Mwanzo 50:1-26

50  Ndipo Yosefu akauangukia uso wa baba yake,+ akamlilia na kumbusu.+  Kisha Yosefu akawaamuru watumishi wake, matabibu, wampake baba yake dawa ya kumfanya asioze.+ Basi wakampaka Israeli dawa ya kumfanya asioze,  nao wakatumia siku 40 kamili kwa ajili yake, kwa maana hiyo ndiyo hesabu ya siku ambazo kwa desturi wao hutumia kupaka dawa ya kumfanya mtu asioze, nao Wamisri wakaendelea kumlilia siku 70.+  Mwishowe siku za kumlilia zikapita, na Yosefu akawaambia watu wa nyumba ya Farao, akisema: “Ikiwa, sasa, nimepata kibali machoni penu,+ tafadhali, nendeni mkaseme masikioni mwa Farao, na kumwambia,  ‘Baba yangu aliniapisha,+ akisema: “Tazama! Ninakufa.+ Katika kaburi ambalo nimechimba mwenyewe katika nchi ya Kanaani+ ndipo utakaponizika.”+ Na sasa, tafadhali, niruhusu niende huko, nikamzike baba yangu, kisha nitarudi.’”  Basi Farao akasema: “Nenda ukamzike baba yako kama alivyokuapisha.”+  Kwa hiyo Yosefu akaenda kumzika baba yake, na watumishi wote wa Farao, wanaume wazee+ wa nyumba yake na wanaume wote wazee wa nchi ya Misri, wakapanda kwenda pamoja naye,  na watu wote wa nyumba ya Yosefu na ndugu zake na nyumba ya baba yake.+ Waliacha tu katika nchi ya Gosheni watoto wao wadogo na makundi yao na mifugo yao.  Pia magari+ na wapanda-farasi walienda pamoja naye, nayo kambi ikawa na idadi kubwa sana. 10  Kisha wakafika kwenye uwanja wa kupuria+ wa Atadi, ulio katika eneo la Yordani,+ na huko wakaomboleza maombolezo makuu sana na kulia sana, naye akafanya desturi za kuomboleza kwa ajili ya baba yake kwa siku saba.+ 11  Nao wakaaji wa nchi hiyo, Wakanaani, wakaona desturi za kuomboleza katika uwanja wa kupuria wa Atadi, nao wakasema: “Haya ni maombolezo makuu ya Wamisri!” Ndiyo sababu mahali hapo paliitwa Abel-misraimu, palipo katika eneo la Yordani.+ 12  Nao wanawe wakamfanyia kama vile tu alivyokuwa amewaamuru.+ 13  Kwa hiyo wanawe wakampeleka mpaka nchi ya Kanaani na kumzika katika pango la shamba la Makpela, shamba ambalo Abrahamu alikuwa amenunua kutoka kwa Efroni Mhiti mbele ya Mamre+ ili awe na mahali pa kuzikia. 14  Baada ya kumzika baba yake, Yosefu akarudi Misri, yeye na ndugu zake na wale wote waliokwenda pamoja naye kumzika baba yake. 15  Ndugu za Yosefu walipoona kwamba baba yao amekufa, wakaanza kusema: “Huenda ikawa Yosefu anatuwekea uadui+ naye hakika atatulipiza kwa sababu ya uovu wote ambao tumemtendea.”+ 16  Basi wakamjulisha Yosefu amri kwa maneno haya: “Baba yako alitoa amri hii kabla ya kifo chake, akisema, 17  ‘Mtamwambia Yosefu hivi: “Tafadhali, nakuomba, usamehe+ maasi ya ndugu zako na dhambi yao kwa kuwa wamekutendea uovu.”’+ Na tafadhali sasa, usamehe maasi ya watumishi wa Mungu wa baba yako.”+ Naye Yosefu akalia waliposema naye. 18  Halafu ndugu zake pia wakaja na kuanguka chini mbele yake. Wakamwambia: “Tazama, sisi ni kama watumwa kwako!”+ 19  Ndipo Yosefu akawaambia: “Msiogope, kwa maana je, mimi niko mahali pa Mungu?+ 20  Kwa upande wenu, ninyi mlikuwa na uovu akilini mwenu kunielekea mimi. Mungu alikuwa na wema akilini kwa kusudi la kutenda kama ilivyo leo hii ili kuhifadhi hai watu wengi.+ 21  Kwa hiyo sasa msiogope. Mimi nitaendelea kuwapa chakula ninyi na watoto wenu wadogo.”+ Basi akawafariji na kusema nao kwa kuwatuliza. 22  Na Yosefu akaendelea kukaa Misri, yeye na nyumba ya baba yake; na Yosefu akaishi miaka mia moja na kumi. 23  Na Yosefu akapata kuona wana wa Efraimu wa kizazi cha tatu,+ pia wana wa Makiri,+ mwana wa Manase. Walizaliwa juu ya magoti ya Yosefu.+ 24  Mwishowe Yosefu akawaambia ndugu zake: “Ninakufa; lakini Mungu hatakosa kuwaelekezea fikira zake,+ naye kwa hakika atawatoa katika nchi hii na kuwapeleka mpaka nchi ambayo aliwaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”+ 25  Basi Yosefu akawaapisha wana wa Israeli, akisema: “Mungu hatakosa kuwaelekezea fikira zake. Kwa hiyo mwichukue mifupa yangu kutoka huku.”+ 26  Kisha Yosefu akafa akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi; nao wakampaka dawa ya kumfanya asioze,+ naye akatiwa ndani ya sanduku huko Misri.

Maelezo ya Chini