Cha Pili cha Samweli 24:1-25
24 Kasirani ya Yehova ikawaka tena juu ya Israeli+ wakati mutu fulani alimuchochea Daudi* juu yao, kwa kusema: “Uende, uhesabie watu+ wa Israeli na Yuda.”+
2 Kwa hiyo mufalme akamuambia Yoabu+ mukubwa wa jeshi mwenye alikuwa pamoja naye: “Tafazali uende katika makabila yote ya Israeli, kuanzia Dani mupaka Beer-sheba,+ na uandikishe watu, ili nijue hesabu ya watu.”
3 Lakini Yoabu akamuambia mufalme: “Yehova Mungu wako afanye watu waongezeke mara mia moja (100), na macho ya bwana wangu mufalme yaone jambo hilo, lakini sababu gani bwana wangu mufalme anataka kufanya jambo la namna hii?”
4 Lakini neno la mufalme likakuwa na nguvu kuliko la Yoabu na la wakubwa wa jeshi. Basi Yoabu na wakubwa wa jeshi wakatoka mbele ya mufalme ili kuandikisha watu wa Israeli.+
5 Wakavuka Yordani na kupiga kambi Aroeri,+ upande wa kuume* wa muji katikati ya bonde,* kuelekea Wagadi, na mupaka Yazeri.+
6 Kisha wakaenda mupaka Gileadi+ na inchi ya Tahtim-hodshi na wakaendelea mupaka Dani-yaani na wakazunguka mupaka Sidoni.+
7 Halafu wakaenda kwenye ngome ya Tiro+ na katika miji yote ya Wahivi+ na ya Wakanaani, na mwishowe wakafika Negebu+ ya Yuda kule Beer-sheba.+
8 Kwa hiyo wakapita katika inchi yote na kuja Yerusalemu kisha miezi kenda (9) na siku makumi mbili (20).
9 Sasa Yoabu akamupatia mufalme hesabu ya watu wenye waliandikishwa. Israeli alikuwa na wapiganaji-vita elfu mia munane (800 000) wenye kubeba panga, na wanaume wa Yuda walikuwa elfu mia tano (500 000).+
10 Lakini moyo wa* Daudi ukajaa sikitiko+ kisha kuhesabia watu. Kisha Daudi akamuambia Yehova: “Nimetenda zambi+ kubwa kwa kufanya jambo hilo. Na sasa, Yehova, tafazali samehe kosa la mutumishi wako,+ kwa maana nimetenda kwa upumbavu sana.”+
11 Wakati Daudi aliamuka asubui, neno la Yehova likakuja kwa Gadi+ nabii, muonaji wa Daudi, likisema:
12 “Uende na umuambie Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Ninakupatia mambo tatu (3) ya kuchagua. Chagua jambo moja lenye nitaleta juu yako.”’”+
13 Basi Gadi akaingia kwa Daudi na kumuambia: “Je, miaka saba (7) ya njaa ikuje juu ya inchi yako?+ Ao je, ukimbie maadui wako kwa miezi tatu (3) wakati watakuwa wanakufuatilia?+ Ao inchi yako ikuwe na ugonjwa wa kuambukiza kwa siku tatu?+ Sasa fikiria kwa uangalifu jambo lenye ninapaswa kumujibu Ule mwenye alinituma.”
14 Kwa hiyo Daudi akamuambia Gadi: “Ni jambo lenye kunihangaisha sana. Tafazali, acha tuanguke katika mukono wa Yehova,+ kwa maana rehema yake ni nyingi;+ lakini usiniache nianguke katika mukono wa mwanadamu.”+
15 Kisha Yehova akatuma ugonjwa wa kuambukiza+ juu ya Israeli kuanzia asubui mupaka wakati wenye uliwekwa, na hivyo watu elfu makumi saba (70 000) wakakufa+ kuanzia Dani mupaka Beer-sheba.+
16 Wakati malaika alinyoosha mukono wake kuelekea Yerusalemu ili kuuharibu, Yehova akasikitika* kuhusu musiba huo,+ na akamuambia malaika mwenye alikuwa analeta uharibifu kati ya watu: “Inatosha! Sasa shusha mukono wako.” Malaika wa Yehova alikuwa karibu na kiwanja cha kupigia-pigia nafaka cha Arauna+ Muyebusi.+
17 Wakati Daudi alimuona malaika mwenye alikuwa anapiga na kuua watu, akamuambia Yehova: “Mimi ndiye nilifanya zambi, na mimi ndiye nilifanya kosa; lakini kondoo hawa+—wamefanya nini? Tafazali, acha mukono wako ukuje juu yangu na juu ya nyumba ya baba yangu.”+
18 Kwa hiyo Gadi akaingia kwa Daudi siku hiyo na kumuambia: “Panda, umusimamishie Yehova mazabahu kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka cha Arauna Muyebusi.”+
19 Basi Daudi akapanda kulingana na neno la Gadi, kama vile Yehova alikuwa ameamuru.
20 Wakati Arauna aliangalia chini na kumuona mufalme na watumishi wake wakikuja kumuelekea, mara moja Arauna akatoka na kuinama uso chini mbele ya mufalme.
21 Arauna akauliza: “Sababu gani Bwana wangu mufalme amekuja kwa mutumishi wake?” Daudi akajibu: “Ili kununua kiwanja chako cha kupigia-pigia nafaka kusudi nimujengee Yehova mazabahu, ili pigo lenye kuwa juu ya watu lisimamishwe.”+
22 Lakini Arauna akamuambia Daudi: “Acha bwana wangu mufalme akichukue na kutoa kitu chenye kuonekana kuwa kizuri kwake.* Angalia, hawa ndio ngombe kwa ajili ya toleo la kuteketezwa na kifaa cha kupiga-piga nafaka na vyombo vya ngombe kwa ajili ya kuni.
23 Vitu hivi vyote, Ee mufalme, Arauna anamupatia mufalme.” Kisha Arauna akamuambia mufalme: “Yehova Mungu wako akuonyeshe wema.”
24 Lakini, mufalme akamuambia Arauna: “Hapana, ninapaswa kukinunua kwa bei fulani. Sitamutolea Yehova Mungu wangu zabihu za kuteketezwa zenye hazinigarimu kitu.” Basi Daudi akanunua kiwanja hicho cha kupigia-pigia nafaka na hao ngombe kwa shekeli* makumi tano (50) za feza.+
25 Na Daudi akamujengea+ Yehova mazabahu pale na kutoa zabihu za kuteketezwa na zabihu za ushirika. Basi Yehova akakubali maombi ya kumulilia kwa ajili ya inchi,+ na pigo lenye lilikuja juu ya Israeli likasimamishwa.
Maelezo ya Chini
^ Ao “wakati Daudi alichochewa.”
^ Ao “kusini.”
^ Ao “bonde la muto.”
^ Ao “zamiri ya.”
^ Ao “akahuzunika.”
^ Tnn., “kile chenye kuwa kizuri katika macho yake.”
^ Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.