Yeremia 35:1-19
-
Warekabu wanaonyesha utii wa pekee (1-19)
35 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova katika siku za Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, na kusema:
2 “Uende katika nyumba ya Warekabu+ na useme nao na kuwaleta katika nyumba ya Yehova, katika kimoja cha vyumba vya kukulia chakula;* na uwapatie divai wakunywe.”
3 Basi nikapeleka Yaazania mwana wa Yeremia mwana wa Habasinia, ndugu zake, wana wake wote, na nyumba yote ya Warekabu
4 katika nyumba ya Yehova. Nikawaleta kwenye chumba cha kukulia chakula cha wana wa Hanani mwana wa Igdalia, mutu wa Mungu wa kweli, chenye kilikuwa pembeni ya chumba cha kukulia chakula cha wakubwa chenye kilikuwa juu ya chumba cha kukulia chakula cha Maaseya mwana wa Shalumu mulinzi wa mulango.
5 Kisha nikaweka vikombe na bilauri vyenye kujaa divai mbele ya watu wa nyumba ya Warekabu na kuwaambia: “Mukunywe divai.”
6 Lakini wakasema: “Hatutakunywa divai, kwa sababu Yehonadabu*+ mwana wa Rekabu, babu yetu, alitupatia amri hii: ‘Ninyi ao wana wenu hamupaswe hata siku moja kunywa divai.
7 Na hamupaswe kujenga nyumba, kupanda mbegu, wala kupanda wala kuwa na shamba la mizabibu. Tofauti na hilo, munapaswa kukaa katika mahema sikuzote, ili muishi wakati murefu katika inchi yenye munaishi ndani mukiwa wageni.’
8 Basi tunaendelea kutii sauti ya Yehonadabu mwana wa Rekabu babu yetu katika mambo yote yenye alituamuru, kwa kutokunywa hata siku moja divai yoyote—sisi, bibi zetu, watoto wetu wanaume, na watoto wetu wanamuke.
9 Na hatujenge nyumba za kukaa ndani, na hatuna mizabibu wala mashamba wala mbegu.
10 Tunaendelea kuishi katika mahema na kutii mambo yote yenye Yehonadabu* babu yetu alituamuru.
11 Lakini wakati Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni alipanda ili kushambulia inchi,+ tukasema, ‘Mukuje, tuingie ndani ya Yerusalemu ili kuponyoka jeshi la Wakaldayo na la Wasiria,’ na sasa tunaishi katika Yerusalemu.”
12 Na neno la Yehova likakuja kwa Yeremia, na kusema:
13 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Uende na uambie watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu: “Je, hamukuendelea kuchochewa mutii maneno yangu?”+ ni vile Yehova anasema.
14 “Yehonadabu mwana wa Rekabu aliamuru wazao wake wasikunywe divai, na wamefuata maneno yake kwa kutoikunywa mupaka leo, na hivyo wametii agizo la babu yao.+ Hata hivyo, nimesema na ninyi tena na tena,* lakini hamukunitii.+
15 Na niliendelea kutuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nikiwatuma tena na tena,*+ na kusema, ‘Tafazali, murudie, kila mumoja wenu kutoka kwenye njia zenu za uovu,+ na mufanye mambo yenye kuwa sawa! Musifuate miungu mingine na kuitumikia. Halafu mutaendelea kukaa katika inchi yenye niliwapatia ninyi na mababu zenu.’+ Lakini hamukutega sikio lenu wala kunisikiliza.
16 Wazao wa Yehonadabu mwana wa Rekabu wamefuata agizo lenye babu yao aliwapatia,+ lakini watu hawa, hawakunisikiliza.”’”
17 “Kwa hiyo Yehova, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Angalia, ninaleta juu ya Yuda na juu ya wakaaji wote wa Yerusalemu musiba wote wenye niliwaonya kuuhusu,+ kwa maana nimesema nao, lakini hawakusikiliza, na niliendelea kuwaita, lakini hawakujibu.’”+
18 Na Yeremia akaambia nyumba ya Warekabu: “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kwa sababu mumetii agizo la babu yenu Yehonadabu na munaendelea kushika maagizo yake yote, na kufanya kabisa mambo yenye aliwaagiza ninyi,
19 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Hakutakosekana hata siku moja muzao wa Yehonadabu* mwana wa Rekabu mwenye atatumika mbele yangu.”’”
Maelezo ya Chini
^ Ao “vyumba.”
^ Tnn., “Yonadabu,” kifupi cha jina Yehonadabu.
^ Tnn., “Yonadabu,” kifupi cha jina Yehonadabu.
^ Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.
^ Tnn., “nikiamuka asubui sana na kusema.”
^ Tnn., “nikiamuka asubui sana na kutuma.”
^ Tnn., “Yonadabu,” kifupi cha jina Yehonadabu.