maji mengi,+Mwenye hazina nyingi,+Mwisho wako umefika, mwisho wako wa* kupata faida.+
14 Yehova wa majeshi ameapa kwa nafsi yake,‘Nitakujaza watu, watu wengi kama nzige,Na watapiga vigelegele vya ushindi juu yako.’+
15 Yeye ndiye Mutengenezaji wa dunia kwa nguvu zake,Ule mwenye alifanya imara inchi yenye kuzaa kwa hekima yake+Na mwenye alitandika mbingu kwa uelewaji wake.+
16 Wakati anafanya sauti yake isikike,Maji yenye kuwa mbinguni yanakuwa na muvurugo,Na anafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia.
Anatokeza umeme wa radi* kwa ajili ya mvua,Na anatosha upepo katika madepo yake.+
17 Kila mutu anatenda kwa kukosa akili na bila ujuzi.
Kila fundi wa chuma atapatishwa haya kwa sababu ya sanamu ya kuchongwa;+Kwa maana sanamu yake ya chuma* ni uongo,Na hakuna roho* ndani yazo.+
18 Hizo ni udanganyifu,*+ kazi ya muzaha.
Wakati siku ya kuziomba zitoe hesabu itakuja, zitaangamia.
19 Fungu la Yakobo haliko kama vitu hivyo,Kwa maana Yeye ndiye alifanya kila kitu,Hata fimbo ya uriti wake.+
Yehova wa majeshi ndilo jina lake.”+
20 “Wewe ni gongo* kwangu, silaha kwa ajili ya vita,Kwa maana nitakutumia kuvunja mataifa.
Nitakutumia ili kuharibu falme.
21 Nitakutumia ili kuvunja farasi na mupandaji wake.
Nitakutumia ili kuvunja gari la vita na mupandaji wake.
22 Nitakutumia ili kuvunja mwanaume na mwanamuke.
Nitakutumia ili kuvunja muzee na kijana mudogo mwanaume.
Nitakutumia ili kuvunja kijana mwanaume na mwanamuke.
23 Nitakutumia ili kuvunja muchungaji na kundi lake.
Nitakutumia ili kuvunja mulimaji na kundi lake la wanyama.
Nitakutumia ili kuvunja magavana na watawala-wasaidizi.
24 Na nitalipa Babiloni na wakaaji wote wa UkaldayoKwa sababu ya uovu wote wenye wametenda katika Sayuni mbele ya macho yenu,”+ ni vile Yehova anasema.
25 “Angalia, nitapigana na wewe,+ Ee mulima wenye uharibifu,” ni vile Yehova anasema,“Wewe mwenye kuharibu dunia yote.+
Nitanyoosha mukono wangu juu yako na kukuviringisha kutoka kwenye miambaNa kukufanya kuwa mulima wenye uliteketezwa kwa moto.”
26 “Watu hawatakamata kutoka kwako jiwe la pembe wala jiwe la musingi,Kwa sababu utakuwa ukiwa milele,”+ ni vile Yehova anasema.
27 “Muinue alama* katika inchi.+
Mupige baragumu kati ya mataifa.
Muweke* mataifa ili yapigane naye.
Muite falme za Ararati ili zipigane naye,+ Mini, na Ashkenazi.+
Muweke juu yake ofisa mwandikishaji.
Mufanye farasi wapande kama nzige wenye kujaa miiba.
28 Muweke* mataifa ili yapigane naye,Wafalme wa Umedi,+ magavana wake na watawala wake wote wasaidiziNa inchi zote zenye wanatawala.
29 Na dunia itatetemeka na kutikisika,Kwa maana mawazo ya Yehova juu ya Babiloni yatatimizwaIli kufanya inchi ya Babiloni kuwa kitu cha kuogopesha, bila mukaaji.+
30 Wapiganaji-vita wa Babiloni wameacha kupigana.
Wanakaa katika ngome zao.
Nguvu zao zimeisha.+
Wamekuwa kama wanamuke.+
Nyumba zake zimewashwa moto.
