MASOMO UNAYOWEZA KUJIFUNZA KATIKA BIBLIA

Utangulizi wa Sehemu ya 13

Kiswahili
Utangulizi wa Sehemu ya 13
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/1102016143/univ/art/1102016143_univ_sqr_xl.jpg
lfb kur. 202-203

Utangulizi wa Sehemu ya 13

Utangulizi wa Sehemu ya 13

Yesu alikuja duniani ili kutoa uhai wake kwa ajili ya wanadamu wasio wakamilifu. Ingawa alikufa, yeye aliushinda ulimwengu. Yehova alikuwa mshikamanifu kwa Mwana wake, hivyo alimfufua. Alipokuwa hai hapa duniani, Yesu aliwatumikia watu kwa unyenyekevu na kuwasamehe walipokosea. Baada ya kufufuliwa, Yesu aliwatokea wanafunzi wake. Aliwafundisha jinsi ya kufanya kazi muhimu aliyokuwa amewapa. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako kuelewa kwamba sisi pia tunapaswa kushiriki katika kazi hiyo.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 87

Mlo wa Mwisho wa Jioni wa Yesu

Yesu aliwapa mitume wake maagizo muhimu wakati wa mlo wao wa mwisho wakiwa pamoja.

SOMO LA 88

Yesu Akamatwa

Yuda Iskariote aliongoza umati wa watu wenye marungu na mapanga ili wamkamate Yesu.

SOMO LA 89

Petro Anamkana Yesu

Ni nini kilichotendeka katika ua wa nyumba ya Kayafa? Yesu alitendewa jinsi gani ndani ya nyumba hiyo?

SOMO LA 90

Yesu Afa huko Golgotha

Kwa nini Pilato anaamuru Yesu auawe?

SOMO LA 91

Yesu Afufuliwa

Ni mambo gani yenye kupendeza yanayotokea siku kadhaa baada ya Yesu kuuawa?

SOMO LA 92

Yesu Awatokea Wavuvi

Anafanya nini ili wamtambue?

SOMO LA 93

Yesu Arudi Mbinguni

Lakini kabla ya kufanya hivyo, anawapa wanafunzi wake maagizo muhimu sana.