Utangulizi wa Sehemu ya 11

Utangulizi wa Sehemu ya 11

Sehemu hii inaeleza kuhusu matukio yaliyo katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Yesu alizaliwa katika familia ya hali ya chini na waliishi katika mji mdogo. Alifanya kazi pamoja na baba yake, aliyekuwa seremala. Yesu ndiye angewaokoa wanadamu. Yehova alikuwa amemchagua kuwa Mfalme wa Ufalme wa mbinguni. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako athamini jinsi Yehova alivyochagua kwa uangalifu familia na mazingira ambayo Yesu angelelewa. Fikiria jinsi Yehova alivyomlinda Yesu asiuawe na Herode na kwamba hakuna chochote kinachoweza kuzuia kusudi la Yehova. Jifunze jinsi Yehova alivyompa Yohana mgawo wa kutayarisha njia kwa ajili ya Yesu. Kazia jinsi Yesu alivyoonyesha kwamba aliipenda hekima ya Yehova tangu alipokuwa mdogo.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 68

Elisabeti Apata Mtoto

Kwa nini mume wa Elisabeti aliambiwa kwamba hangeweza kuzungumza mpaka mtoto azaliwe?

SOMO LA 69

Gabrieli Anamtembelea Maria

Alimpa ujumbe uliobadili maisha yake.

SOMO LA 70

Malaika Watangaza Kuzaliwa kwa Yesu

Wachungaji waliosikia tangazo hilo walichukua hatua haraka.

SOMO LA 71

Yehova Alimlinda Yesu

Mfalme mwovu alitaka kumwua Yesu.

SOMO LA 72

Yesu Akiwa Kijana

Yesu akiwa hekaluni aliwashangaza walimu jinsi gani?

SOMO LA 73

Yohana Atayarisha Njia

Yohana anakuwa nabii anapokuwa mtu mzima. Anafundisha kwamba Masihi anakuja. Watu wanaitikiaje ujumbe wake?