Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Kitabu hiki kitakusaidia ujifunze historia, kuanzia simulizi la Biblia la uumbaji, kuzaliwa na huduma ya Yesu, hadi wakati wa kuja kwa Ufalme.
Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza
Kitabu hiki kinaweza kutumiwaje?
SOMO LA 1
Mungu Aliumba Mbingu na Dunia
Biblia inasema kwamba Mungu aliumba mbingu na dunia. Kwa nini Mungu alimuumba malaika mmoja kabla ya vitu vingine vyote?
SOMO LA 2
Mungu Alimuumba Mwanamume na Mwanamke wa Kwanza
Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke wa kwanza na kuwaweka katika bustani ya Edeni. Alitaka waanzishe familia na kuifanya dunia yote kuwa paradiso.
SOMO LA 3
Adamu na Hawa Hawakumtii Mungu
Kwa nini mti mmoja ulikuwa wa pekee katika bustani ya Edeni? Kwa nini Hawa alikula tunda la mti huo?
SOMO LA 4
Hasira Yasababisha Mauaji
Mungu alikubali dhabihu ya Abeli lakini aliikataa dhabihu ya Kaini. Kaini alipojua hilo alikasirika sana na akafanya jambo baya sana.
SOMO LA 5
Safina ya Noa
Malaika walipokuja duniani na kujichukulia wanawake, walizaa watoto ambao walikuwa majitu. Jeuri ilienea kotekote. Lakini Noa alikuwa tofauti—alimpenda na kumtii Mungu.
SOMO LA 6
Watu Nane Waliokoka na Kuingia Katika Ulimwengu Mpya
Mvua ya Gharika ilinyesha kwa siku 40 mchana na usiku. Noa na familia yake walikaa ndani ya safina kwa zaidi ya mwaka mmoja. Hatimaye, Mungu aliwaambia watoke katika safina.
SOMO LA 7
Mnara wa Babeli
Baadhi ya watu waliamua kujenga jiji na mnara ambao kilele chake kingefika mbinguni. Kwa nini Mungu alifanya wazungumze lugha tofauti-tofauti ghafla?
SOMO LA 8
Abrahamu na Sara Walimtii Mungu
Kwa nini Abrahamu na Sara waliacha maisha yao mazuri na kuhamia nchi ya Kanaani?
SOMO LA 9
Hatimaye Wapata Mtoto!
Mungu angetimizaje ahadi yake kwa Abrahamu? Ni mtoto yupi wa Abrahamu angehusika—Isaka au Ishmaeli?
SOMO LA 10
Mkumbuke Mke wa Loti
Mungu alinyesha mvua ya moto na kiberiti katika majiji ya Sodoma and Gomora. Kwa nini majiji hayo yaliharibiwa? Kwa nini tunapaswa kumkumbuka mke wa Loti?
SOMO LA 11
Jaribu la Imani
Mungu alimwambia Abrahamu hivi: ‘Tafadhali, mchukue mwana wako wa pekee na umtoe akiwa dhabihu kwenye mlima Moria.’ Abrahamu angekabili jinsi gani jaribu hilo la imani?
SOMO LA 12
Yakobo Alipewa Urithi
Isaka na Rebeka walikuwa na watoto wawili mapacha Esau na Yakobo. Kwa kuwa Esau alikuwa mzaliwa wa kwanza, angepata urithi wa pekee. Kwa nini aliuza haki hiyo kwa bakuli la mchuzi?
SOMO LA 13
Yakobo na Esau Wafanya Amani
Yakobo alipata baraka kutoka kwa malaika jinsi gani? Na alifanyaje amani na Esau?
SOMO LA 14
Mtumwa Aliyemtii Mungu
Yosefu alifanya mambo mazuri, lakini bado aliteseka sana. Kwa nini?
SOMO LA 15
Yehova Hakumsahau Yosefu Kamwe
Ingawa Yosefu alikuwa mbali na familia yao, Mungu alimthibitishia kwamba alikuwa pamoja naye.
SOMO LA 17
Musa Aliamua Kumwabudu Yehova
Alipokuwa mtoto, Musa aliokolewa kwa sababu ya hekima ya mama yake.
