Kulingana na Luka 24:1-53
24 Hata hivyo, siku ya kwanza ya juma, walikuja asubui sana kwenye kaburi,* wakiwa na manukato yenye walikuwa wametayarisha.+
2 Lakini wakakuta jiwe limeviringishwa kutoka kwenye kaburi,*+
3 na wakati waliingia, hawakupata mwili wa Bwana Yesu.+
4 Wakati walikuwa wamevurugika juu ya jambo hilo, angalia! wanaume wawili wenye kuvaa nguo zenye kungaa wakasimama pembeni yao.
5 Wanamuke hao wakaogopa sana na wakainamisha nyuso zao kuelekea chini; basi wale wanaume wakawaambia: “Sababu gani munatafuta mutu mwenye kuishi kati ya wafu?+
6 Haiko hapa, amefufuliwa. Mukumbuke namna aliwaambia wakati alikuwa angali Galilaya;
7 alisema kama Mwana wa binadamu lazima atiwe katika mikono ya watu wenye zambi, auawe kwenye muti, na siku ya tatu (3) afufuliwe.”+
8 Basi wakakumbuka maneno yake,+
9 na wakarudia kutoka kwenye kaburi,* wakaenda kuelezea mambo hayo yote wale Kumi na Moja (11) na wengine wote.+
10 Walikuwa Maria Magdalene, Yoana, na Maria mama ya Yakobo. Pia, wanamuke wengine wenye walikuwa pamoja nao walikuwa wanaelezea mitume mambo hayo.
11 Hata hivyo, maneno hayo yalionekana kwao kama hayana maana, na hawakuamini wanamuke hao.
12 Lakini Petro akasimama na kukimbia mupaka kwenye kaburi,* akainama na kuchungulia ndani, akaona tu zile nguo za kitani. Kwa hiyo akaondoka, akijiuliza ni nini ilikuwa imefanyika.
13 Lakini angalia! siku ileile, wawili kati yao walikuwa wanasafiri kuenda katika kijiji chenye kuitwa Emau, kilometre kumi na moja (11)* hivi kutoka Yerusalemu,
14 na walikuwa wanaongea kati yao juu ya mambo hayo yote yenye yalikuwa yamefanyika.
15 Sasa wakati walikuwa wanaongea na kuzungumuzia mambo hayo, Yesu mwenyewe akakaribia na kuanza kutembea pamoja nao,
16 lakini macho yao yalizuiliwa ili yasiweze kumutambua.+
17 Akawauliza: “Ni mambo gani haya yenye munazungumuzia kati yenu wakati muko munatembea?” Wakasimama, na wakaonekana wenye huzuni.
18 Mumoja wao mwenye kuitwa Kleopa akamuambia: “Je, wewe ni mugeni na unakaa peke yako Yerusalemu na kwa hiyo haujue* mambo yenye yalifanyika mule siku hizi?”
19 Akawauliza: “Mambo gani?” Wakamujibu: “Mambo yenye kuhusu Yesu Munazareti,+ mwenye alijionyesha kuwa nabii mwenye nguvu katika matendo na maneno mbele ya Mungu na watu wote;+
20 na namna wakubwa wetu wa makuhani na watawala walimutoa ili ahukumiwe kifo,+ kisha wakamupigilia misumari kwenye muti.
21 Lakini sisi tulitumaini kama mutu huyo ndiye angekomboa Israeli.+ Ndiyo, na zaidi ya hayo yote, hii ni siku ya tatu (3) tangu mambo hayo yalifanyika.
22 Tena, wanamuke fulani kati yetu walitushangaza pia, kwa sababu walienda asubui sana kwenye kaburi*+
23 na wakati walikosa mwili wake, walikuja wakisema kwamba waliona pia jambo la ajabu—malaika waliwatokea na kuwaambia kuwa Yesu iko* muzima.
24 Kisha wamoja kati ya wale wenye walikuwa pamoja na sisi walienda kwenye kaburi,*+ na wakalikuta kama vile wale wanamuke walikuwa wamesema, lakini hawakumuona.”
