Utangulizi wa Sehemu ya 5
Miezi miwili baada ya kuvuka Bahari Nyekundu, Waisraeli walifika kwenye Mlima Sinai. Wakiwa hapo, Yehova alifanya agano pamoja na Waisraeli ili wawe taifa lake la pekee. Aliwalinda na kuwaandalia kila kitu walichohitaji—aliwapa mana ili wale, mavazi yasiyochakaa, na mahali salama pa kuishi. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako aelewe kwa nini Yehova aliwapa Waisraeli Sheria, maskani, na ukuhani. Kazia umuhimu wa kutimiza mambo tunayoahidi, kuendelea kuwa wanyenyekevu, na sikuzote kudumisha ushikamanifu kwa Yehova.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 23
Waisraeli Wamtolea Yehova Ahadi
Waisraeli walimtolea Mungu ahadi ya pekee walipokuwa wamepiga kambi kwenye Mlima Sinai.
SOMO LA 26
Wale Wapelelezi Kumi na Wawili
Yoshua na Kalebu walikuwa tofauti na wale wapelelezi wengine kumi ambao waliipeleleza nchi ya Kanaani.
SOMO LA 27
Walimwasi Yehova
Kora, Dathani, Abiramu, na wanaume wengine 250 walikosa kutambua jambo fulani muhimu kumhusu Yehova.