SOMO LA 19
Mapigo Matatu ya Kwanza
Farao aliwasababishia watu wake msiba kwa sababu kiburi kilimzuia kuchukua hatua moja tu rahisi.
SOMO LA 21
Pigo la Kumi
Pigo la mwisho lilikuwa baya sana hivi kwamba mwishowe hata Farao mwenye kiburi alikubali kuwaruhusu Waisraeli waondoke.
SOMO LA 22
Muujiza Katika Bahari Nyekundu
Farao aliokoka mapigo kumi, lakini je, aliokoka muujiza huu wa Mungu?
SOMO LA 23
Waisraeli Wamtolea Yehova Ahadi
Waisraeli walimtolea Mungu ahadi ya pekee walipokuwa wamepiga kambi kwenye Mlima Sinai.
SOMO LA 26
Wale Wapelelezi Kumi na Wawili
Yoshua na Kalebu walikuwa tofauti na wale wapelelezi wengine kumi ambao waliipeleleza nchi ya Kanaani.
SOMO LA 27
Walimwasi Yehova
Kora, Dathani, Abiramu, na wanaume wengine 250 walikosa kutambua jambo fulani muhimu kumhusu Yehova.
SOMO LA 30
Rahabu Awaficha Wapelelezi
Kuta za Yeriko zilianguka chini. Lakini nyumba ya Rahabu iliendelea kusimama, hata ingawa ilikuwa imejengwa kwenye ukuta.
SOMO LA 31
Yoshua na Wagibeoni
Yoshua alisali kwa Mungu na kusema: “Jua, simama tuli!” Je, Mungu alijibu?
SOMO LA 32
Kiongozi Mpya na Wanawake Wawili Jasiri
Baada ya Yoshua kufa, Waisraeli walianza kuabudu sanamu. Maisha yakawa magumu, lakini Yehova akawasaidia kupitia mwamuzi Baraka, nabii wa kike Debora, na Yaeli na kigingi cha hema lake!
SOMO LA 33
Ruthu na Naomi
Wanawake wawili ambao walifiwa na waume zao walirudi Israeli. Mmoja kati ya wanawake hao, Ruthu, alienda kufanya kazi mashambani, na huko Boazi akamwona.
SOMO LA 34
Gideoni Aliwashinda Wamidiani
Baada ya Wamidiani kuwakandamiza Waisraeli kwa muda fulani, watu walianza kumwomba Yehova msaada. Jeshi dogo la Gideoni liliwezaje kuwashinda askari 135,000 wa Wamidiani?
SOMO LA 35
Hana Alisali Ili Apate Mwana
Elkana aliwapeleka Hana, Penina, na watoto wao ili wakaabudu katika maskani huko Shilo. Wakiwa huko, Hana alisali ili apate mwana. Mwaka uliofuata , Samweli akazaliwa!
SOMO LA 36
Ahadi ya Yeftha
Yeftha alitoa ahadi gani, na kwa nini? Binti ya Yeftha alitendaje kuhusu ahadi ya baba yake?
SOMO LA 37
Yehova Azungumza na Samweli
Kuhani Mkuu Eli alikuwa na wana wawili waliotumikia wakiwa makuhani katika maskani, lakini hawakutii sheria za Mungu. Kijana Samweli alikuwa tofauti na Yehova alizungumza naye.
SOMO LA 38
Yehova Alimfanya Samsoni Awe na Nguvu
Mungu alimfanya Samsoni alimpatia nguvu nyingi za kupigana na Wafilisti lakini Samsoni alipofanya uamuzi mbaya, Wafilisti walimkamata.
SOMO LA 39
Mfalme wa Kwanza wa Israeli
Ingawa Yehova alikuwa amewapa Waisraeli waamuzi wa kuwaongoza, bado walitaka wawe na mfalme. Samweli alimtia mafuta Sauli awe mfalme wa kwanza wa Israeli, lakini baadaye Yehova alimkataa Sauli. Kwa nini?
SOMO LA 40
Daudi na Goliathi
Yehova anamchagua Daudi kuwa mfalme wa Israeli anayefuata, na Daudi anaonyesha kwa nini huo ulikuwa uchaguzi unaofaa.
