Yeremia 8:1-22
8 “Wakati huo,” ni vile Yehova anasema, “mifupa ya wafalme wa Yuda, mifupa ya wakubwa wake, mifupa ya makuhani, mifupa ya manabii, na mifupa ya wakaaji wa Yerusalemu itachukuliwa kutoka katika makaburi yao.
2 Itatandikwa mbele ya jua na mbele ya mwezi na mbele ya jeshi lote la mbinguni vyenye wamependa na kutumikia na kufuata na kutafuta na kuinamia.+ Haitakusanywa, na haitazikwa. Itakuwa kama mbolea juu ya uso wa inchi.”+
3 “Na mabaki ya familia hii yenye uovu wenye wataokoka watachagua kifo kuliko uzima katika sehemu zote kwenye nitawatawanya,” ni vile Yehova wa majeshi anasema.
4 “Na unapaswa kuwaambia, ‘Yehova anasema hivi:
“Je, wataanguka na wasisimame tena?
Kama mutu mumoja anarudia, je, ule mwingine hatarudia pia?
5 Sababu gani watu hawa, Yerusalemu, wanakosa uaminifu kwa ukosefu wa uaminifu wenye kudumu?
Wanashikilia sana udanganyifu;Wanakataa kurudia.+
6 Nilitega sikio na kuendelea kusikiliza, lakini namna walikuwa wanasema haikukuwa sawa.
Hakuna mutu mwenye alitubu uovu wake ao kuuliza, ‘Nimefanya nini?’+
Kila mumoja anaendelea kurudia kwenye njia yenye inapendwa na wengi, kama farasi mwenye anakimbilia kwenye pigano.
7 Hata korongo katika anga anajua vipindi vyake;*Njiwa-tetere na ndege teleka na ndege kuruwiji* hawasahau wakati wao wa kurudia.*
Lakini watu wangu mwenyewe hawaelewe hukumu ya Yehova.”’+
8 ‘Namna gani munaweza kusema: “Tuko na hekima, na tuko na sheria ya* Yehova”?
Kwa maana hakika, kalamu ya uongo+ ya waandishi imetumiwa tu kwa ajili ya uongo.
9 Wenye hekima wamepatishwa haya.+
Wameingiwa na woga na watakamatwa.
Angalia! Wamekataa neno la Yehova,Na wako na hekima gani?
10 Basi nitapatia wanaume wengine bibi zao,Mashamba yao nitayapatia watu wengine;+Kwa maana kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi, kila mumoja anajipatia faida yenye haiko ya haki;+Kuanzia nabii mupaka kuhani, kila mumoja anatenda kwa upunjaji.+
11 Na wanajaribu kuponyesha kijuujuu kuvunjika kwa binti ya watu wangu, wakisema,“Kuko amani! Kuko amani!”
Wakati hakuna amani.+
12 Je, wanasikia haya kwa sababu ya mambo yenye kuchukiza yenye wamefanya?
Hawasikie haya hata kidogo!
Hata hawajue namna ya kufezeheka!+
Basi wataanguka kati ya wale wenye kuanguka.
Wakati nitaleta azabu juu yao watajikwaa,”+ ni vile Yehova anasema.
13 ‘Wakati nitawakusanya, nitawafikisha kwenye mwisho wao,’ ni vile Yehova anasema.
‘Hakutakuwa zabibu zenye kubakia kwenye muzabibu, ao tini kwenye muti wa tini, na majani yatakauka.
Na watapoteza kile chenye niliwapatia.’”
14 “Sababu gani tunakaa hapa?
Tukusanyike pamoja na tuingie katika miji yenye ngome+ na tuangamie mule.
Kwa maana Yehova Mungu wetu atatuharibu,Na anatupatia maji yenye sumu tukunywe,+Kwa sababu tumemutendea Yehova zambi.
15 Kulikuwa tumaini la kupata amani, lakini hakuna mema yenye yalikuja,Tumaini la kupata kipindi cha kuponyeshwa, lakini kuko woga!+
16 Kukoroma kwa farasi wake kumesikiwa kutoka Dani.
Kwa sauti ya mulio wa farasi-dume wake,Inchi nzima inatetemeka.
Wanaingia na kurarua inchi na kila kitu chenye kuwa ndani,Muji na wakaaji wake.”
17 “Kwa maana angalia, ninatuma nyoka kati yenu,Nyoka wenye sumu wenye hawawezi kuchezeshwa,Na hakika watawauma ninyi,” ni vile Yehova anasema.
18 Huzuni yangu haiwezi kupona;Moyo wangu ni mugonjwa.
19 Kutoka inchi ya mbali kuko kilio cha kuomba musaadaKutoka kwa binti ya watu wangu:
“Je, Yehova haiko katika Sayuni?
Ao je, mufalme wake haiko ndani yake?”
“Sababu gani wamenikasirisha kupitia sanamu zao za kuchongwa,Kupitia miungu yao ya kigeni yenye haina mafaa yoyote?”
20 “Mavuno yamepita, kipindi cha joto kimeisha,Lakini hatukuokolewa!”
21 Nimevunjwa-vunjwa kwa sababu ya kuvunjika kwa binti ya watu wangu;+Nimehuzunika.
Nimeshikwa na woga.
22 Je, hakuna zeri* katika Gileadi?+
Ao, je, hakuna muponyaji* kule?+
Sababu gani binti ya watu wangu hakuponyeshwa?+
Maelezo ya Chini
^ Ao “nyakati zake zenye ziliwekwa.”
^ Ao pengine, “korongo.”
^ Ao “kuhama.”
^ Ao “agizo la.”
^ Ao “mafuta yenye kutuliza.”
^ Ao “munganga.”