Utangulizi wa Sehemu ya 10
Yehova ni Mfalme juu ya kila kitu. Sikuzote amekuwa na mamlaka juu ya kila kitu, naye ataendelea kuwa na mamlaka. Kwa mfano, Yeremia alipotupwa ndani ya shimo, Yehova alimwokoa ili asife. Alimwokoa Shadraki, Meshaki, na Abednego kutoka katika tanuru la moto na akamwokoa Danieli kutoka katika vinywa vya simba. Yehova alimlinda Esta ili aokoe taifa lake lote. Hataruhusu uovu uendelee milele. Unabii kuhusu ile sanamu kubwa na mti mkubwa unatoa uhakikisho kwamba hivi karibuni Ufalme wa Yehova utaondoa uovu wote na kutawala dunia.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 57
Yehova Amtuma Yeremia Akahubiri
Mambo ambayo nabii huyu kijana alisema yaliwafanya wazee wa Yuda wakasirike sana.
SOMO LA 58
Yerusalemu Laharibiwa
Watu wa Yuda wanaendelea kuabudu miungu ya uwongo, hivyo Yehova anawaacha.
SOMO LA 59
Wavulana Wanne Waliomtii Yehova
Wavulana Wayudea waliazimia kubaki waaminifu kwa Yehova hata walipokuwa katika makao ya mfalme huko Babiloni.
SOMO LA 61
Hawakuinamia Sanamu
Shadraki, Meshaki, na Abednego wanakataa kuabudu sanamu ya dhahabu ya mfalme wa Babiloni.
SOMO LA 65
Esta Awaokoa Watu Wake
Ingawa alikuwa yatima kutoka nchi nyingine, baadaye alikuwa malkia.
SOMO LA 66
Ezra Alifundisha Sheria ya Mungu
Baada ya Waisraeli kumsikiliza Ezra, walimtolea Mungu ahadi ya pekee.
SOMO LA 67
Kuta za Yerusalemu
Nehemia alipogundua kwamba maadui wake walitaka kuwashambulia, kwa nini hakuogopa?

