Kulingana na Matayo 21:1-46

  • esu anaingia kwa ushindi (1-11)

  • Yesu anasafisha hekalu (12-17)

  • Muti wa tini unalaaniwa (18-22)

  • Mamlaka ya Yesu yanatiliwa mashaka (23-27)

  • Mufano wa wana wawili (28-32)

  • Mufano wa walimaji wauaji (33-46)

    • Jiwe kubwa la pembe linakataliwa (42)

21  Wakati walikaribia Yerusalemu, wakafika Betfage kwenye Mulima wa Mizeituni, basi Yesu akatuma wanafunzi wawili,+  akawaambia: “Muende katika kijiji chenye munaona mbele yenu, na mara moja mutakuta punda amefungwa, na mwana-punda pamoja naye. Muwafungue na kuniletea.  Mutu fulani akiwaambia jambo lolote, munapaswa kumuambia, ‘Bwana iko* na lazima yao.’ Mara moja ataacha ule punda na mwana-punda.”  Kwa kweli jambo hilo lilitokea ili kutimiza neno lenye lilisemwa kupitia nabii, wakati alisema:  “Mumuambie binti ya Sayuni, ‘Angalia! Mufalme wako anakuja kwako,+ yeye ni mwenye tabia ya upole+ na amepanda juu ya punda, ndiyo, juu ya mwana-punda, uzao wa munyama wa kubeba mizigo.’”+  Kwa hiyo wale wanafunzi wakaenda na kufanya kama vile Yesu alikuwa amewaagiza.+  Wakaleta huyo punda na mwana-punda wake, kisha wakaweka juu yao nguo zao za inje, na kukaa juu yake.+  Wengi kati ya wale watu wakatandika nguo zao za inje katika barabara,+ na wengine walikuwa wanakata matawi ya miti na kuyatandika katika barabara.  Zaidi ya hilo, watu wengi wenye walikuwa mbele yake na wale wenye walikuwa wanamufuata wakaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Okoa, tunaomba, Mwana wa Daudi!+ Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova!*+ Umuokoe, tunaomba, wewe mwenye kuwa kwenye nafasi za juu!”+ 10  Na wakati aliingia Yerusalemu, muji wote ukakuwa katika fujo, na walikuwa wanasema: “Huyu ni nani?” 11  Wale watu wengi wakaendelea kusema: “Huyu ni nabii Yesu+ wa Nazareti ya Galilaya!” 12  Yesu akaingia katika hekalu na kufukuza wote wenye walikuwa wanauzisha na kununua ndani, na akapindua meza za wale wenye walikuwa wanabadilisha feza na viti vya wale wenye walikuwa wanauzisha njiwa.+ 13  Na akawaambia: “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala,’+ lakini ninyi munaifanya kuwa pango la wanyanganyi.”+ 14  Pia, vipofu na vilema wakamuendea katika hekalu, na akawaponyesha. 15  Wakati wakubwa wa makuhani na waandishi waliona mambo ya ajabu yenye alifanya na pia wale vijana wanaume wenye walikuwa wanasema kwa sauti kubwa katika hekalu: “Okoa, tunaomba, Mwana wa Daudi!”+ wakakasirika+ 16  na kumuambia: “Unasikia mambo yenye hawa wanasema?” Yesu akawaambia: “Ndiyo. Je, hamujasoma jambo hili, ‘Kutoka katika kinywa cha watoto wadogo na watoto wenye kunyonya umetokeza sifa’?”+ 17  Kisha akawaacha, akatoka katika muji na kuenda Betania na kulala kule.+ 18  Wakati alikuwa anarudia katika muji asubui sana, akasikia njaa.+ 19  Akaona muti wa tini pembeni ya barabara na kuukaribia, lakini hakupata kitu juu ya muti huo isipokuwa majani tu,+ na akauambia: “Usizae matunda tena hata siku moja.”+ Mara moja ule muti wa tini ukakauka. 20  Wakati wanafunzi waliona jambo hilo, wakashangaa na kusema: “Namna gani muti huu wa tini umekauka mara moja?”+ 21  Yesu akawajibu na kusema: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, kama muko na imani na hamuna mashaka, hamutafanya tu jambo lenye nilifanyia muti wa tini, lakini hata mukiambia mulima huu, ‘Ondoka na utupwe katika bahari,’ jambo hilo litatendeka.+ 22  Na mambo yote yenye munaomba katika sala, kama muko na imani, mutayapokea.”