Kulingana na Luka 14:1-35

  • Mutu mwenye ugonjwa wa kuvimbisha mwili anaponyeshwa siku ya Sabato (1-6)

  • Ukuwe mugeni munyenyekevu (7-11)

  • Ualike wale wenye hawawezi kukulipa (12-14)

  • Mufano wa waalikwa wenye walitoa visingizio (15-24)

  • Garama ya kuwa mwanafunzi (25-33)

  • Chumvi yenye inapoteza nguvu yake (34, 35)

14  Wakati mwingine alienda kula chakula katika nyumba ya kiongozi mumoja wa Wafarisayo, katika siku ya Sabato, na walikuwa wanamuangalia sana.  Na angalia! mbele yake kulikuwa mutu fulani mwenye alikuwa na ugonjwa wenye kuvimbisha mwili.  Basi Yesu akauliza wale wenye kujua sana Sheria, na Wafarisayo: “Je, inaruhusiwa kuponyesha siku ya Sabato ao hapana?”+  Lakini wakabakia kimya. Basi akakamata mutu huyo, akamuponyesha, na akamuacha aende.  Kisha akawauliza: “Ni nani kati yenu, kama mwana wake ao ngombe-dume wake anaanguka ndani ya kisima+ siku ya Sabato hatamutosha mara moja ndani ya kisima hicho?”+  Na hawakuweza kumujibu.  Kisha akawaambia mufano wale wenye walialikwa wakati aliona namna walikuwa wanajichagulia nafasi za heshima zaidi.+ Akawaambia:  “Wakati mutu anakualika kwenye karamu ya ndoa, usikae nafasi ya heshima zaidi.+ Pengine amealika pia mutu wa heshima zaidi kuliko wewe.  Na ule mwenye aliwaalika ninyi wawili atakuja na kukuambia, ‘Achia mutu huyu nafasi yako.’ Kisha utaondoka na haya na kukaa nafasi ya chini zaidi. 10  Lakini wakati unaalikwa, uende na kukaa nafasi ya chini zaidi, ili wakati mutu mwenye alikualika atakuja, akuambie, ‘Rafiki, uende ukae nafasi ya heshima zaidi.’ Kisha utakuwa na heshima mbele ya wageni wenzako wote.+ 11  Kwa maana kila mutu mwenye kujiinua atanyenyekezwa, na kila mutu mwenye kujinyenyekeza atainuliwa.”+ 12  Kisha akamuambia pia ule mutu mwenye alimualika: “Wakati unatayarisha chakula cha muchana ao cha mangaribi, usiite marafiki wako, ao ndugu zako, ao watu wa jamaa yako, ao majirani wako wenye ni matajiri. Ukifanya vile, wao pia wanaweza kukualika, na hiyo ingekuwa malipo yako. 13  Lakini wakati unatayarisha karamu, ualike maskini, viwete, vilema, na vipofu;+ 14  na utakuwa mwenye furaha, kwa sababu hawana kitu cha kukulipa. Kwa maana utalipwa katika ufufuo+ wa wenye haki.” 15  Wakati mumoja wa wageni wenzake alisikia mambo hayo, akamuambia: “Mwenye furaha ni ule mwenye anakula* katika Ufalme wa Mungu.” 16  Yesu akamuambia: “Mutu fulani alikuwa anatayarisha chakula kikubwa cha mangaribi,+ na akaalika watu wengi. 17  Wakati saa ya kula chakula cha mangaribi ilifika, akatuma mutumwa wake inje ili aambie wenye walialikwa, ‘Mukuje, kwa sababu sasa kila kitu kiko tayari.’ 18  Lakini wote kwa namna moja wakaanza kutoa visingizio.+ Wa kwanza akasema, ‘Nilinunua shamba, na inaomba niende kuliona; ninakuomba unisamehe.’ 19  Na mwingine akasema, ‘Nimenunua ngombe kumi (10), na ninaenda kuwachunguza; ninaomba unisamehe.’+ 20  Mwingine pia akasema, ‘Nimeoa sasa hivi, kwa hiyo siwezi kuja.’ 21  Basi ule mutumwa akakuja na kumuambia bwana wake mambo hayo. Kisha ule bwana wa nyumba akakasirika na kuambia mutumwa wake, ‘Uende haraka kwenye njia kubwa na kwenye njia za kidogo-kidogo za muji, na ulete hapa maskini, viwete, vipofu, na vilema.’ 22  Kisha wakati fulani ule mutumwa akasema, ‘Bwana, mambo yenye uliagiza yamefanywa, na kungali nafasi.’ 23  Basi ule bwana akamuambia, ‘Uende inje kwenye barabara na kwenye njia za kidogo na ulazimishe watu wakuje, ili nyumba yangu ijae.+ 24  Kwa maana ninawaambia ninyi, hakuna hata mumoja wa watu wenye walikuwa wamealikwa mwenye ataonja chakula changu cha mangaribi.’”+ 25  Sasa watu wengi sana walikuwa wanasafiri pamoja naye, na akageuka na kuwaambia: 26  “Kama mutu yeyote anakuja kwangu na hamuchukie* baba yake, mama yake, bibi yake, watoto wake, ndugu na dada zake, ndiyo, hata uzima wake* mwenyewe,+ hawezi kuwa mwanafunzi wangu.+ 27  Kila mutu mwenye habebe muti wake wa mateso* na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.+ 28  Kwa mufano, ni nani kati yenu mwenye akitaka kujenga munara hakae kwanza na kuhesabia garama, ili aone kama iko* na vitu vya kutosha ili kuumaliza? 29  Kama hafanye vile, anaweza kuweka musingi lakini anashindwa kumaliza munara, na wale wenye kumuangalia wataanza kumuchekelea, 30  na kusema: ‘Mutu huyu alianza kujenga lakini hakuweza kumaliza.’ 31  Ao ni mufalme gani mwenye kuwa na maaskari elfu kumi (10000) mwenye anaenda kukutana katika vita na mufalme mwingine, ambaye hakae kwanza na kufanya shauri aone kama ataweza kumushinda ule mwenye anakuja kupigana naye akiwa na maaskari elfu makumi mbili (20000)? 32  Ikiwa kwa kweli hawezi kumushinda, basi wakati ule mufalme mwingine angali mbali, yeye anatuma baraza la mabalozi* na kuomba amani. 33  Vilevile, mukuwe hakika kwamba, hakuna hata mumoja wenu mwenye anaweza kuwa mwanafunzi wangu kama haachane na* vitu vyake vyote.+ 34  “Kwa kweli chumvi ni ya muzuri. Lakini chumvi ikipoteza nguvu yake, itakolezwa na nini?+ 35  Haifae kwa ajili ya udongo ao kwa ajili ya mbolea. Watu wanaitupa. Ule mwenye kuwa na masikio ya kusikiliza, asikilize.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “mwenye anakula mukate.”
Ao “hamupendi kwa kiasi kidogo.”
Ao “nafsi yake.”
Ao “eko.”
Ao “ambassadeurs.”
Tnn., “haseme kwa heri kwa.”