Utangulizi wa Sehemu ya 5

Utangulizi wa Sehemu ya 5

Miezi miwili baada ya kuvuka Bahari Nyekundu, Waisraeli walifika kwenye Mlima Sinai. Wakiwa hapo, Yehova alifanya agano pamoja na Waisraeli ili wawe taifa lake la pekee. Aliwalinda na kuwaandalia kila kitu walichohitaji—aliwapa mana ili wale, mavazi yasiyochakaa, na mahali salama pa kuishi. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako aelewe kwa nini Yehova aliwapa Waisraeli Sheria, maskani, na ukuhani. Kazia umuhimu wa kutimiza mambo tunayoahidi, kuendelea kuwa wanyenyekevu, na sikuzote kudumisha ushikamanifu kwa Yehova.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 23

Waisraeli Wamtolea Yehova Ahadi

Waisraeli walimtolea Mungu ahadi ya pekee walipokuwa wamepiga kambi kwenye Mlima Sinai.

SOMO LA 24

Walivunja Ahadi Yao

Musa alipokuwa akipewa zile Amri Kumi, watu walitenda dhambi nzito.

SOMO LA 25

Maskani ya Ibada

Hema hilo la pekee lilikuwa na sanduku la agano.

SOMO LA 26

Wale Wapelelezi Kumi na Wawili

Yoshua na Kalebu walikuwa tofauti na wale wapelelezi wengine kumi ambao waliipeleleza nchi ya Kanaani.

SOMO LA 27

Walimwasi Yehova

Kora, Dathani, Abiramu, na wanaume wengine 250 walikosa kutambua jambo fulani muhimu kumhusu Yehova.

SOMO LA 28

Punda wa Balaamu Azungumza

Punda aliona mtu ambaye Balaamu hangeweza kumwona.