Cha Pili cha Samweli 22:1-51
22 Na Daudi akamuambia Yehova maneno ya wimbo huu+ siku yenye Yehova alimuokoa katika mukono wa maadui wake wote+ na katika mukono wa Sauli.+
2 Akasema:
“Yehova ni mwamba wangu na ngome yangu+ na Ule mwenye ananiokoa.+
3 Mungu wangu ni mwamba wangu,+ mwenye ninakimbilia,Ngao yangu+ na pembe* yangu ya wokovu,* kimbilio langu salama*+Na mahali pangu pa kukimbilia,+ mwokozi wangu;+ wewe mwenye unaniokoa katika jeuri.
4 Ninamuitia Yehova, mwenye anastahili kusifiwa,Na nitaokolewa kutoka kwa maadui wangu.
5 Mawimbi ya kifo yalinizunguka pande zote;+Mafuriko ya kushitukia ya watu wenye hawana mafaa yoyote yaliniogopesha sana.+
6 Kamba za Kaburi* zilinizunguka;+Mitego ya kifo ilikuwa mbele yangu.+
7 Katika taabu yangu nilimuitia Yehova,+Niliendelea kumuita Mungu wangu.
Kisha akiwa katika hekalu lake akasikia sauti yangu,Na kilio changu cha kuomba musaada kikafika katika masikio yake.+
8 Dunia ikaanza kutetemeka na kutikisika huku na huku;+Misingi ya mbingu ikatetemeka+Na kutikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+
9 Moshi ulipanda kutoka katika matundu ya pua yake,Na moto wenye kuteketeza ukatoka katika kinywa chake;+Makaa yenye kuwaka yakatoka kwake.
10 Alifanya mbingu zikunjame wakati alikuwa anashuka,+Na giza nzito lilikuwa chini ya miguu yake.+
11 Alipanda juu ya kerubi+ na akakuja akiruka.
Alionekana juu ya mabawa ya roho.*+
12 Kisha akatia giza kumuzunguka kama kibanda,+Katika maji yenye giza na mawingu mazito.
13 Kutoka katika mwangaza wenye kuwa mbele yake makaa yenye moto yaliwaka.
14 Kisha Yehova akaanza kunguruma akiwa mbinguni;+Mwenye Kuwa Juu Zaidi akafanya sauti yake isikike.+
15 Akapiga mishale yake+ na kuwasambaza;Umeme wa radi, na kuwatia katika muvurugo.+
16 Sehemu ya chini ya bahari ikaonekana;+Misingi ya inchi ikafunuliwa kwa kemeo la Yehova,Kwa mulipuko wa pumuzi kutoka katika matundu ya pua yake.+
17 Akiwa juu, alininyooshea mukono;Akanishika na kunikokota kutoka katika maji yenye kuenda chini sana.+
18 Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+Kutoka kwa wale wenye kunichukia, wenye walikuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19 Walinishambulia katika siku ya musiba wangu,+Lakini Yehova alikuwa tegemeo langu.
