Kulingana na Luka 8:1-56

  • Wanamuke wenye walimufuata Yesu (1-3)

  • Mufano wa mupandaji (4-8)

  • Sababu gani Yesu alitumia mifano (9, 10)

  • Mufano wa mupandaji unafasiriwa (11-15)

  • Taa haipaswe kufunikwa (16-18)

  • Mama na ndugu za Yesu (19-21)

  • Yesu anatuliza zoruba (22-25)

  • Yesu anatuma pepo wachafu waingie ndani ya nguruwe (26-39)

  • Binti ya Yairo; mwanamuke fulani anagusa nguo za inje za Yesu (40-56)

8  Kisha wakati kidogo, akasafiri kutoka muji mupaka muji na kijiji mupaka kijiji, akihubiri na kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu.+ Na wale Kumi na Mbili (12) walikuwa pamoja naye,  na pia wanamuke fulani wenye walikuwa wameponyeshwa roho waovu na magonjwa: Maria mwenye aliitwa Magdalene, mwenye pepo wachafu saba (7) walikuwa wametoka ndani yake;  Yoana+ bibi ya Kuza, musimamizi wa nyumba ya Herode; Suzana; na wanamuke wengine wengi wenye walikuwa wanawatumikia kwa kutumia mali zao.+  Sasa wakati watu wengi sana walikuwa wamekusanyika pamoja na wale wenye walitoka katika miji mbalimbali na kuja kwake, akasema nao kwa kutumia mufano:+  “Mupandaji alienda kupanda mbegu zake. Wakati alikuwa anapanda, mbegu fulani zilianguka pembeni ya barabara na zikakanyangwa-kanyangwa, na ndege wa mbinguni wakazikula.+  Zingine zilianguka kwenye mwamba, na kisha kuota, zikakauka kwa sababu hazikupata maji.+  Zingine zilianguka katikati ya miiba, na miiba yenye ilikomaa pamoja nazo ikazifinya.+  Lakini zingine zilianguka kwenye udongo muzuri, na kisha kuota, zikazaa matunda mara mia moja (100) zaidi.”+ Kisha kusema mambo hayo, akasema kwa sauti kubwa: “Ule mwenye kuwa na masikio ya kusikiliza, asikilize.”+  Lakini wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mufano huo.+ 10  Akawaambia: “Ninyi mumepewa uwezo wa kuelewa siri takatifu za Ufalme wa Mungu, lakini wengine ninasema nao kwa mifano,+ ili hata kama wanaona waone bure, na hata kama wanasikia, wasielewe maana.+ 11  Basi hii ndiyo maana ya mufano huo: Mbegu ni neno la Mungu.+ 12  Mbegu zenye zilianguka pembeni ya barabara ni watu wenye wamesikia, na kisha Ibilisi anakuja na kuondoa lile neno katika mioyo yao ili wasiamini na wasiokolewe.+ 13  Mbegu zenye zilianguka kwenye mwamba ni watu wenye, wakati wanasikia neno, wanalipokea kwa furaha, lakini hawana mizizi. Wanaamini kwa wakati fulani, lakini wakati wa jaribu, wanaanguka.+ 14  Na mbegu zenye zilianguka katikati ya miiba ni watu wenye wamesikia, lakini kwa kuwa wanabebwa na mahangaiko, utajiri,+ na raha za maisha haya,+ wanafinywa kabisa na hawafikie ukomavu.+ 15  Na mbegu zenye zilianguka kwenye udongo muzuri ni watu wenye, kisha kusikia neno kwa moyo muzuri na mwema,+ wanalichunga na kuzaa matunda kwa uvumilivu.+ 16  “Hakuna mutu mwenye anawasha taa na kuifunika na chombo ao kuiweka chini ya kitanda, lakini anaiweka juu ya kinara cha taa, ili wenye kuingia ndani waone mwangaza.+ 17  Kwa maana hakuna jambo lenye kufichwa lenye halitafunuliwa, na hakuna jambo lenye kufunikwa muzuri lenye halitajulikana na kuwekwa wazi.