Kulingana na Matayo 8:1-34

  • Mutu mwenye ukoma anaponyeshwa (1-4)

  • Imani ya ofisa mumoja wa jeshi (5-13)

  • Yesu anaponyesha watu wengi Kapernaumu (14-17)

  • Namna ya kumufuata Yesu (18-22)

  • Yesu anatuliza zoruba (23-27)

  • Yesu anatuma pepo wachafu katika nguruwe (28-34)

8  Wakati alishuka kutoka kwenye mulima, watu wengi sana wakamufuata.  Na angalia! mutu fulani mwenye ukoma akakuja, akainama mbele yake, na kusema: “Bwana, kama tu unataka, unaweza kunifanya kuwa safi.”+  Basi, akanyoosha mukono wake, akamugusa, na kusema: “Ninataka! Kuwa safi.”+ Mara moja akakuwa safi na ukoma wake ukaisha.+  Kisha Yesu akamuambia: “Fanya angalisho, usiambie mutu yeyote,+ lakini uende, ujionyeshe kwa kuhani,+ na utoe zawadi yenye Musa aliagiza,+ ili ikuwe ushahidi kwao.”  Wakati aliingia Kapernaumu, ofisa mumoja wa jeshi alikuja kwake, akimulilia+  na kusema: “Bwana, mutumishi wangu analala katika nyumba, iko* na ugonjwa wa kupooza na anateseka sana.”  Akamuambia: “Wakati nitafika kule, nitamuponyesha.”  Ofisa huyo wa jeshi akamujibu: “Bwana, mimi sistahili kukupokea katika nyumba yangu, lakini sema neno moja tu na mutumishi wangu atapona.  Kwa maana mimi pia niko chini ya mamlaka, na niko na maaskari wenye kuwa chini yangu, na ninamuambia huyu, ‘Uende!’ na anaenda, na mwingine, ‘Kuja!’ na anakuja, na mutumwa wangu, ‘Fanya jambo hili!’ na analifanya.” 10  Wakati Yesu alisikia maneno hayo, akashangaa na kuambia wale wenye walikuwa wanamufuata: “Ninawaambia ninyi kweli, katika Israeli sijaona mutu mwenye imani kubwa kama hii.+ 11  Lakini ninawaambia kwamba watu wengi kutoka mashariki na mangaribi watakuja na kukaa kwenye meza pamoja na Abrahamu, Isaka, na Yakobo katika Ufalme wa mbinguni;+ 12  hata hivyo wana wa Ufalme watatupwa inje katika giza. Ni kule watalia na kusaga meno yao.”+ 13  Kisha Yesu akamuambia ule ofisa wa jeshi: “Uende. Na ifanyike kwako kulingana na imani yako.”+ Na ule mutumishi akapona saa ileile.+ 14  Na wakati Yesu aliingia katika nyumba ya Petro, aliona mama-mukwe wa Petro+ amelala na alikuwa na ugonjwa wa homa.+ 15  Basi akagusa mukono wake,+ na homa hiyo ikamutoka, akasimama na kuanza kumutumikia. 16  Lakini wakati ilikuwa mangaribi, watu walimuletea watu wengi wenye walikuwa na pepo wachafu; akafukuza hao roho kwa kusema neno moja, na akaponyesha wote wenye walikuwa wagonjwa, 17  ili kutimiza maneno yenye yalisemwa kupitia nabii Isaya: “Yeye mwenyewe alichukua magonjwa yetu na kubeba maumivu yetu.”+ 18  Wakati Yesu aliona watu wengi wanamuzunguka, akaamuru wanafunzi wavuke na kuenda ngambo ingine ya bahari.+ 19  Na mwandishi fulani akakuja na kumuambia: “Mwalimu, nitakufuata kila mahali utaenda.”+ 20  Lakini Yesu akamuambia: “Mbweha wako na mashimo na ndege wa mbinguni wako na chicha,* lakini Mwana wa binadamu hana mahali pa kulalisha kichwa chake.”+ 21  Kisha mwingine kati ya wanafunzi akamuambia: “Bwana, uniruhusu kwanza niende nimuzike baba yangu.”+ 22  Yesu akamuambia: “Endelea kunifuata, na uache wafu wazike wafu wao.”+ 23  Na wakati alipanda katika mashua,* wanafunzi wake wakamufuata.+ 24  Sasa angalia! upepo mukali ukatokea katika bahari, mupaka mawimbi yalikuwa yanafunika mashua;* lakini Yesu alikuwa amelala usingizi.+ 25  Wakakuja, wakamuamusha, na kusema: “Bwana, utuokoe, tuko karibu kufa!” 26  Lakini akawaambia: “Sababu gani munaogopa sana,* ninyi wenye imani kidogo?”+ Kisha akasimama na kukemea upepo na bahari, na kukakuwa utulivu mukubwa.+ 27  Basi wanafunzi wakashangaa na kusema: “Huyu ni mutu wa namna gani? Hata upepo na bahari vinamutii.” 28  Wakati alifika upande mwingine katika inchi ya Wagadarene, wanaume wawili wenye walikuwa na pepo wachafu wakatoka katikati ya makaburi* na kukutana naye.+ Walikuwa wakali sana, kwa hiyo watu wote waliogopa kupita katika barabara hiyo. 29  Na angalia! wakasema kwa sauti kubwa: “Tuko na shida gani na wewe, Mwana wa Mungu?+ Je, umekuja hapa kututesa+ mbele ya wakati wenye Mungu aliweka?”+ 30  Lakini kule mbali nao kulikuwa kundi la nguruwe wengi wenye walikuwa wanakula.+ 31  Basi wale pepo wachafu wakaanza kumuomba, na kusema: “Ukitufukuza, ututume katika lile kundi la nguruwe.”+ 32  Na akawaambia: “Muende!” Halafu wakatoka na kuingia ndani ya wale nguruwe, na angalia! nguruwe wote wakakimbia, wakaruka kwenye poromoko,* likaingia katika bahari na kufa katika maji. 33  Lakini wachungaji wakakimbia na kuingia katika muji, wakaeleza kila kitu, kutia ndani habari ya wale watu wenye walikuwa na pepo wachafu. 34  Na angalia! watu wote katika muji wakaenda kukutana na Yesu, na wakati walimuona, wakamuomba sana atoke katika eneo lao.+

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “nyumba; viota.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “muko na moyo wa woga.”
Ao “makaburi ya ukumbusho.”
Ni kusema, sehemu ya pembeni ya bahari yenye muteremuko mukali.