20 Alinipeleka inje na kunitia mahali kwenye usalama;*+Aliniokoa kwa sababu alipendezwa na mimi.+
21 Yehova ananipatia zawabu kulingana na haki yangu;+Ananilipa kulingana na kutokuwa na hatia kwa* mikono yangu.+
22 Kwa maana nimeshika njia za Yehova,Na sijamuacha kwa uovu Mungu wangu.
23 Hukumu zake zote+ ziko mbele yangu;Sitageuka pembeni kuacha sheria zake.+
24 Nitabakia bila lawama+ mbele yake,Na nitajiepusha na kosa.+
25 Yehova anilipe kulingana na haki yangu,+Kulingana na kutokuwa kwangu na hatia mbele yake.+
26 Kwa mutu mushikamanifu unatenda kwa ushikamanifu;+Kwa mutu mwenye hana lawama, mwenye nguvu, unatenda bila lawama;+
27 Kwa mwenye kuwa safi unajionyesha kuwa safi,+Lakini kwa mwenye kupotoka unajionyesha kuwa mwenye busara.*+
28 Kwa maana unaokoa wanyenyekevu,+Lakini macho yako yanachukia wenye majivuno, na unawashusha.+
29 Kwa maana wewe ni taa yangu, Ee Yehova;+Yehova ndiye anafanya giza langu liangaze.+
30 Kwa musaada wako ninaweza kushambulia kikundi cha wanyanganyi;Kwa nguvu za Mungu ninaweza kupanda ukuta.+
31 Njia ya Mungu wa kweli ni kamilifu;+Neno la Yehova ni lenye kusafishwa.+
Yeye ni ngao kwa wote wenye kumukimbilia.+
32 Kwa maana ni nani iko* Mungu isipokuwa Yehova?+
Na ni nani iko* mwamba isipokuwa Mungu wetu?+
33 Mungu wa kweli ndiye ngome yangu yenye nguvu,+Na atafanya njia yangu ikuwe kamilifu.+
34 Anafanya miguu yangu ikuwe kama ya paa;Ananifanya nisimame mahali pa juu.+
35 Anazoeza mikono yangu kwa ajili ya vita;Mikono yangu inaweza kukunja upinde wa shaba.
36 Unanipatia ngao yako ya wokovu,Na unyenyekevu wako unanifanya nikuwe mukubwa.+
37 Unapanua njia kwa ajili ya hatua zangu;Miguu yangu haitatereza.*+
38 Nitafuatilia maadui wangu na kuwaharibu;Sitarudia mupaka wakati watakuwa wamefutwa.
39 Na nitawafuta na kuwaponda-ponda, na hivyo hawatasimama;+Wataanguka chini ya miguu yangu.
40 Utanipatia nguvu kwa ajili ya vita;+Utafanya maadui wangu waanguke chini yangu.+
41 Utafanya maadui wangu wanikimbie;*+Nitamaliza* wale wenye kunichukia.+
42 Wanalilia musaada, lakini hakuna mutu wa kuwaokoa;Hata wanamulilia Yehova, lakini yeye hawajibu.+
43 Nitawatwanga ili wakuwe laini kama mavumbi ya dunia;Nitawaponda-ponda na kuwakanyanga-kanyanga kama matope katika barabara.
44 Utaniokoa kutokana na tabia ya watu wangu ya kutafuta-tafuta makosa.+
Utanilinda ili nikuwe kichwa cha mataifa;+Watu wenye sikujua watanitumikia.+
45 Wageni watakuja wakijikunja kwa woga mbele yangu;+Mambo yenye watasikia kunihusu yatawafanya wanitii.*
46 Wageni watakosa uhodari;*Watakuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao.
47 Yehova ni mwenye kuishi! Mwamba wangu asifiwe!+
Mungu wa mwamba wa wokovu wangu atukuzwe.+
48 Mungu wa kweli ananilipizia kisasi;+Anatiisha vikundi vya watu chini yangu;+
49 Ananiokoa kutoka kwa maadui wangu.
Unaniinua+ juu ya wale wenye kunishambulia;Unaniokoa kutokana na mutu mwenye jeuri.+
50 Ndiyo sababu nitakushukuru, Ee Yehova, kati ya mataifa,+Na nitaimbia jina lako sifa:*+
51 Anatenda matendo makubwa ya wokovu* kwa ajili ya mufalme wake;+Anamuonyesha mutiwa-mafuta wake upendo mushikamanifu,Kwa Daudi na uzao wake* milele.”+
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “mwokozi wangu mwenye nguvu.”
^ Ao “mahali pangu salama pa juu.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “ya upepo.”
^ Ao “mahali penye nafasi kubwa.”
^ Tnn., “usafi wa.”
^ Ao pengine, “unatenda kama mupumbavu.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “Vifundo vya miguu yangu havitatereza.”
^ Ao “Utanipatia migongo ya maadui wangu.”
^ Tnn., “Nitanyamazisha.”
^ Tnn., “Wakati tu sikio lao linasikia, watanitii.”
^ Ao “watafifia.”
^ Ao “nitapigia jina lako muziki.”
^ Ao “Analeta ushindi mukubwa.”
^ Tnn., “mbegu yake.”