+ 18  Basi, mukuwe waangalifu juu ya namna munasikiliza, kwa maana kila mutu mwenye iko* na kitu ataongezewa,+ lakini kila mutu mwenye hana kitu, atanyanganywa hata kile chenye anawaza iko* nacho.”+ 19  Sasa mama yake na ndugu zake+ wakakuja, lakini hawakuweza kufika karibu yake kwa sababu ya watu wengi.+ 20  Basi akaambiwa: “Mama yako na ndugu zako wamesimama inje, wanataka kukuona.” 21  Akajibu na kuwaambia: “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wenye wanasikia neno la Mungu na kulitenda.”+ 22  Siku moja, Yesu na wanafunzi wake waliingia katika mashua,* na akawaambia: “Tuvuke na tuende ngambo ingine ya bahari.” Basi wakaanza safari.+ 23  Lakini wakati walikuwa katika safari, akalala usingizi. Na zoruba kali yenye upepo mukali ikatokea katika bahari, na mashua* yao ikaanza kujaa maji na kuwa katika hatari.+ 24  Basi wakaenda kumuamusha na kusema: “Mwalimu, Mwalimu, tuko karibu kufa!” Halafu akaamuka, akakemea upepo na muchafuko wa maji, na hivyo vikatulia, na kukakuwa utulivu.+ 25  Kisha akawaambia: “Imani yenu iko wapi?” Lakini walikuwa wameogopa sana, wakashangaa, na kuambiana: “Kwa kweli huyu ni nani? Kwa maana anaamuru hata upepo na maji, na vinamutii.”+ 26  Wakafika kwenye inchi kavu katika eneo la Wagerasene,+ lenye kuangaliana na Galilaya. 27  Wakati Yesu alishuka kuenda kwenye inchi kavu, akakutana na mutu fulani wa muji huo; mutu huyo alikuwa na pepo wachafu. Alikuwa amefanya wakati murefu bila kuvaa nguo, na hakukuwa anakaa katika nyumba, lakini katikati ya makaburi.*+ 28  Wakati alimuona Yesu, akalia kwa sauti kubwa na kuanguka chini mbele yake, na kusema kwa sauti kubwa: “Niko na shida gani na wewe, Yesu, Mwana wa Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi? Ninakuomba, usinitese.”+ 29  (Kwa ­maana Yesu ­alikuwa amemuamuru ule roho muchafu atoke ndani ya ule mutu. Ule roho alikuwa amemushika mara nyingi,*+ na alifungwa mara kwa mara kwa minyororo na pingu na kuwekwa chini ya ulinzi, lakini alikuwa anavunja vifungo hivyo na ule pepo muchafu alikuwa anamupeleka mahali kwenye hakuna watu.) 30  Yesu akamuuliza: “Jina lako nani?” Akajibu: “Lejioni,”* kwa maana pepo wachafu wengi walikuwa wamemuingia. 31  Na wakaendelea kumulilia asiwaamuru waende katika abiso.+ 32  Sasa kundi kubwa la nguruwe+ lilikuwa linakula kwenye mulima, basi wale pepo wachafu wakamuomba awaruhusu waingie ndani ya wale nguruwe, na akawaruhusu.+ 33  Basi wale pepo wachafu wakatoka ndani ya mutu huyo na kuingia ndani ya wale nguruwe, na lile kundi la nguruwe likakimbia, likaruka kwenye poromoko,* likaingia katika bahari na kufa katika maji. 34  Lakini wakati wachungaji waliona jambo lenye lilitokea, wakakimbia na kupeleka habari katika muji na kwenye eneo la mashamba. 35  Kisha watu wakaondoka ili kuona kile kilikuwa kimetokea. Wakakuja kwenye Yesu alikuwa na wakamukuta ule mutu mwenye alitokwa na pepo wachafu. Alikuwa amevaa nguo na akili yake ilikuwa sawa, alikuwa amekaa kwenye miguu ya Yesu, na wakaogopa. 36  Wale wenye walikuwa wameona jambo hilo wakawaelezea namna ule mutu mwenye alikuwa na pepo wachafu aliponyeshwa. 