Utangulizi wa Sehemu ya 9
Sehemu hii inatufundisha kuhusu vijana, manabii, na wafalme walioonyesha imani ya pekee kumwelekea Yehova. Kule Siria, msichana mdogo Mwisraeli alikuwa na imani kwamba nabii wa Yehova angemponya Naamani. Nabii Elisha alikuwa na uhakika kwamba Yehova angemlinda kutokana na jeshi adui. Kuhani Mkuu Yehoyada alihatarisha uhai wake ili kumlinda Yehoashi, aliyekuwa bado mtoto, kutokana na nyanya (au bibi) yake mwovu, Athalia. Mfalme Hezekia alikuwa na uhakika kwamba Yehova angeliokoa Yerusalemu, na hata alipotishiwa na Waashuru hakusalimu amri. Mfalme Yosia aliondoa kabisa ibada ya sanamu katika nchi yote, akarekebisha hekalu, na akarudisha ibada ya kweli nchini.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 51
Shujaa na Msichana Mdogo
Msichana Mwisraeli alimweleza mke wa bwana wake kuhusu nguvu za Yehova, naye Naamani akaponywa kimuujiza.
SOMO LA 52
Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto
Jinsi mtumishi wa Elisha alivyoona kwamba ‘kuna wengi walio pamoja nasi kuliko wale walio pamoja nao.’
SOMO LA 54
Yehova Alimwonyesha Yona Subira
Ni jambo gani lililofanya nabii mmoja wa Mungu amezwe na samaki mkubwa? Alitokaje katika samaki huyo? Na Yehova alimfundisha jambo gani?
SOMO LA 55
Malaika wa Yehova Alimlinda Hezekia
Maadui wa Yuda walisema kwamba Yehova hatawalinda watu wake, lakini walikosea!
SOMO LA 56
Yosia Aliipenda Sheria ya Mungu
Yosia anaanza kutawala akiwa na umri wa miaka nane, naye anawasaidia watu wake kumwabudu Yehova.