MASOMO UNAYOWEZA KUJIFUNZA KATIKA BIBLIA

Utangulizi wa Sehemu ya 3

Kiswahili
Utangulizi wa Sehemu ya 3
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/1102016133/univ/art/1102016133_univ_sqr_xl.jpg
lfb kur. 22-23

Utangulizi wa Sehemu ya 3

Utangulizi wa Sehemu ya 3

Baada ya Gharika, Biblia inasimulia kuhusu watu wachache waliomtumikia Yehova. Mmoja wao ni Abrahamu, aliyejulikana kuwa rafiki ya Yehova. Kwa nini aliitwa rafiki ya Yehova? Ikiwa wewe ni mzazi, mfundishe mtoto wako kwamba Yehova anapendezwa naye kibinafsi na anataka kumsaidia. Kama Abrahamu na wanaume wengine waaminifu, kama vile Loti na Yakobo, tunaweza kumwomba Yehova atusaidie. Tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atatimiza ahadi zake zote.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 7

Mnara wa Babeli

Baadhi ya watu waliamua kujenga jiji na mnara ambao kilele chake kingefika mbinguni. Kwa nini Mungu alifanya wazungumze lugha tofauti-tofauti ghafla?

SOMO LA 8

Abrahamu na Sara Walimtii Mungu

Kwa nini Abrahamu na Sara waliacha maisha yao mazuri na kuhamia nchi ya Kanaani?

SOMO LA 9

Hatimaye Wapata Mtoto!

Mungu angetimizaje ahadi yake kwa Abrahamu? Ni mtoto yupi wa Abrahamu angehusika​—⁠Isaka au Ishmaeli?

SOMO LA 10

Mkumbuke Mke wa Loti

Mungu alinyesha mvua ya moto na kiberiti katika majiji ya Sodoma and Gomora. Kwa nini majiji hayo yaliharibiwa? Kwa nini tunapaswa kumkumbuka mke wa Loti?

SOMO LA 11

Jaribu la Imani

Mungu alimwambia Abrahamu hivi: ‘Tafadhali, mchukue mwana wako wa pekee na umtoe akiwa dhabihu kwenye mlima Moria.’ Abrahamu angekabili jinsi gani jaribu hilo la imani?

SOMO LA 12

Yakobo Alipewa Urithi

Isaka na Rebeka walikuwa na watoto wawili mapacha Esau na Yakobo. Kwa kuwa Esau alikuwa mzaliwa wa kwanza, angepata urithi wa pekee. Kwa nini aliuza haki hiyo kwa bakuli la mchuzi?

SOMO LA 13

Yakobo na Esau Wafanya Amani

Yakobo alipata baraka kutoka kwa malaika jinsi gani? Na alifanyaje amani na Esau?