Utangulizi wa Sehemu ya 14
Wakristo wa mapema walieneza habari njema ya Ufalme mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia. Yesu aliwaelekeza mahali pa kuhubiri na akawawezesha kimuujiza kuwafundisha watu katika lugha zao wenyewe. Yehova aliwapa ujasiri na nguvu za kukabiliana na mateso makali.
Yesu alimpa mtume Yohana maono ya utukufu wa Yehova. Katika maono mengine, Yohana aliona Ufalme wa mbinguni ukimshinda Shetani na kukomesha utawala wake milele. Yohana alimwona Yesu akitawala akiwa Mfalme pamoja na watawala wenzake 144,000. Pia, Yohana aliona dunia yote ikigeuzwa kuwa paradiso ambapo watu wote wanamwabudu Yehova kwa amani na umoja.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 95
Hakuna Chochote Ambacho Kingeweza Kuwazuia
Viongozi wa kidini waliofanya Yesu auawe, sasa wanajaribu kuwanyamazisha wanafunzi. Lakini hawaweza.
SOMO LA 96
Yesu Amchagua Sauli
Sauli ni adui mkatili wa Wakristo, lakini angebadilika baada ya muda mfupi.
SOMO LA 97
Kornelio Apokea Roho Takatifu
Kwa nini Mungu alimtuma Petro nyumbani kwa mwanamume huyo, ambaye si Myahudi?
SOMO LA 98
Ukristo Waenea Katika Mataifa Mengi
Mtume Paulo na waandamani wake waanza kuhubiri katika maeneo ya mbali.
SOMO LA 99
Mlinzi wa Jela Ajifunza Kweli
Roho mwovu, tetemeko la ardhi, na upanga vinahusikaje katika hadithi hii?
SOMO LA 100
Paulo na Timotheo
Wanaume hao wawili walifanya kazi pamoja kwa miaka mingi wakiwa marafiki na wafanyakazi wenzi.
SOMO LA 101
Paulo Apelekwa Roma
Safari imejaa hatari, lakini hakuna hali yoyote ngumu inayoweza kumzuia mtume huyu.
SOMO LA 103
“Ufalme Wako na Uje”
Ufunuo kwa Yohana unaonyesha jinsi Ufalme wa Mungu utakavyobadili maisha duniani.

