Utangulizi wa Sehemu ya 1

Utangulizi wa Sehemu ya 1

Biblia inaanza kwa kusimulia kuhusu uumbaji. Tunapotazama tunaona vitu vingi vizuri ambavyo Yehova ameumba, vilivyo mbinguni na duniani. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako kuona uzuri wa uumbaji. Mweleze kwamba Mungu aliwaumba wanadamu wakiwa tofauti sana na wanyama, kwa kuwapa uwezo wa kuongea, kufikiri, kubuni, kuimba, na kusali. Msaidie athamini nguvu na hekima ya Yehova na jambo muhimu zaidi upendo wake kwa viumbe wote—kutia ndani kila mmoja wetu.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 1

Mungu Aliumba Mbingu na Dunia

Biblia inasema kwamba Mungu aliumba mbingu na dunia. Kwa nini Mungu alimuumba malaika mmoja kabla ya vitu vingine vyote?

SOMO LA 2

Mungu Alimuumba Mwanamume na Mwanamke wa Kwanza

Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke wa kwanza na kuwaweka katika bustani ya Edeni. Alitaka waanzishe familia na kuifanya dunia yote kuwa paradiso.