Kulingana na Luka 7:1-50
7 Wakati alimaliza kuambia watu mambo hayo, akaingia Kapernaumu.
2 Sasa ofisa mumoja wa jeshi alikuwa na mutumwa mwenye alikuwa anapenda sana, na sasa mutumwa huyo alikuwa mugonjwa sana, karibu kufa.+
3 Wakati alisikia habari juu ya Yesu, akatuma kwake wazee fulani wa Wayahudi wamuombe akuje kumuponyesha mutumwa wake.
4 Wakakuja kwa Yesu na kuanza kumulilia sana, na kusema: “Anastahili umutendee jambo hili,
5 kwa maana anapenda taifa letu na yeye mwenyewe alijenga sinagogi letu.”
6 Basi Yesu akaenda pamoja nao. Lakini wakati alikuwa karibu na nyumba, ule ofisa wa jeshi alikuwa ametuma marafiki wake wamuambie: “Bwana, usijisumbue, kwa maana mimi sistahili kukupokea katika nyumba yangu.+
7 Ndiyo sababu nilijiona sistahili kuja kwako. Lakini sema neno moja tu, na mutumishi wangu atapona.
8 Kwa maana mimi pia niko chini ya mamlaka, na niko na maaskari wenye kuwa chini yangu, na ninaambia huyu, ‘Uende!’ na anaenda, na mwingine, ‘Kuja!’ na anakuja, na mutumwa wangu, ‘Fanya jambo hili!’ na analifanya.”
9 Wakati Yesu alisikia maneno hayo akashangazwa naye, akageuka na kuangalia watu wengi wenye walikuwa wanamufuata, na akasema: “Ninawaambia ninyi, hata katika Israeli sijaona imani kubwa kama hii.”+
10 Na wakati wale wenye walikuwa wametumwa walirudia kwao, wakamukuta ule mutumwa amepona.+
11 Kisha wakati kidogo, akasafiri na kuenda kwenye muji mumoja wenye kuitwa Naini, na wanafunzi wake pamoja na watu wengi sana walikuwa wanasafiri pamoja naye.
12 Wakati alikaribia mulango mukubwa wa muji, angalia! kulikuwa mufu mwenye alikuwa anapelekwa inje, alikuwa mwana mumoja tu* wa mama yake.+ Zaidi ya hayo, mama huyo alikuwa mujane. Watu wengi sana kutoka katika muji huo walikuwa pamoja na ule mwanamuke.
13 Wakati Bwana alimuona, akamusikilia huruma,+ na akamuambia: “Acha kulia.”+
14 Akakaribia na kugusa kitanda cha kubebea maiti, na wale wenye walikuwa wanakibeba wakasimama. Kisha akasema: “Kijana, ninakuambia, amuka!”+
15 Ule mufu akakaa na akaanza kusema, na Yesu akamupatia mama yake.+
16 Basi wote wakaogopa, na wakaanza kumutukuza Mungu na kusema: “Nabii mukubwa ameinuliwa katikati yetu,”+ na, “Mungu amekumbuka watu wake.”+
17 Na habari hii juu yake ikaenea katika Yudea yote na inchi yote ya pembeni-pembeni.
18 Sasa wanafunzi wa Yohana wakamujulisha mambo hayo yote.+
19 Basi Yohana akaita wawili kati ya wanafunzi wake na akawatuma kwa Bwana wamuulize: “Wewe ndiye Ule Mwenye Anakuja,+ ao tungojee mwingine?”
20 Wakati walifika kwenye alikuwa, wanaume hao wakasema: “Yohana Mubatizaji alitutuma kwako tukuulize: ‘Wewe ndiye Ule Mwenye Anakuja ao tungojee mwingine?’”
21 Saa hiyo akaponyesha watu wengi magonjwa,+ maumivu makali, akafukuza roho waovu, na kupatia vipofu wengi zawadi ya kuona.
22 Akajibu na kuwaambia: “Muende na mumuelezee Yohana mambo yenye mumeona na kusikia: Sasa vipofu wanaona,+ vilema wanatembea, wenye ukoma wanafanywa kuwa safi, viziwi wanasikia,+ wafu wanafufuliwa, na maskini wanatangaziwa habari njema.+
23 Mwenye furaha ni mutu mwenye hapate ndani yangu sababu yoyote ya kukwazika.”+
24 Wakati wajumbe wa Yohana waliondoka, Yesu akaanza kuambia watu wengi habari juu ya Yohana: “Mulienda kuona nini katika jangwa? Utete wenye kutikiswa na upepo?+
25 Basi, mulienda kuona nini? Mutu mwenye kuvaa nguo za muzuri?+ Kwa sababu wale wenye kuvaa nguo za muzuri na kuishi maisha ya raha wako katika nyumba za kifalme.
