Utangulizi wa Sehemu ya 3
Baada ya Gharika, Biblia inasimulia kuhusu watu wachache waliomtumikia Yehova. Mmoja wao ni Abrahamu, aliyejulikana kuwa rafiki ya Yehova. Kwa nini aliitwa rafiki ya Yehova? Ikiwa wewe ni mzazi, mfundishe mtoto wako kwamba Yehova anapendezwa naye kibinafsi na anataka kumsaidia. Kama Abrahamu na wanaume wengine waaminifu, kama vile Loti na Yakobo, tunaweza kumwomba Yehova atusaidie. Tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atatimiza ahadi zake zote.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 7
Mnara wa Babeli
Baadhi ya watu waliamua kujenga jiji na mnara ambao kilele chake kingefika mbinguni. Kwa nini Mungu alifanya wazungumze lugha tofauti-tofauti ghafla?
SOMO LA 8
Abrahamu na Sara Walimtii Mungu
Kwa nini Abrahamu na Sara waliacha maisha yao mazuri na kuhamia nchi ya Kanaani?
SOMO LA 9
Hatimaye Wapata Mtoto!
Mungu angetimizaje ahadi yake kwa Abrahamu? Ni mtoto yupi wa Abrahamu angehusika—Isaka au Ishmaeli?
SOMO LA 10
Mkumbuke Mke wa Loti
Mungu alinyesha mvua ya moto na kiberiti katika majiji ya Sodoma and Gomora. Kwa nini majiji hayo yaliharibiwa? Kwa nini tunapaswa kumkumbuka mke wa Loti?
SOMO LA 11
Jaribu la Imani
Mungu alimwambia Abrahamu hivi: ‘Tafadhali, mchukue mwana wako wa pekee na umtoe akiwa dhabihu kwenye mlima Moria.’ Abrahamu angekabili jinsi gani jaribu hilo la imani?
SOMO LA 12
Yakobo Alipewa Urithi
Isaka na Rebeka walikuwa na watoto wawili mapacha Esau na Yakobo. Kwa kuwa Esau alikuwa mzaliwa wa kwanza, angepata urithi wa pekee. Kwa nini aliuza haki hiyo kwa bakuli la mchuzi?
SOMO LA 13
Yakobo na Esau Wafanya Amani
Yakobo alipata baraka kutoka kwa malaika jinsi gani? Na alifanyaje amani na Esau?

