MASOMO UNAYOWEZA KUJIFUNZA KATIKA BIBLIA

Mnara wa Babeli

Kiswahili
Mnara wa Babeli
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/1102016017/univ/art/1102016017_univ_sqr_xl.jpg
lfb somo la 7

SOMO LA 7

Mnara wa Babeli

Mnara wa Babeli

Baada ya Gharika, wana wa Noa na wake zao walizaa watoto wengi. Watu waliongezeka na kuenea duniani, kama Yehova alivyokuwa amewaagiza.

Lakini baadhi ya watu hawakumtii Yehova. Walisema: ‘Acheni tujenge jiji na kukaa pamoja. Tutajenga mnara mrefu sana na kilele chake kitafika mbinguni. Kisha, tutakuwa watu mashuhuri.’

Yehova hakupendezwa na mambo ambayo watu hao walifanya, hivyo aliamua kusimamisha ujenzi huo. Je, unajua alifanya hivyo jinsi gani? Yehova alifanya watu hao wazungumze lugha mbalimbali. Kwa kuwa hawakuelewana, ujenzi ulikoma. Jiji walilojenga liliitwa Babeli, jina linalomaanisha “Machafuko.” Watu walitawanyika na kuishi maeneo mbalimbali ya dunia. Hata hivyo, waliendelea kufanya mambo mabaya katika maeneo mapya walioishi. Je, kuna watu walioendelea kumpenda Yehova? Tutajifunza jambo hilo katika somo linalofuata.

“Kila mtu anayejiinua atafedheheshwa, lakini yeyote anayejinyenyekeza atainuliwa.”​—Luka 18:14