MASOMO UNAYOWEZA KUJIFUNZA KATIKA BIBLIA

Utangulizi wa Sehemu ya 14

Kiswahili
Utangulizi wa Sehemu ya 14
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/1102016144/univ/art/1102016144_univ_sqr_xl.jpg
lfb kur. 218-219

Utangulizi wa Sehemu ya 14

Utangulizi wa Sehemu ya 14

Wakristo wa mapema walieneza habari njema ya Ufalme mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia. Yesu aliwaelekeza mahali pa kuhubiri na akawawezesha kimuujiza kuwafundisha watu katika lugha zao wenyewe. Yehova aliwapa ujasiri na nguvu za kukabiliana na mateso makali.

Yesu alimpa mtume Yohana maono ya utukufu wa Yehova. Katika maono mengine, Yohana aliona Ufalme wa mbinguni ukimshinda Shetani na kukomesha utawala wake milele. Yohana alimwona Yesu akitawala akiwa Mfalme pamoja na watawala wenzake 144,000. Pia, Yohana aliona dunia yote ikigeuzwa kuwa paradiso ambapo watu wote wanamwabudu Yehova kwa amani na umoja.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 94

Wanafunzi Wapokea Roho Takatifu

Roho takatifu iliwapatia nguvu gani kimuujiza?

SOMO LA 95

Hakuna Chochote Ambacho Kingeweza Kuwazuia

Viongozi wa kidini waliofanya Yesu auawe, sasa wanajaribu kuwanyamazisha wanafunzi. Lakini hawaweza.

SOMO LA 96

Yesu Amchagua Sauli

Sauli ni adui mkatili wa Wakristo, lakini angebadilika baada ya muda mfupi.

SOMO LA 97

Kornelio Apokea Roho Takatifu

Kwa nini Mungu alimtuma Petro nyumbani kwa mwanamume huyo, ambaye si Myahudi?

SOMO LA 98

Ukristo Waenea Katika Mataifa Mengi

Mtume Paulo na waandamani wake waanza kuhubiri katika maeneo ya mbali.

SOMO LA 99

Mlinzi wa Jela Ajifunza Kweli

Roho mwovu, tetemeko la ardhi, na upanga vinahusikaje katika hadithi hii?

SOMO LA 100

Paulo na Timotheo

Wanaume hao wawili walifanya kazi pamoja kwa miaka mingi wakiwa marafiki na wafanyakazi wenzi.

SOMO LA 101

Paulo Apelekwa Roma

Safari imejaa hatari, lakini hakuna hali yoyote ngumu inayoweza kumzuia mtume huyu.

SOMO LA 102

Ufunuo kwa Yohana

Yesu alimpa mfululizo wa maono kuhusu wakati ujao.

SOMO LA 103

“Ufalme Wako na Uje”

Ufunuo kwa Yohana unaonyesha jinsi Ufalme wa Mungu utakavyobadili maisha duniani.