Kulingana na Luka 17:1-37

  • Kukwazika, musamaha, na imani (1-6)

  • Watumwa wenye hawana mafaa yoyote (7-10)

  • Watu kumi wenye ukoma wanaponyeshwa (11-19)

  • Kuja kwa Ufalme wa Mungu (20-37)

    • “Ufalme wa Mungu uko katikati yenu.” (21)

    • “Mukumbuke bibi ya Loti” (32)

17  Kisha akaambia wanafunzi wake: “Lazima mambo yenye kuleta vikwazo yakuje. Lakini, ole wake mutu mwenye yatakuja kupitia yeye!  Ingekuwa muzuri zaidi kwake kama jiwe la kusagia lingefungiwa kwenye shingo yake na atupwe katika bahari, kuliko yeye amukwaze mumoja wa hawa wadogo.+  Mujiangalie ninyi wenyewe. Kama ndugu yako anatenda zambi, umukemee,+ na kama anatubu, umusamehe.+  Hata kama anakutendea zambi mara saba (7) kwa siku, na anarudia kwako mara saba, akisema, ‘Ninatubu,’ unapaswa kumusamehe.”+  Sasa mitume wakamuambia Bwana: “Utupatie imani zaidi.”+  Kisha Bwana akasema: “Kama mungekuwa na imani yenye ukubwa wa mbegu ya haradali, mungeambia muti huu wa muforsadi mweusi, ‘Ongoka na upandwe katika bahari!’ na ungewatii.+  “Ni nani kati yenu mwenye kama iko* na mutumwa mwenye kulima ao mwenye kuchunga wanyama, anaweza kumuambia wakati anarudia kutoka katika shamba, ‘Kuja hapa mara moja na ukule kwenye meza’?  Lakini, je, hatamuambia, ‘Nitayarishie chakula changu cha mangaribi, na uvae aproni* na unitumikie mupaka nimalize kula na kunywa, na kisha unaweza kula na kunywa’?  Hatashukuru mutumwa huyo kwa sababu alifanya mambo yenye aliombwa afanye, haiko vile? 10  Vilevile, wakati mumefanya mambo yote yenye muliombwa kufanya, museme: ‘Sisi ni watumwa wenye hawana mafaa yoyote. Mambo yenye tumefanya ni yale tulipaswa kufanya.’”+ 11  Wakati alikuwa anaenda Yerusalemu, alikuwa anapita kati ya Samaria na Galilaya. 12  Na wakati alikuwa anaingia katika kijiji fulani, alikutana na wanaume kumi (10) wenye ukoma, lakini wakasimama mbali naye.+ 13  Na wakasema kwa sauti kubwa: “Yesu, Mwalimu, utusikilie huruma!” 14  Wakati aliwaona, akawaambia: “Muende mujionyeshe kwa makuhani.”+ Basi wakati walikuwa wanaenda, wakatakaswa.+ 15  Mumoja wao, wakati aliona kuwa amepona, akarudia akimutukuza Mungu kwa sauti kubwa. 16  Akapiga magoti kwenye miguu ya Yesu na kuinama mupaka chini, akimushukuru. Na tena, alikuwa Musamaria.+ 17  Yesu akasema: “Wote kumi (10) walitakaswa, haiko vile? Basi, wale wengine kenda (9) wako wapi? 18  Je, hakuna mwingine mwenye alirudia ili kumutukuza Mungu isipokuwa mutu huyu wa taifa lingine?” 19  Kisha akamuambia: “Simama uende; imani yako imekuponyesha.”+ 20  Wakati Wafarisayo walimuuliza Ufalme wa Mungu utakuja wakati gani,+ aliwajibu: “Ufalme wa Mungu hautakuja kwa njia yenye kuonekana na watu wote; 21  na watu hawatasema, ‘Muangalie hapa!’ ao, ‘Pale!’ Kwa maana muangalie! Ufalme wa Mungu uko katikati yenu.”+ 22  Kisha akaambia wanafunzi wake: “Siku zitakuja wakati mutatamani kuona moja ya siku za Mwana wa binadamu, lakini hamutaiona. 23  Na watu watawaambia ninyi, ‘Muangalie pale!’ ao, ‘Muangalie hapa!’ Musiende wala musiwafuate.+ 24  Kwa maana kama vile umeme wa radi unawaka kutoka upande mumoja wa mbingu mupaka upande mwingine wa mbingu, ni vile Mwana wa binadamu+ atakuwa katika siku yake.+ 25  Lakini, lazima kwanza apatwe na mateso mengi na kukataliwa na kizazi hiki.+ 26  Zaidi ya hayo, kama vile ilikuwa katika siku za Noa,+ ni vile itakuwa katika siku za Mwana wa binadamu:+ 27  walikuwa wanakula, walikuwa wanakunywa, wanaume walikuwa wanaoa, wanamuke walikuwa wanaolewa mupaka ile siku Noa aliingia ndani ya safina,+ na Garika ikakuja na kuwaharibu wote.+ 28  Pia, kama vile ilikuwa katika siku za Loti:+ walikuwa wanakula, walikuwa wanakunywa, walikuwa wananunua, walikuwa wanauzisha, walikuwa wanapanda, walikuwa wanajenga. 29  Lakini ile siku yenye Loti alitoka Sodoma, kulinyesha mvua ya moto na kiberiti kutoka mbinguni na kuwaharibu wote.+ 30  Itakuwa vilevile ile siku yenye Mwana wa binadamu atafunuliwa.+ 31  “Siku hiyo mutu mwenye kuwa kwenye sehemu ya juu ya nyumba lakini vitu vyake viko katika nyumba asishuke kuvikamata, vilevile mutu mwenye kuwa katika shamba asirudilie vitu vyenye kuwa nyuma. 32  Mukumbuke bibi ya Loti.+ 33  Kila mutu mwenye anatafuta kulinda uzima wake ataupoteza,* lakini kila mutu mwenye anaupoteza atauokoa.+ 34  Ninawaambia ninyi, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mumoja atachukuliwa, lakini mwingine ataachwa.+ 35  Wanamuke wawili watakuwa wakisaga kwenye jiwe moja; mumoja atachukuliwa, lakini mwingine ataachwa.” 36  *​—hs-1​— 37  Basi wakamuuliza: “Wapi, Bwana?” Akawajibu: “Mahali kwenye kuwa maiti, tai pia watakusanyika pale pamoja.”+

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “tablier.”
Ao “nafsi yake ataipoteza.”