MASOMO UNAYOWEZA KUJIFUNZA KATIKA BIBLIA

Utangulizi wa Sehemu ya 10

Kiswahili
Utangulizi wa Sehemu ya 10
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/1102016140/univ/art/1102016140_univ_sqr_xl.jpg
lfb kur. 136-137

Utangulizi wa Sehemu ya 10

Utangulizi wa Sehemu ya 10

Yehova ni Mfalme juu ya kila kitu. Sikuzote amekuwa na mamlaka juu ya kila kitu, naye ataendelea kuwa na mamlaka. Kwa mfano, Yeremia alipotupwa ndani ya shimo, Yehova alimwokoa ili asife. Alimwokoa Shadraki, Meshaki, na Abednego kutoka katika tanuru la moto na akamwokoa Danieli kutoka katika vinywa vya simba. Yehova alimlinda Esta ili aokoe taifa lake lote. Hataruhusu uovu uendelee milele. Unabii kuhusu ile sanamu kubwa na mti mkubwa unatoa uhakikisho kwamba hivi karibuni Ufalme wa Yehova utaondoa uovu wote na kutawala dunia.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 57

Yehova Amtuma Yeremia Akahubiri

Mambo ambayo nabii huyu kijana alisema yaliwafanya wazee wa Yuda wakasirike sana.

SOMO LA 58

Yerusalemu Laharibiwa

Watu wa Yuda wanaendelea kuabudu miungu ya uwongo, hivyo Yehova anawaacha.

SOMO LA 59

Wavulana Wanne Waliomtii Yehova

Wavulana Wayudea waliazimia kubaki waaminifu kwa Yehova hata walipokuwa katika makao ya mfalme huko Babiloni.

SOMO LA 60

Ufalme Ambao Utadumu Milele

Danieli aeleza maana ya ndoto ya ajabu ya Nebukadneza.

SOMO LA 61

Hawakuinamia Sanamu

Shadraki, Meshaki, na Abednego wanakataa kuabudu sanamu ya dhahabu ya mfalme wa Babiloni.

SOMO LA 62

Ufalme Unaofananishwa na Mti Mkubwa

Ndoto ya Nebukadneza yatabiri wakati wake ujao.

SOMO LA 63

Maandishi Ukutani

Maandishi hayo ya ajabu yalitokea wakati gani, na yalimaanisha nini?

SOMO LA 64

Danieli Ndani ya Shimo la Simba

Sali kwa Yehova kila siku, kama Danieli alivyofanya!

SOMO LA 65

Esta Awaokoa Watu Wake

Ingawa alikuwa yatima kutoka nchi nyingine, baadaye alikuwa malkia.

SOMO LA 66

Ezra Alifundisha Sheria ya Mungu

Baada ya Waisraeli kumsikiliza Ezra, walimtolea Mungu ahadi ya pekee.

SOMO LA 67

Kuta za Yerusalemu

Nehemia alipogundua kwamba maadui wake walitaka kuwashambulia, kwa nini hakuogopa?