37  Kisha watu wengi kutoka katika eneo la pembeni-pembeni la Wagerasene wakamuomba Yesu aondoke kwao, kwa sababu walikuwa wameogopa sana. Basi akapanda katika mashua* ili aondoke. 38  Hata hivyo, ule mutu mwenye alikuwa ametokwa na pepo wachafu akaendelea kumuomba abakie pamoja naye, lakini Yesu hakumuruhusu, akamuambia:+ 39  “Rudia kwako, na uendelee kueleza mambo yenye Mungu amekutendea.” Basi akaenda, akitangaza katika muji wote mambo yenye Yesu alimutendea. 40  Wakati Yesu alirudia, watu wengi wakamupokea kwa fazili, kwa maana wote walikuwa wanamungojea.+ 41  Lakini angalia! mwanaume mwenye kuitwa Yairo akakuja; alikuwa ofisa-musimamizi wa sinagogi. Akaanguka kwenye miguu ya Yesu na kuanza kumulilia aende kwenye nyumba yake,+ 42  kwa sababu binti yake wa pekee,* mwenye miaka karibu kumi na mbili (12), alikuwa karibu kufa. Wakati Yesu alikuwa anaenda, watu wengi walimusonga sana. 43  Sasa kulikuwa mwanamuke mumoja mwenye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu+ kwa miaka kumi na mbili (12), na hakupata mutu hata mumoja mwenye aliweza kumuponyesha.+ 44  Akakaribia kutokea nyuma na kugusa sehemu ya chini ya nguo yake ya inje,+ na mara moja damu ikaacha kumutoka. 45  Basi Yesu akauliza: “Ni nani amenigusa?” Wakati wote walikuwa wanakana, Petro akasema: “Mwalimu, watu wengi wanakuzunguka na kukusonga sana.”+ 46  Lakini Yesu akasema: “Mutu fulani amenigusa, kwa maana ninajua nguvu+ zimenitoka.” 47  Wakati aliona kama jambo lenye alifanya lilijulikana, ule mwanamuke akakuja akitetemeka na kuanguka mbele yake, na kusema mbele ya watu wote sababu gani alimugusa na namna aliponyeshwa mara moja. 48  Lakini Yesu akamuambia: “Binti yangu, imani yako imekuponyesha. Uende kwa amani.”+ 49  Wakati alikuwa angali anasema, mujumbe mumoja wa ofisa-musimamizi wa Sinagogi akakuja, akasema: “Binti yako amekufa; usiendelee kumusumbua Mwalimu.”+ 50  Wakati Yesu alisikia jambo hilo, akamuambia Yairo: “Usiogope, ukuwe tu na imani, na ataokolewa.”+ 51  Wakati alifika kwenye nyumba hiyo, hakuruhusu mutu yeyote aingie pamoja naye isipokuwa Petro, Yohana, Yakobo, na baba na mama ya ule mutoto mwanamuke. 52  Lakini watu wote walikuwa wanalia na kujipiga-piga kwa huzuni kwa ajili ya ule mutoto mwanamuke. Basi akawaambia: “Muache kulia,+ kwa maana hakukufa lakini analala usingizi.”+ 53  Halafu wakaanza kumucheka kwa zarau, kwa sababu walijua amekufa. 54  Lakini akamukamata mukono na kumuita: “Mutoto, amuka!”+ 55  Na roho+ yake* ikarudia, na akasimama mara moja,+ na Yesu akaamuru apewe chakula. 56  Basi, wazazi wake wakafurahi sana, lakini Yesu akawaamuru wasimuambie mutu yeyote jambo lenye lilitendeka.+

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “makaburi ya ukumbusho.”
Ao pengine, “Alikuwa amemushika kwa muda murefu.”
Katika jeshi la Roma, lejioni ilikuwa kikundi kikubwa cha maaskari karibu 4000 mupaka 6000.
Ni kusema, sehemu ya pembeni ya bahari yenye muteremuko mukali.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Tnn., “muzaliwa-pekee.”
Ao “nguvu yake ya uzima.”