26 Basi, kwa kweli mulienda kuona nini? Nabii? Ndiyo, ninawaambia ninyi, ni mutu mukubwa zaidi kupita nabii.+
27 Huyu ndiye imeandikwa hivi kumuhusu, ‘Angalia! ninamutuma mujumbe wangu mbele yako,* mwenye atatayarisha njia yako mbele yako.’+
28 Ninawaambia ninyi, kati ya wale wenye walizaliwa na wanamuke, hakuna mwenye kuwa mukubwa kuliko Yohana, lakini mutu mwenye kuwa mudogo zaidi katika Ufalme wa Mungu, ni mukubwa kuliko yeye.”+
29 (Wakati watu wote na wakusanya-kodi walisikia jambo hilo, wakamutangaza Mungu kuwa mwenye haki, kwa sababu walikuwa wamebatizwa ubatizo wa Yohana.+
30 Lakini Wafarisayo na wale wenye kujua sana Sheria walipuuza shauri lenye* Mungu aliwapatia,+ kwa kuwa hawakubatizwa na Yohana.)
31 “Basi, nitalinganisha watu wa kizazi hiki na nani, na wanafanana na nani?+
32 Wanafanana na watoto wadogo wenye kukaa katika soko wakiitana, na kusema: ‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamukucheza; tuliomboleza, lakini hamukulia.’
33 Vilevile, wakati Yohana Mubatizaji alikuja hakukuwa anakula mukate na hakukuwa anakunywa divai,+ lakini munasema: ‘Iko* na pepo muchafu.’
34 Wakati Mwana wa binadamu alikuja alikuwa anakula na kunywa, lakini munasema: ‘Angalia! Mutu mulafi na mwenye anazoea kunywa divai, rafiki ya wakusanya-kodi na watenda-zambi!’+
35 Hata hivyo, hekima inaonekana kuwa yenye haki* kupitia watoto wake wote.”*+
36 Sasa, mumoja wa Wafarisayo aliendelea kumuomba amutembelee ili kula chakula pamoja naye. Basi akaingia katika nyumba ya Mufarisayo huyo na akakaa kwenye meza.
37 Na angalia! mwanamuke mwenye alijulikana katika muji kuwa mutenda-zambi akapata habari kwamba alikuwa anakula* katika nyumba ya Mufarisayo, na akaleta chupa ya alabasta yenye kuwa na mafuta yenye marashi.+
38 Akakaa nyuma, kwenye miguu ya Yesu, akalia na kuanza kulowanisha miguu ya Yesu kwa machozi yake na kuipanguza kwa nywele za kichwa chake. Pia, akabusu miguu ya Yesu kwa upole wote* na kuimwangia yale mafuta yenye marashi.
39 Wakati ule Mufarisayo mwenye alimualika Yesu aliona jambo hilo, akasema katika moyo wake: “Kwa kweli mutu huyu angekuwa kabisa nabii, angejua mwanamuke huyu mwenye anamugusa ni nani na ni wa namna gani, kwamba ni mutenda-zambi.”+
40 Lakini Yesu akamujibu: “Simoni, niko na jambo fulani la kukuambia.” Akasema: “Sema, Mwalimu!”
41 “Watu wawili walikuwa na deni la mukopeshaji fulani; mumoja alikuwa na deni la dinari* mia tano (500), lakini mwingine la makumi tano (50).
42 Wakati walikosa kitu cha kumulipa, akawasamehe wote wawili kwa kupenda. Kwa hiyo, ni nani kati yao mwenye atamupenda zaidi?”
43 Simoni akajibu: “Ninafikiri ni ule mwenye alisamehewa deni kubwa zaidi.” Akamuambia: “Umejibu muzuri.”
44 Halafu akageuka na kumuangalia ule mwanamuke na kumuambia Simoni: “Unaona mwanamuke huyu? Niliingia katika nyumba yako; haukunipatia maji ya kunawa miguu. Lakini mwanamuke huyu alilowanisha miguu yangu kwa machozi yake na kuipanguza kwa nywele zake.
45 Haukunibusu, lakini tangu saa niliingia, mwanamuke huyu, hajaacha kubusu miguu yangu kwa upole wote.*
46 Haukumwanga mafuta kwenye kichwa changu, lakini mwanamuke huyu amemwanga mafuta yenye marashi kwenye miguu yangu.
47 Kwa sababu hiyo, ninakuambia, zambi zake, hata kama ni nyingi,* zimesamehewa,+ kwa sababu alipenda sana. Lakini mwenye anasamehewa kidogo, anapenda kidogo.”
48 Kisha akamuambia ule mwanamuke: “Zambi zako zimesamehewa.”+
49 Wale wenye walikuwa wanakaa kwenye meza pamoja naye wakaanza kusema kati yao: “Mutu huyu ni nani mwenye hata anasamehe zambi?”+
50 Lakini akamuambia ule mwanamuke: “Imani yako imekuokoa;+ uende kwa amani.”
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “mwana muzaliwa-pekee.”
^ Tnn., “mbele ya uso wako.”
^ Ao “muongozo wenye.”
^ Ao “Eko.”
^ Ao “inatetewa.”
^ Ao “kupitia matokeo yake.”
^ Ao “alikuwa amekaa kwenye meza.”
^ Ao “wororo.”
^ Angalia Nyongeza B14.
^ Ao “wororo.”
^ Ao “kubwa.”