Mwanzo 30:1-43

30  Raheli alipoona kwamba alikuwa hajamzalia Yakobo mwana yeyote, Raheli akamwonea wivu dada yake naye akaanza kumwambia Yakobo:+ “Nipe watoto, kama sivyo nitakufa mimi.”+  Kwa hiyo hasira ya Yakobo ikawaka juu ya Raheli naye akasema:+ “Je, mimi niko badala ya Mungu, ambaye amekuzuilia uzao wa tumbo?”+  Basi yeye akasema: “Kijakazi wangu Bilha+ huyu. Lala naye, apate kuzaa magotini pangu ili kwamba mimi, naam mimi, nipate watoto kwake.”+  Basi akampa Bilha mjakazi wake awe mke na Yakobo akalala naye.+  Na Bilha akapata mimba na baada ya muda akamzalia Yakobo mwana.+  Ndipo Raheli akasema: “Mungu ametenda kama mwamuzi+ wangu na pia ameisikiliza sauti yangu, akanipa mwana.” Ndiyo sababu alimwita jina lake Dani.+  Na Bilha, mjakazi wa Raheli, akapata mimba mara nyingine tena, na baada ya muda akamzalia Yakobo mwana wa pili.  Kisha Raheli akasema: “Nimepigana miereka yenye nguvu na dada yangu. Nami nimekuwa mshindi!” Kwa hiyo akamwita jina lake Naftali.+  Lea alipoona kwamba ameacha kuzaa, akamchukua Zilpa mjakazi wake akampa Yakobo kuwa mke.+ 10  Baada ya muda Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana. 11  Ndipo Lea akasema: “Neema!” Basi akamwita jina lake Gadi.+ 12  Baada ya hayo, Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana wa pili. 13  Kisha Lea akasema: “Pamoja na furaha yangu! Kwa maana binti watanitangaza kuwa mwenye furaha.”+ Basi akamwita jina lake Asheri.+ 14  Ndipo Rubeni+ akaenda kutembea siku za mavuno ya ngano,+ akapata dudai shambani. Kwa hiyo akazileta kwa Lea mama yake. Kisha Raheli akamwambia Lea: “Tafadhali, nipe baadhi ya dudai za mwana wako.”+ 15  Akajibu akamwambia: “Je, hili ni jambo dogo, kwamba wewe umemchukua mume wangu,+ na sasa wewe uzichukue pia dudai za mwanangu?” Basi Raheli akasema: “Kwa sababu hiyo yeye atalala nawe usiku wa leo kwa kubadilishana na dudai za mwana wako.” 16  Yakobo alipokuwa akitoka shambani jioni,+ Lea akaenda kumpokea kisha akasema: “Utalala nami, kwa sababu nimekukodi moja kwa moja kwa dudai za mwanangu.” Basi akalala naye usiku huo.+ 17  Basi Mungu akamsikia na kumjibu Lea naye akapata mimba na baada ya muda akamzalia Yakobo mwana wa tano.+ 18  Kisha Lea akasema: “Mungu amenipa mshahara wa mtu wa kukodiwa, kwa sababu nimempa mume wangu mjakazi wangu.” Kwa hiyo akamwita jina lake Isakari.+ 19  Lea akapata mimba mara nyingine tena na baada ya muda akamzalia Yakobo mwana wa sita.+ 20  Ndipo Lea akasema: “Mungu amenipa kipawa, ndiyo, kipawa chema. Mwishowe mume wangu atanivumilia,+ kwa sababu nimemzalia wana sita.”+ Basi akamwita jina lake Zabuloni.+ 21  Na baadaye akazaa binti kisha akamwita jina lake Dina.+ 22  Mwishowe Mungu akamkumbuka Raheli, naye Mungu akamsikia na kumjibu kwa kuwa alifungua tumbo lake la uzazi.+ 23  Naye akapata mimba, akazaa mwana. Kisha akasema: “Mungu ameondolea mbali shutuma yangu!”+ 24  Basi akamwita jina lake Yosefu,+ akisema: “Yehova ananiongezea mwana mwingine.” 25  Ikawa kwamba Raheli alipokuwa amemzaa Yosefu, bila kukawia Yakobo akamwambia Labani: “Niruhusu niende kwangu na katika nchi yangu.+ 26  Nipe wake zangu na watoto wangu, ambao kwa ajili yao nimekutumikia, ili nipate kwenda; kwa maana wewe mwenyewe unajua utumishi wangu ambao nimekutolea.”