Utangulizi wa Sehemu ya 8
Yehova alimbariki Sulemani kwa kumpa hekima nyingi na akampa pendeleo la kujenga hekalu. Hata hivyo, hatua kwa hatua Sulemani alimwacha Yehova. Ikiwa wewe ni mzazi, mweleze mtoto wako jinsi walioabudu sanamu walivyomfanya Sulemani amwasi Mungu. Ufalme uligawanyika na wafalme wabaya wakawafanya watu wawe waasi-imani na waabudu sanamu. Wakati huo, manabii wengi washikamanifu wa Yehova waliteswa na kuuawa. Malkia Yezebeli aliwafanya watu wa ufalme wa kaskazini watumbukie zaidi katika uasi-imani. Hicho kilikuwa kipindi kibaya sana katika historia ya Israeli. Lakini bado kulikuwa na watumishi wengi waaminifu wa Yehova, kutia ndani Mfalme Yehoshafati na nabii Eliya.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 44
Hekalu kwa Ajili ya Yehova
Mungu alikubali ombi la Mfalme Sulemani na kumpa mapendeleo mengi.
SOMO LA 49
Malkia Mwovu Aadhibiwa
Yezebeli anapanga njama ya kumwua Nabothi ili amnyang’anye shamba lake la mizabibu! Yehova Mungu anaona uovu na tendo lake la ukosefu wa haki.
SOMO LA 50
Yehova Amlinda Yehoshafati
Mfalme Yehoshafati anasali kwa Mungu Yuda inapotishiwa na mataifa adui.

