Yeremia 20:1-18

  • Pashuri anamupiga Yeremia (1-6)

  • Yeremia hawezi kuacha kuhubiri (7-13)

    • Ujumbe wa Mungu kama moto wenye kuwaka (9)

    • Yehova kama mupiganaji-vita mwenye kuogopesha (11)

  • Malalamiko ya Yeremia (14-18)

20  Sasa Pashuri mwana wa Imeri, kuhani, mwenye alikuwa pia musimamizi mukubwa katika nyumba ya Yehova, alikuwa anasikiliza wakati Yeremia alikuwa anatoa unabii wa mambo hayo. 2  Kisha Pashuri akamupiga Yeremia nabii na kumuweka katika mikatale+ yenye ilikuwa kwenye Mulango Mukubwa wa Juu wa Benyamini, wenye ulikuwa katika nyumba ya Yehova. 3  Lakini katika siku yenye ilifuata wakati Pashuri alimutosha Yeremia katika ile mikatale, Yeremia akamuambia: “Yehova amekupatia jina, hapana Pashuri, lakini Woga Pande Zote.+ 4  Kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Nitakufanya kuwa kitu cha kuogopesha kwako wewe mwenyewe na kwa marafiki wako wote, na wataanguka kwa upanga wa maadui wao wakati macho yako yatakuwa yanaangalia;+ na nitatia watu wote wa Yuda katika mukono wa mufalme wa Babiloni, na atawapeleka katika uhamisho kule Babiloni na kuwaua kwa upanga.+ 5  Na nitatia utajiri wote wa muji huu, mali yake yote, vitu vyake vyote vyenye samani, na hazina zote za wafalme wa Yuda katika mukono wa maadui wao.+ Na watavinyanganya na kuvikamata na kuvipeleka Babiloni.+ 6  Na wewe, Pashuri, na wote wenye wanaishi katika nyumba yako, mutaenda katika utekwa. Utaenda Babiloni na kufa kule, na utazikwa kule pamoja na marafiki wako wote, kwa sababu umewatolea unabii wa uongo.’”+  7  Umenipumbaza, Ee Yehova, na nikapumbazika. Ulitumia nguvu zako ili kunipinga, na ukashinda.+ Nimekuwa kitu cha kuchekwa muchana wote;Kila mutu ananichekelea.+  8  Kwa maana kila mara wakati ninasema, ninapaswa kulia na kutangaza,“Jeuri na uharibifu!” Kwangu neno la Yehova limekuwa sababu ya kutukanwa na kuchekwa muchana wote.+  9  Basi nikasema: “Sitamutaja,Na sitasema tena katika jina lake.”+ Lakini katika moyo wangu hilo lilikuwa kama moto wenye kuwaka wenye kufungiwa katika mifupa yangu,Na nikachoka kulizuia;Singeweza tena kuvumilia.+ 10  Kwa maana nilisikia habari nyingi za uovu zenye haziko hakika;Woga ulinizunguka.+ “Mumushitaki; tumushitaki!” Kila mutu mwenye kunitakia amani alikuwa anangojea nianguke:+ “Pengine atafanya kosa la upumbavu,Na tunaweza kushinda na kujilipizia kisasi juu yake.” 11  Lakini Yehova alikuwa pamoja na mimi kama mupiganaji-vita mwenye kuogopesha.+ Ndiyo sababu wale wenye kunitesa watajikwaa na hawatashinda.+ Watapatishwa haya kubwa, kwa maana hawatafanikiwa. Haya yao ya milele haitasahauliwa.+ 12  Lakini wewe, Ee Yehova wa majeshi, unachunguza mwenye haki;Unaona mawazo ya ndani kabisa* na moyo.+ Acha nione kisasi chako juu yao,+Kwa maana nimeleta kesi yangu ya hukumu kwako.+ 13  Mumuimbie Yehova! Mumusifu Yehova! Kwa maana amekomboa maskini* kutoka katika mukono wa watenda-maovu. 14  Ilaaniwe siku yenye nilizaliwa! Siku yenye mama yangu alinizaa isibarikiwe!+ 15  Alaaniwe mutu mwenye alimuletea baba yangu habari njema, akisema: “Mwana amezaliwa kwako, kijana mwanaume!” Na kumufanya afurahi sana. 16  Mutu huyo akuwe kama miji yenye Yehova aliharibu bila kusikitika. Asikie kilio asubui na sauti ya mulio ya katikati ya muchana. 17  Sababu gani hakuniua ndani ya tumbo la uzazi,Ili mama yangu akuwe kaburi languNa tumbo lake la uzazi likuwe na mimba sikuzote?+ 18  Sababu gani iliomba nitoke ndani ya tumbo la uzaziIli kuona taabu na huzuni,Ili kumaliza siku zangu katika haya?+

Maelezo ya Chini

Ao “hisia za ndani kabisa.” Tnn., “figo.”
Ao “nafsi ya maskini.”