SOMO LA 41
Daudi na Sauli
Kwa nini mwanamume mmoja alimchukia mwenzake, na yule aliyechukiwa alitendaje?
SOMO LA 42
Yonathani Alikuwa Jasiri na Mshikamanifu
Mwana wa mfalme alikuwa rafiki wa karibu wa Daudi.
SOMO LA 44
Hekalu kwa Ajili ya Yehova
Mungu alikubali ombi la Mfalme Sulemani na kumpa mapendeleo mengi.
SOMO LA 49
Malkia Mwovu Aadhibiwa
Yezebeli anapanga njama ya kumwua Nabothi ili amnyang’anye shamba lake la mizabibu! Yehova Mungu anaona uovu na tendo lake la ukosefu wa haki.
SOMO LA 50
Yehova Amlinda Yehoshafati
Mfalme Yehoshafati anasali kwa Mungu Yuda inapotishiwa na mataifa adui.
SOMO LA 51
Shujaa na Msichana Mdogo
Msichana Mwisraeli alimweleza mke wa bwana wake kuhusu nguvu za Yehova, naye Naamani akaponywa kimuujiza.
SOMO LA 52
Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto
Jinsi mtumishi wa Elisha alivyoona kwamba ‘kuna wengi walio pamoja nasi kuliko wale walio pamoja nao.’
SOMO LA 54
Yehova Alimwonyesha Yona Subira
Ni jambo gani lililofanya nabii mmoja wa Mungu amezwe na samaki mkubwa? Alitokaje katika samaki huyo? Na Yehova alimfundisha jambo gani?
SOMO LA 55
Malaika wa Yehova Alimlinda Hezekia
Maadui wa Yuda walisema kwamba Yehova hatawalinda watu wake, lakini walikosea!
SOMO LA 56
Yosia Aliipenda Sheria ya Mungu
Yosia anaanza kutawala akiwa na umri wa miaka nane, naye anawasaidia watu wake kumwabudu Yehova.
SOMO LA 57
Yehova Amtuma Yeremia Akahubiri
Mambo ambayo nabii huyu kijana alisema yaliwafanya wazee wa Yuda wakasirike sana.
SOMO LA 58
Yerusalemu Laharibiwa
Watu wa Yuda wanaendelea kuabudu miungu ya uwongo, hivyo Yehova anawaacha.
SOMO LA 59
Wavulana Wanne Waliomtii Yehova
Wavulana Wayudea waliazimia kubaki waaminifu kwa Yehova hata walipokuwa katika makao ya mfalme huko Babiloni.
SOMO LA 61
Hawakuinamia Sanamu
Shadraki, Meshaki, na Abednego wanakataa kuabudu sanamu ya dhahabu ya mfalme wa Babiloni.
SOMO LA 65
Esta Awaokoa Watu Wake
Ingawa alikuwa yatima kutoka nchi nyingine, baadaye alikuwa malkia.
SOMO LA 66
Ezra Alifundisha Sheria ya Mungu
Baada ya Waisraeli kumsikiliza Ezra, walimtolea Mungu ahadi ya pekee.
SOMO LA 67
Kuta za Yerusalemu
Nehemia alipogundua kwamba maadui wake walitaka kuwashambulia, kwa nini hakuogopa?
SOMO LA 68
Elisabeti Apata Mtoto
Kwa nini mume wa Elisabeti aliambiwa kwamba hangeweza kuzungumza mpaka mtoto azaliwe?
SOMO LA 70
Malaika Watangaza Kuzaliwa kwa Yesu
Wachungaji waliosikia tangazo hilo walichukua hatua haraka.
SOMO LA 73
Yohana Atayarisha Njia
Yohana anakuwa nabii anapokuwa mtu mzima. Anafundisha kwamba Masihi anakuja. Watu wanaitikiaje ujumbe wake?
SOMO LA 74
Yesu Anakuwa Masihi
Yohana anamaanisha nini anaposema kwamba Yesu ndiye Mwana-Kondoo wa Mungu?
Ibilisi Anamjaribu Yesu
Ibilisi anamjaribu Yesu mara tatu. Yesu alijaribiwa kwa njia gani tatu? Yesu anatendaje?
