Utangulizi wa Sehemu ya 6
Waisraeli walipofika Nchi ya Ahadi, maskani ikawa kitovu cha ibada ya kweli. Makuhani waliwafundisha watu Sheria, na waamuzi wakaongoza taifa hilo. Sehemu hii inaonyesha jinsi maamuzi na matendo ya mtu yanavyoweza kuwaathiri sana watu wengine. Kila Mwisraeli alikuwa na wajibu mbele za Yehova na kwa watu wengine. Onyesha jinsi mifano mizuri ya Debora, Naomi, Yoshua, Hana, binti ya Yeftha, na Samweli ilivyowachochea wengine. Kazia kwamba hata watu fulani ambao hawakuwa Waisraeli, kama vile Rahabu, Ruthu, Yaeli, na Wagibeoni waliamua kujiunga na Waisraeli kwa kuwa walitambua kwamba Mungu alikuwa pamoja nao.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 30
Rahabu Awaficha Wapelelezi
Kuta za Yeriko zilianguka chini. Lakini nyumba ya Rahabu iliendelea kusimama, hata ingawa ilikuwa imejengwa kwenye ukuta.
SOMO LA 31
Yoshua na Wagibeoni
Yoshua alisali kwa Mungu na kusema: “Jua, simama tuli!” Je, Mungu alijibu?
SOMO LA 32
Kiongozi Mpya na Wanawake Wawili Jasiri
Baada ya Yoshua kufa, Waisraeli walianza kuabudu sanamu. Maisha yakawa magumu, lakini Yehova akawasaidia kupitia mwamuzi Baraka, nabii wa kike Debora, na Yaeli na kigingi cha hema lake!
SOMO LA 33
Ruthu na Naomi
Wanawake wawili ambao walifiwa na waume zao walirudi Israeli. Mmoja kati ya wanawake hao, Ruthu, alienda kufanya kazi mashambani, na huko Boazi akamwona.
SOMO LA 34
Gideoni Aliwashinda Wamidiani
Baada ya Wamidiani kuwakandamiza Waisraeli kwa muda fulani, watu walianza kumwomba Yehova msaada. Jeshi dogo la Gideoni liliwezaje kuwashinda askari 135,000 wa Wamidiani?
SOMO LA 35
Hana Alisali Ili Apate Mwana
Elkana aliwapeleka Hana, Penina, na watoto wao ili wakaabudu katika maskani huko Shilo. Wakiwa huko, Hana alisali ili apate mwana. Mwaka uliofuata , Samweli akazaliwa!
SOMO LA 36
Ahadi ya Yeftha
Yeftha alitoa ahadi gani, na kwa nini? Binti ya Yeftha alitendaje kuhusu ahadi ya baba yake?
SOMO LA 37
Yehova Azungumza na Samweli
Kuhani Mkuu Eli alikuwa na wana wawili waliotumikia wakiwa makuhani katika maskani, lakini hawakutii sheria za Mungu. Kijana Samweli alikuwa tofauti na Yehova alizungumza naye.
SOMO LA 38
Yehova Alimfanya Samsoni Awe na Nguvu
Mungu alimfanya Samsoni alimpatia nguvu nyingi za kupigana na Wafilisti lakini Samsoni alipofanya uamuzi mbaya, Wafilisti walimkamata.