Mapingo* yake yamevunjwa.+
31 Muleta-habari mumoja anakimbia kukutana na muleta-habari mwingine,Na mujumbe mumoja kukutana na mujumbe mwingine,Ili kujulisha mufalme wa Babiloni kwamba muji wake umekamatwa kila upande,+
32 Kwamba nafasi za kuvukia zimeshikwa,+Kwamba mashua* za mafunjo* zimeteketezwa kwa moto,Na kwamba maaskari wameingiwa na woga.”
33 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi:
“Binti ya Babiloni ni kama kiwanja cha kupigia-pigia nafaka.
Ni wakati wa kumukanyangia chini ili akuwe mugumu.
Karibuni wakati wa mavuno utakuja kwa ajili yake.”
34 “Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni amenimeza;+Amenivuruga.
Ameniweka chini kama chombo chenye kuwa wazi.
Amenimeza kama nyoka mukubwa;+Amejaza tumbo lake kwa vitu vyangu vya muzuri.
Ameniondolea mbali kwa maji.
35 ‘Jeuri yenye nilitendewa mimi na mwili wangu ikuje juu ya Babiloni!’ ni vile mukaaji wa Sayuni anasema.+
‘Na damu yangu ikuwe juu ya wakaaji wa Ukaldayo!’ ni vile Yerusalemu anasema.”
36 Kwa hiyo Yehova anasema hivi:
“Angalia, ninatetea kesi yako ya hukumu,+Na nitakulipizia kisasi.+
Nitakausha bahari yake na kukausha visima vyake.+
37 Na Babiloni atakuwa marundo ya majiwe,+Pango la mbweha,+Kitu cha kuogopesha na kitu cha kupigiwa muluzi,Bila mukaaji.+
38 Wote pamoja watanguruma kama vile wana-simba.*
Watanguruma kama watoto wa simba.”
39 “Wakati watakuwa wamesisimuka, nitafanya karamu yao na kuwalewesha,Ili wafurahi;+Kisha watalala usingizi wa kudumu,Wenye hawataamuka kutoka ndani,”+ ni vile Yehova anasema.
40 “Nitawashusha kama wana-kondoo wenye kuenda kwenye machinjo,Kama kondoo-dume pamoja na mbuzi.”
41 “Namna Sheshaki* amekamatwa,+Namna Sifa ya dunia yote imekamatwa!+
Namna Babiloni amekuwa kitu cha kuogopesha kati ya mataifa!
42 Bahari imekuja juu ya Babiloni.
Amefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake.
43 Miji yake imekuwa kitu cha kuogopesha, inchi yenye haina maji na jangwa.
Inchi yenye hakuna mutu mwenye ataishi ndani na hakuna mutu mwenye atapita ndani.+
44 Nitakaza uangalifu wangu juu ya Beli+ katika Babiloni,Na nitatosha katika kinywa chake kile chenye amemeza.+
Mataifa hayatamiminika kwake tena,Na ukuta wa Babiloni utaanguka.+
45 Mutoke katikati yake, watu wangu!+
Muponyoke ili kuokoa uzima wenu*+ kutoka kwa kasirani ya Yehova yenye kuwaka!+
46 Musikuwe na moyo wa woga wala kuogopa juu ya habari yenye itasikiwa katika inchi.
Katika mwaka mumoja habari itakuja,Na mwaka wenye kufuata habari ingine,Ya jeuri katika inchi na ya mutawala juu ya mutawala.
47 Kwa hiyo muangalie! siku zinakujaWakati nitakaza uangalifu wangu juu ya sanamu za kuchongwa za Babiloni.
Inchi yake yote itapatishwa haya,Na watu wake wote wenye waliuawa wataanguka katikati yake.+
48 Mbingu na dunia na vyote vyenye kuwa ndaniVitapiga vigelegele vya shangwe juu ya Babiloni,+Kwa maana wenye kuharibu watakuja kwake kutoka kaskazini,”+ ni vile Yehova anasema.
49 “Babiloni hakutokeza tu kuanguka kwa wenye waliuawa wa Israeli+Lakini pia kule Babiloni wenye waliuawa wa dunia yote wameanguka.
50 Ninyi wenye kuponyoka upanga, muendelee kuenda, musisimame wima!+
Mukumbuke Yehova kutoka mbali,Na Yerusalemu aingie katika moyo wenu.”+
51 “Tumepatishwa haya, kwa maana tumesikia zihaka.