+ 27  Ndipo Labani akamwambia: “Ikiwa, sasa, nimepata kibali machoni pako,—nimezifasiri zile ishara za bahati zinazoonyesha kwamba Yehova ananibariki kwa ajili yako.”+ 28  Naye akaongezea kusema: “Niambie masharti ya mshahara wako nami nitayatimiza.”+ 29  Basi akamwambia hivi: “Wewe mwenyewe unajua jinsi nimekutumikia na jinsi hali ya mifugo yako imekuwa mkononi mwangu;+ 30  kwamba kwa kweli ulikuwa na kidogo kabla ya kuja kwangu, nayo ikaendelea kuongezeka na kuwa mingi, kwa kuwa Yehova alikubariki tangu nilipoingia.+ Basi sasa ni wakati gani mimi nitafanya jambo pia kwa ajili ya nyumba yangu mwenyewe?”+ 31  Kisha akasema: “Nikupe nini?” Naye Yakobo akaendelea kusema: “Hutanipa chochote kamwe!+ Ukinitendea jambo hili, mimi nitaanza tena kuchunga kundi lako.+ Nitaendelea kulilinda.+ 32  Mimi nitapita kati ya kundi lako lote leo. Wewe uweke kando kutoka hapo kila kondoo mwenye mabaka na mwenye madoa-doa ya rangi, na kila kondoo mwenye rangi ya kahawia kati ya wana-kondoo dume na yeyote kati ya mbuzi-jike mwenye madoa-doa ya rangi na mabaka. Baada ya hapo hao wawe mshahara wangu.+ 33  Na wema wangu niliotenda utanitetea siku yoyote ya baadaye ambayo huenda ukaja kuutazama mshahara wangu;+ kila mmoja asiye na mabaka na madoa-doa ya rangi kati ya mbuzi-jike na rangi ya kahawia kati ya wana-kondoo dume ni kitu kilichoibwa ikiwa yupo pamoja nami.”+ 34  Labani akajibu akasema: “Ni vema! Na iwe kulingana na neno lako.”+ 35  Kisha akaweka kando siku hiyo mbuzi-dume wenye mistari-mistari na madoa-doa ya rangi na mbuzi-jike wote wenye mabaka na madoa-doa ya rangi, kila mmoja kati ya wana-kondoo dume aliyekuwa na weupe wowote na kila mmoja wa rangi ya kahawia, lakini akawatia mikononi mwa wanawe. 36  Baada ya hayo akaenda kukaa umbali wa safari ya siku tatu kati yake na Yakobo, na Yakobo alikuwa akichunga mifugo ya Labani iliyobaki. 37  Kisha Yakobo akachukua fimbo zilizokuwa bado mbichi za mlubna+ na za mlozi+ na za mwaramoni ili azitumie,+ akaziambua madoa meupe kwa kumenya sehemu nyeupe-nyeupe zilizokuwa kwenye hizo fimbo.+ 38  Mwishowe zile fimbo alizokuwa amezimenya akaziweka mbele ya kundi, katika mifereji, katika vyombo vya kunyweshea wanyama,+ ambapo makundi wangekuja kunywa, ili wapate kupandana mbele yazo walipokuja kunywa. 39  Basi hayo makundi yalikuwa yakipata hamu ya kupandana mbele ya hizo fimbo, nayo makundi yalikuwa yakizaa wenye mistari-mistari, wenye mabaka na wenye madoa-doa ya rangi.+ 40  Naye Yakobo akatenganisha wale wana-kondoo dume kisha akageuza nyuso za makundi kuelekea wale wenye mistari-mistari na wote wa rangi ya kahawia kati ya makundi ya Labani. Halafu akaweka makundi yake mwenyewe peke yake wala hakuwaweka kando ya mifugo ya Labani. 41  Ikawa sikuzote kwamba wakati wowote ambao makundi yenye nguvu+ yalikuwa tayari kupandana, Yakobo alikuwa akiweka hizo fimbo katika michirizi+ mbele ya macho ya makundi, ili wapate hamu ya kupandana kando ya hizo fimbo. 42  Lakini makundi hayo yalipoonyesha unyonge hakuyaweka hapo. Kwa hiyo wanyonge sikuzote wakawa wa Labani, lakini wenye nguvu wakawa wa Yakobo.+ 43  Na huyo mwanamume akaendelea kuongezeka zaidi na zaidi, akawa na makundi makubwa na wajakazi na watumishi wanaume na ngamia na punda.+

Maelezo ya Chini