SOMO LA 76
Yesu Analisafisha Hekalu
Kwa nini Yesu anawafukuza wanyama nje ya hekalu na kupindua meza za wanaobadili pesa?
SOMO LA 77
Mwanamke Kisimani
Mwanamke Msamaria anashangaa kwamba Yesu anazungumza naye. Kwa nini? Yesu anamwambia jambo gani ambalo hakuwa amemwambia mtu mwingine yeyote?
SOMO LA 78
Yesu Anahubiri Ujumbe wa Ufalme
Yesu anawaalika baadhi ya wanafunzi wake wawe ‘wavuvi wa watu.’ Baadaye, anawazoeza 70 kati ya wafuasi wake kuhubiri habari njema.
SOMO LA 79
Yesu Anafanya Miujiza Mingi
Popote anapoenda, wagonjwa wanamfikia ili awasaidie, naye anawaponya wote. Hata anamfufua msichana mdogo.
SOMO LA 80
Yesu Anachagua Mitume Kumi na Wawili
Kwa nini Yesu anawachagua? Je, unakumbuka majina yao?
SOMO LA 82
Yesu Awafundisha Wanafunzi Wake Jinsi ya Kusali
Yesu aliwaambia wanafunzi wake waendelee kuomba mambo gani?
SOMO LA 84
Yesu Anatembea Juu ya Maji
Je, unaweza kuwazia jinsi ambavyo mitume walihisi walipoona muujiza huo?
SOMO LA 85
Yesu Aponya Siku ya Sabato
Kwa nini si watu wote waliofurahishwa na mambo ambayo Yesu alifanya?
SOMO LA 86
Yesu Amfufua Lazaro
Yesu alipomwona Maria akilia, yeye pia alianza kulia. Hata hivyo, huzuni yao ikageuka na kuwa shangwe.
SOMO LA 87
Mlo wa Mwisho wa Jioni wa Yesu
Yesu aliwapa mitume wake maagizo muhimu wakati wa mlo wao wa mwisho wakiwa pamoja.
SOMO LA 88
Yesu Akamatwa
Yuda Iskariote aliongoza umati wa watu wenye marungu na mapanga ili wamkamate Yesu.
SOMO LA 89
Petro Anamkana Yesu
Ni nini kilichotendeka katika ua wa nyumba ya Kayafa? Yesu alitendewa jinsi gani ndani ya nyumba hiyo?
SOMO LA 91
Yesu Afufuliwa
Ni mambo gani yenye kupendeza yanayotokea siku kadhaa baada ya Yesu kuuawa?
SOMO LA 93
Yesu Arudi Mbinguni
Lakini kabla ya kufanya hivyo, anawapa wanafunzi wake maagizo muhimu sana.
SOMO LA 95
Hakuna Chochote Ambacho Kingeweza Kuwazuia
Viongozi wa kidini waliofanya Yesu auawe, sasa wanajaribu kuwanyamazisha wanafunzi. Lakini hawaweza.
SOMO LA 96
Yesu Amchagua Sauli
Sauli ni adui mkatili wa Wakristo, lakini angebadilika baada ya muda mfupi.
SOMO LA 97
Kornelio Apokea Roho Takatifu
Kwa nini Mungu alimtuma Petro nyumbani kwa mwanamume huyo, ambaye si Myahudi?
SOMO LA 98
Ukristo Waenea Katika Mataifa Mengi
Mtume Paulo na waandamani wake waanza kuhubiri katika maeneo ya mbali.
SOMO LA 99
Mlinzi wa Jela Ajifunza Kweli
Roho mwovu, tetemeko la ardhi, na upanga vinahusikaje katika hadithi hii?
SOMO LA 100
Paulo na Timotheo
Wanaume hao wawili walifanya kazi pamoja kwa miaka mingi wakiwa marafiki na wafanyakazi wenzi.
SOMO LA 101
Paulo Apelekwa Roma
Safari imejaa hatari, lakini hakuna hali yoyote ngumu inayoweza kumzuia mtume huyu.
SOMO LA 103
“Ufalme Wako na Uje”
Ufunuo kwa Yohana unaonyesha jinsi Ufalme wa Mungu utakavyobadili maisha duniani.