Yeremia 47:1-7
-
Unabii juu ya Wafilisti (1-7)
47 Hili ndilo neno la Yehova kwa Yeremia nabii kuhusu Wafilisti,+ mbele ya Farao kupiga Gaza.
2 Yehova anasema hivi:
“Angalia! Maji yanakuja kutoka kaskazini.
Yatakuwa muto wenye kujaa sana.
Na yataleta mafuriko juu ya inchi na juu ya kila kitu chenye kuwa ndani yake,Muji na wale wenye kukaa ndani.
Watu watalia kwa sauti kubwa,Na kila mutu mwenye anaishi katika inchi ataomboleza.
3 Kutokana na sauti ya kishindo cha kwato* za farasi-dume wake,Kutokana na mulio wa magari yake ya vitaNa kunguruma kwa magurudumu* yake,Baba hawatageuka hata kwa ajili ya wana wao,Kwa maana mikono yao inaregea,
4 Kwa sababu siku yenye inakuja itaharibu Wafilisti wote;+Itaondoa katika Tiro+ na katika Sidoni+ kila musaidizi mwenye kubakia.
Kwa maana Yehova ataharibu Wafilisti,Wenye wamebakia kutoka kisiwa cha Kaftori.*+
5 Upara* utakuja Gaza.
Ashkeloni imenyamazishwa.+
Ee mabaki ya bonde lao tambarare,*Utaendelea kujikata-kata mupaka wakati gani?+
6 “Aa! Upanga wa Yehova!+
Hautanyamaza mupaka wakati gani?
Rudia ndani ya mufuko wako wa upanga.
Pumuzika na unyamaze.
7 Namna gani unaweza kukaa kimyaWakati Yehova ameuamuru?
Juu ya Ashkeloni na eneo la pembeni ya bahari,+Ni pale amechagua ukuwe.”
Maelezo ya Chini
^ Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.
^ Ao “mipeto; pneus.”
^ Ni kusema, Krete.
^ Ni kusema, watanyoa vichwa vyao kwa kuomboleza na kwa haya.
^ Ao “eneo tambarare la chini.”