MASOMO UNAYOWEZA KUJIFUNZA KATIKA BIBLIA

Utangulizi wa Sehemu ya 4

Kiswahili
Utangulizi wa Sehemu ya 4
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/1102016134/univ/art/1102016134_univ_sqr_xl.jpg
lfb kur. 38-39

Utangulizi wa Sehemu ya 4

Utangulizi wa Sehemu ya 4

Katika sehemu hii tutajifunza kuhusu Yosefu, Ayubu, Musa, na Waisraeli. Wote walivumilia mambo mengi mabaya kutoka kwa Ibilisi. Baadhi yao walitendewa isivyo haki, wakafungwa gerezani, wakawa watumwa, na hata wengine wakauawa. Hata hivyo, Yehova aliwalinda katika njia mbalimbali. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako aelewe jinsi ambavyo watumishi hao wa Yehova walivumilia mambo mabaya bila kuruhusu imani yao idhoofike.

Yehova alileta Mapigo Kumi ili kuonyesha yeye ni mwenye nguvu kuliko miungu yote ya Wamisri. Kazia jinsi ambavyo Yehova aliwalinda watu wake wakati uliopita na jinsi anavyofanya hivyo leo.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 14

Mtumwa Aliyemtii Mungu

Yosefu alifanya mambo mazuri, lakini bado aliteseka sana. Kwa nini?

SOMO LA 15

Yehova Hakumsahau Yosefu Kamwe

Ingawa Yosefu alikuwa mbali na familia yao, Mungu alimthibitishia kwamba alikuwa pamoja naye.

SOMO LA 16

Ayubu Alikuwa Nani?

Alimtii Yehova hata ilipokuwa vigumu.

SOMO LA 17

Musa Aliamua Kumwabudu Yehova

Alipokuwa mtoto, Musa aliokolewa kwa sababu ya hekima ya mama yake.

SOMO LA 18

Kichaka Kinachowaka Moto

Kwa nini moto haukukiteketeza kichaka hicho?

SOMO LA 19

Mapigo Matatu ya Kwanza

Farao aliwasababishia watu wake msiba kwa sababu kiburi kilimzuia kuchukua hatua moja tu rahisi.

SOMO LA 20

Mapigo Sita Yaliyofuata

Mapigo hayo yalitofautianaje na mapigo matatu ya kwanza?

SOMO LA 21

Pigo la Kumi

Pigo la mwisho lilikuwa baya sana hivi kwamba mwishowe hata Farao mwenye kiburi alikubali kuwaruhusu Waisraeli waondoke.

SOMO LA 22

Muujiza Katika Bahari Nyekundu

Farao aliokoka mapigo kumi, lakini je, aliokoka muujiza huu wa Mungu?