+ 23  Kisha Yesu kuingia katika hekalu, wakubwa wa makuhani na wazee wa watu wakakuja kwenye alikuwa wakati alikuwa anafundisha, na wakamuuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani alikupatia mamlaka hii?”+ 24  Yesu akawajibu na kuwaambia: “Nitawauliza pia jambo moja. Mukiniambia, halafu mimi pia nitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani: 25  Ubatizo wa Yohana, ulitoka wapi? Ulitoka mbinguni ao kwa wanadamu?” Lakini wakaanza kuambiana kati yao, na kusema: “Kama tunasema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuambia, ‘Basi, sababu gani hamukumuamini?’+ 26  Lakini kama tunasema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ tunaogopa mambo yenye watu wanaweza kututendea, kwa maana wote wanamuona Yohana kuwa nabii.” 27  Basi wakamujibu Yesu: “Hatujue.” Yesu naye akawaambia: “Na mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani. 28  “Munawaza nini? Mutu fulani alikuwa na watoto wawili. Akamuendea wa kwanza, akamuambia, ‘Mutoto wangu, leo uende kufanya kazi katika shamba la mizabibu.’ 29  Huyu akamujibu na kusema, ‘Sitaenda,’ lakini kisha, akasikitika na akaenda. 30  Akamukaribia wa pili na kumuambia jambo lilelile. Huyo akajibu, ‘Nitaenda, Bwana,’ lakini hakuenda. 31  Kati ya hao wawili, ni nani alifanya mapenzi ya baba yake?” Wakasema: “Ule wa kwanza.” Yesu akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba wakusanya-kodi na makahaba wanawatangulia ninyi kuingia katika Ufalme wa Mungu. 32  Kwa maana Yohana alikuja kwenu katika njia ya haki, lakini hamukumuamini. Hata hivyo, wakusanya-kodi na makahaba walimuamini,+ na hata kisha ninyi kuona jambo hilo, hamukusikitika ili mumuamini. 33  “Musikie mufano mwingine: Kulikuwa mutu fulani, mwenye shamba, mwenye alipanda shamba la mizabibu+ na kulizungushia ukuta, akachimba ndani yake kikamulio cha divai na akasimamisha munara;+ kisha akalikodisha kwa walimaji na akasafiri kuenda katika inchi ingine.+ 34  Wakati kipindi cha kuvuna matunda kilifika, akatuma watumwa wake kwa walimaji ili wakusanye matunda yake. 35  Lakini, walimaji wakakamata watumwa wake, mumoja wakamupiga, mwingine wakamuua, na mwingine wakamupiga majiwe.+ 36  Akatuma tena watumwa wengine, wengi kuliko wale wa kikundi cha kwanza, lakini wakawatendea vilevile.+ 37  Mwishowe akawatumia mwana wake, na kusema, ‘Watamuheshimia mwana wangu.’ 38  Wakati walimaji walimuona ule mwana, wakaambiana, ‘Huyu ndiye muriti.+ Mukuje, tumuue na tukamate uriti wake!’ 39  Kwa hiyo wakamukamata na kumutupa inje ya shamba la mizabibu na kumuua.+ 40  Basi, wakati mwenye shamba la mizabibu atakuja, atawatendea namna gani walimaji hao?” 41  Wakamuambia: “Kwa sababu ni waovu, ataleta uharibifu mubaya juu yao na kukodisha shamba hilo la mizabibu kwa walimaji wengine, wenye watamupatia matunda kwa wakati wake.” 42  Yesu akawaambia: “Je, hamujasoma hata siku moja katika Maandiko kwamba ‘Jiwe lenye wajenzi walikataa ndilo limekuwa jiwe kubwa la pembe.*+ Jambo hili limetoka kwa Yehova,* na ni la ajabu mbele ya macho yetu’?+ 43  Ndiyo sababu ninawaambia ninyi, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa taifa lenye kuzaa matunda yake. 44  Pia, mutu mwenye ataangukia jiwe hilo atavunjika-vunjika.+ Na kila mutu mwenye litaangukia, litamuponda-ponda.”+ 45  Wakati wakubwa wa makuhani na Wafarisayo walisikia mifano yake, wakajua kama alikuwa anawasema wao.+ 46  Hata kama walitaka kumukamata, waliogopa watu kwa sababu walimuona kuwa nabii.+

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Tnn., “kichwa cha pembe.”