Haya imefunika nyuso zetu,Kwa maana wageni* wameshambulia mahali patakatifu pa nyumba ya Yehova.”+
52 “Kwa hiyo muangalie! siku zinakuja,” ni vile Yehova anasema,“Wakati nitakaza uangalifu wangu juu ya sanamu zake za kuchongwa,Na katika inchi yake yote wenye waliumizwa watalia kwa maumivu.”+
53 “Hata Babiloni akipanda mbinguni,+Hata akiimarisha ngome zake za murefu,Wenye kumuharibu watakuja kutoka kwangu,”+ ni vile Yehova anasema.
54 “Musikilize! Kuko kilio kutoka Babiloni,+Sauti ya musiba mukubwa kutoka inchi ya Wakaldayo,+
55 Kwa maana Yehova anaharibu Babiloni,Atanyamazisha sauti yake kubwa,Na mawimbi yao yatavuma kama maji mengi.
Makelele ya sauti yao yatasikika.
56 Kwa maana mwenye kuharibu atakuja juu ya Babiloni;+Wapiganaji-vita wake watakamatwa,+Pinde zao zitavunjwa-vunjwa,Kwa maana Yehova ni Mungu wa kisasi.+
Hakika atalipa.+
57 Nitalewesha wakubwa wake na watu wake wenye hekima,+Magavana wake na watawala wake wasaidizi na wapiganaji-vita wake,Na watalala usingizi wa kudumu,Wenye hawataamuka kutoka ndani,”+ ni vile Mufalme anasema, yeye mwenye jina lake ni Yehova wa majeshi.
58 Yehova wa majeshi anasema hivi:
“Ukuta wa Babiloni, hata kama ni mupana, utabomolewa kabisa,+Na milango yake mikubwa, hata kama ni mirefu, itawashwa moto.
Vikundi vya watu vitafanya kazi ya jasho bure;Mataifa yatajichokesha ili tu kuchochea moto.”+
59 Hili ndilo neno lenye Yeremia nabii alimuamuru Seraya mwana wa Neria+ mwana wa Mahseya wakati alienda na Mufalme Sedekia wa Yuda kule Babiloni katika mwaka wa ine (4) wa utawala wake; Seraya alikuwa musimamizi wa makao.
60 Yeremia aliandika katika kitabu kimoja musiba wote wenye ungekuja juu ya Babiloni, maneno haya yote yenye yaliandikwa juu ya Babiloni.
61 Zaidi ya hayo, Yeremia alimuambia Seraya: “Wakati utafika Babiloni na kuona muji huo, unapaswa kusoma kwa sauti kubwa maneno haya yote.
62 Kisha useme, ‘Ee Yehova, umesema juu ya mahali hapa kwamba pataharibiwa na kuachwa bila mukaaji, mwanadamu wala munyama, na kwamba atakuwa ukiwa milele.’+
63 Na wakati utamaliza kusoma kitabu hiki, ukifunge kwenye jiwe na kukitupa katikati ya Efrati.
64 Kisha useme: ‘Ni hivi Babiloni atazama na hatainuka tena hata siku moja+ kwa sababu ya musiba wenye ninaleta juu yake; na watachoka.’”+
Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.
Maelezo ya Chini
^ Inaonekana hili ni jina la siri la Ukaldayo.
^ Tnn., “asikanyange.”
^ Ni kusema, inchi ya Wakaldayo.
^ Ao “nafsi yenu.”
^ Ao pengine, “mujaze mifuko ya mishale.”
^ Ao “nguzo ya alama.”
^ Tnn., “kipimo chako cha.”
^ Ao “anafanya mivuke ipande.”
^ Ao pengine, “milango.”
^ Ao “sanamu yake ya kuyeyushwa.”
^ Ao “pumuzi.”
^ Ao “ubatili.”
^ Gongo ni fimbo yenye kuvimba kwenye mwisho wake mumoja.
^ Ao “nguzo ya alama.”
^ Tnn., “Mutakase.”
^ Tnn., “Mutakase.”
^ Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
^ Ao “mashua za maji; bateaux.”
^ Ao “papyrus.” Angalia Maana ya Maneno.
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Ao “wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
^ Inaonekana hili ni jina la siri la Babeli (Babiloni).
^ Ao “nafsi zenu.”
^ Ao “watu wa inchi ya kigeni.”