Yeremia 16:1-21

  • Yeremia hapaswe kuoa, kuomboleza, wala kufanya karamu (1-9)

  • Azabu, kisha kurudishwa (10-21)

16  Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2  “Haupaswe kujichukulia bibi, na haupaswe kuwa na watoto wanaume na watoto wanamuke mahali hapa. 3  Kwa maana Yehova anasema hivi juu ya watoto wanaume na watoto wanamuke wenye wanazaliwa hapa na juu ya mama zao wenye wanawazaa na juu ya baba zao wenye wanawazaa katika inchi hii: 4  ‘Watakufa kwa magonjwa yenye kuua,+ lakini hakuna mwenye atawaombolezea wala kuwazika; watakuwa kama mbolea juu ya uso wa inchi.+ Watakufa kwa upanga na kwa njaa,+ na maiti zao zitakuwa chakula kwa ndege wa mbinguni na kwa wanyama wa dunia.’  5  Kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Usiingie katika nyumba yenye ndani yake munafanyika karamu ya waombolezaji,Na usiende kuomboleza wala kutoa pole,’+‘Kwa maana nimeondoa amani yangu kwa watu hawa,’ ni vile Yehova anasema,‘Pamoja na upendo wangu mushikamanifu na rehema.+  6  Wakubwa na wadogo pia watakufa katika inchi hii. Hawatazikwa,Hakuna mutu mwenye atawaombolezea,Ao mutu yeyote mwenye atajikata-kata wala kujitia upara kwa ajili yao.*  7  Na hakuna mutu mwenye atapatia chakula wale wenye kuwa katika maombolezo,Ili kuwafariji juu ya mutu wao mwenye alikufa;Na hakuna mutu yeyote mwenye atawapatia kikombe cha farajaIli kunywa kwa sababu ya kupoteza baba yao ao mama yao.  8  Na usiingie katika nyumba ya karamuIli kukaa pamoja nao ili kula na kunywa.’ 9  “Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Angalia, katika mahali hapa, katika siku zenu na mbele ya macho yenu, nitamaliza sauti za furaha na shangwe, sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi.’+ 10  “Wakati utaambia watu hawa maneno haya yote, watakuuliza, ‘Sababu gani Yehova amesema kuhusu musiba wote huu mukubwa juu yetu? Ni kosa gani na zambi gani tumemutendea Yehova Mungu wetu?’+ 11  Unapaswa kuwajibu, ‘“Kwa sababu mababu zenu waliniacha,”+ ni vile Yehova anasema, “na waliendelea kufuata miungu mingine na kuitumikia na kuiinamia.+ Lakini waliniacha, na sheria yangu hawakuishika.+ 12  Na mumejiendesha mubaya zaidi kuliko mababu zenu,+ na kila mumoja wenu anafuata ugumu wa moyo wake muovu kuliko kunitii.+ 13  Basi nitawatupa ninyi inje ya inchi hii katika inchi yenye ninyi wala mababu zenu hamukujua,+ na kule mutatumikia miungu mingine muchana na usiku,+ kwa sababu sitawaonyesha wema wowote.”’ 14  “‘Hata hivyo, siku zinakuja,’ ni vile Yehova anasema, ‘wakati hawatasema tena: “Kama vile hakika Yehova anaishi, mwenye alitosha watu wa Israeli katika inchi ya Misri!”+ 15  lakini tofauti na hilo: “Kama vile hakika Yehova anaishi, mwenye alitosha watu wa Israeli katika inchi ya kaskazini na katika inchi zote kwenye alikuwa amewatawanya!” na nitawarudisha kwenye inchi yao, yenye nilipatia mababu zao.’+ 16  ‘Angalia, ninaita wavuvi wengi wa samaki,’ ni vile Yehova anasema,‘Na watawavua. Kisha, nitaita wawindaji wengi,Na watawawinda kwenye kila mulima na kila kilimaNa kutoka katika mipasuko ya miamba. 17  Kwa maana macho yangu yako juu ya kila kitu chenye wanafanya.* Hawakufichwa kutoka mbele yangu,Wala kosa lao halikufichwa kutoka mbele ya macho yangu. 18  Kwanza, nitalipa kiasi kamili chenye kustahili kosa lao na zambi yao,+Kwa maana wamechafua inchi yangu kwa mifano yenye haina uzima ya* sanamu zao zenye kuchukizaNa wamejaza uriti wangu mambo yao yenye kuchukiza.’”+ 19  Ee Yehova, nguvu zangu na ngome yangu,Mahali pangu pa kukimbilia katika siku ya taabu,+Kwako mataifa yatakuja kutoka kwenye miisho ya dunia,Na watasema: “Mababu zetu waliriti uongo kabisa,Mambo ya bure kabisa* na vitu vyenye havina mafaa, vyenye havina faida yoyote.”+ 20  Je, mwanadamu anaweza kujitengenezea miunguWakati kwa kweli hiyo haiko miungu?+ 21  “Basi nitawafanya wajue;Wakati huu nitawafanya wajue nguvu zangu na uwezo wangu,Na watajua kwamba jina langu ni Yehova.”

Maelezo ya Chini

Desturi ya kipagani ya kuomboleza yenye inawezekana ilifanywa katika Israeli yenye iliasi imani.
Tnn., “juu ya njia zao zote.”
Tnn., “kwa maiti za.”
Ao “Ubatili.”