MASOMO UNAYOWEZA KUJIFUNZA KATIKA BIBLIA

Utangulizi wa Sehemu ya 8

Kiswahili
Utangulizi wa Sehemu ya 8
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/1102016138/univ/art/1102016138_univ_sqr_xl.jpg
lfb kur. 106-107

Utangulizi wa Sehemu ya 8

Utangulizi wa Sehemu ya 8

Yehova alimbariki Sulemani kwa kumpa hekima nyingi na akampa pendeleo la kujenga hekalu. Hata hivyo, hatua kwa hatua Sulemani alimwacha Yehova. Ikiwa wewe ni mzazi, mweleze mtoto wako jinsi walioabudu sanamu walivyomfanya Sulemani amwasi Mungu. Ufalme uligawanyika na wafalme wabaya wakawafanya watu wawe waasi-imani na waabudu sanamu. Wakati huo, manabii wengi washikamanifu wa Yehova waliteswa na kuuawa. Malkia Yezebeli aliwafanya watu wa ufalme wa kaskazini watumbukie zaidi katika uasi-imani. Hicho kilikuwa kipindi kibaya sana katika historia ya Israeli. Lakini bado kulikuwa na watumishi wengi waaminifu wa Yehova, kutia ndani Mfalme Yehoshafati na nabii Eliya.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 44

Hekalu kwa Ajili ya Yehova

Mungu alikubali ombi la Mfalme Sulemani na kumpa mapendeleo mengi.

SOMO LA 45

Ufalme Wagawanyika

Waisraeli wengi waliacha kumwabudu Yehova.

SOMO LA 46

Jaribio Kwenye Mlima Karmeli

Mungu wa kweli ni nani? Yehova au Baali?

SOMO LA 47

Yehova Amwimarisha Eliya

Je, unafikiri anaweza kukuimarisha pia?

SOMO LA 48

Mwana wa Mjane Afanywa Kuwa Hai Tena

Miujiza miwili katika nyumba ileile!

SOMO LA 49

Malkia Mwovu Aadhibiwa

Yezebeli anapanga njama ya kumwua Nabothi ili amnyang’anye shamba lake la mizabibu! Yehova Mungu anaona uovu na tendo lake la ukosefu wa haki.

SOMO LA 50

Yehova Amlinda Yehoshafati

Mfalme Yehoshafati anasali kwa Mungu Yuda inapotishiwa na mataifa adui.