25 Basi akawaambia: “Ninyi wenye kukosa akili na wenye mioyo mizito kuamini mambo yote yenye manabii walisema!
26 Je, haikukuwa lazima Kristo apatwe na mambo haya+ na aingie katika utukufu wake?”+
27 Na akianza na Musa na Manabii wote,+ akawafasiria mambo yenye kumuhusu yeye mwenyewe katika Maandiko yote.
28 Mwishowe wakakaribia kijiji kwenye walikuwa wanaenda, na akafanya kama vile alitaka kuendelea na safari.
29 Lakini wakamuomba abakie, wakisema: “Kaa pamoja na sisi, kwa sababu mangaribi imekaribia na karibuni muchana utaisha.” Basi akaingia ili akae pamoja nao.
30 Na wakati alikuwa anakula* pamoja nao, akakamata mukate, akaubariki, akauvunja na akaanza kuwapatia.+
31 Basi macho yao yakafunguliwa kabisa na wakamutambua; lakini akapotea.+
32 Wakaambiana: “Je, mioyo yetu haikukuwa inawaka wakati alikuwa anazungumuza na sisi katika barabara, na wakati alikuwa anatufasiria Maandiko waziwazi?”
33 Na wakasimama saa ileile na kurudia Yerusalemu, na wakakuta wale Kumi na Moja (11) na wale wenye walikuwa wamekusanyika pamoja nao,
34 na hawa wakasema: “Kwa kweli Bwana alifufuliwa, na alimutokea Simoni!”+
35 Kisha wakawaelezea mambo yenye yalitokea katika barabara na namna walifikia kumutambua wakati alivunja mukate.+
36 Wakati walikuwa wanasema mambo hayo, Yesu mwenyewe akasimama katikati yao na kuwaambia: “Mukuwe na amani.”+
37 Lakini kwa sababu walikuwa wameshituka na walikuwa na woga, waliwazia kwamba wanaona roho.
38 Basi akawaambia: “Sababu gani munaogopa, na sababu gani mashaka yametokea katika mioyo yenu?
39 Muangalie mikono na miguu yangu, kwamba ni mimi mwenyewe; muniguse na muone, kwa maana roho haina nyama na mifupa kama vile munaona mimi niko navyo.”
40 Na wakati alikuwa anasema mambo hayo, akawaonyesha mikono na miguu yake.
41 Lakini wakati walikuwa hawajaamini kwa sababu tu ya furaha na mushangao, akawauliza: “Muko na chakula hapa?”
42 Basi wakamupatia kipande cha samaki wa kuchomwa,
43 akakikamata, na akakikula mbele ya macho yao.
44 Kisha akawaambia: “Haya ndiyo maneno yangu yenye niliwaambia wakati nilikuwa ningali pamoja na ninyi,+ kwamba mambo yote yenye yaliandikwa juu yangu katika Sheria ya Musa na katika Manabii, na Zaburi yanapaswa kutimizwa.”+
45 Basi akafungua akili zao waziwazi ili waelewe maana ya Maandiko,+
46 na akawaambia: “Haya ndiyo yameandikwa: kwamba Kristo atateseka na atafufuliwa kutoka kwa wafu siku ya tatu (3),+
47 na kwa musingi wa jina lake kutubu kwenye kuongoza kwenye musamaha wa zambi+ kungehubiriwa katika mataifa yote+—kuanzia Yerusalemu.+
48 Ninyi munapaswa kuwa mashahidi wa mambo haya.+
49 Na muangalie! nitatuma juu yenu kile Baba yangu aliahidi. Lakini, mubakie katika muji mupaka wakati mutajazwa nguvu kutoka juu.”+
50 Kisha akawaongoza mupaka Betania, na akainua mikono yake na kuwabariki.
51 Wakati alikuwa anawabariki, akatenganishwa nao na kuchukuliwa juu mbinguni.+
52 Wakainama mbele yake na wakarudia Yerusalemu wakiwa na furaha kubwa.+
53 Na kila siku walikuwa katika hekalu, wakimusifu Mungu.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “kaburi la ukumbusho.”
^ Ao “kaburi la ukumbusho.”
^ Ao “kaburi la ukumbusho.”
^ Ao “kaburi la ukumbusho.”
^ Tnn., “stadia 60.” Stadiamu moja ilikuwa sawa na metre 185 (futi 606.95). Angalia Nyongeza B14.
^ Ao pengine, “Je, wewe tu ndiye mugeni katika Yerusalemu mwenye haujue?”
^ Ao “kaburi la ukumbusho.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “kaburi la ukumbusho.”
^ Ao “wakati alikuwa anakaa kwenye meza.