Isaya 9:1-21

  • Nuru kuu kwa ajili ya nchi ya Galilaya (1-7)

    • “Mkuu wa Amani” azaliwa (6, 7)

  • Mkono wa Mungu dhidi ya Israeli (8-21)

9  Hata hivyo, utusitusi huo hautakuwa kama nchi ilipokuwa na taabu, kama nyakati za zamani nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali zilipodharauliwa.+ Lakini baadaye Yeye ataifanya iheshimiwe—njia iliyo kando ya bahari, katika eneo la Yordani, Galilaya ya mataifa.   Watu waliokuwa wakitembea gizaniWameona nuru kuu. Na wale wanaokaa katika nchi ya kivuli kizito,Nuru imewaangazia.+   Umelifanya taifa hilo liwe na watu wengi;Umefanya shangwe yake iwe kubwaWanashangilia mbele zakoKama watu wanavyoshangilia wakati wa mavuno,Kama wale wanaogawana nyara kwa shangwe.   Kwa maana umeivunjavunja nira ya mzigo wao,Fimbo iliyo kwenye mabega yao, gongo la msimamizi wa kazi,Kama katika siku ya Midiani.+   Kila kiatu cha askari kinachotikisa dunia kinapopiga mwendoNa kila vazi lililoloweshwa katika damuLitakuwa kuni kwa ajili ya moto.   Kwa maana mtoto amezaliwa kwetu,+Tumepewa mwanaNa utawala* utakaa juu ya bega lake.+ Jina lake litakuwa Mshauri wa Ajabu,+ Mungu Mwenye Nguvu,+ Baba wa Milele, Mkuu wa Amani.   Kwa wingi wa utawala wake*Na amani, hakutakuwa na mwisho,+Kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na juu ya ufalme wakeIli kuuimarisha kabisa+ na kuutegemezaKupitia haki+ na uadilifu,+Kuanzia sasa mpaka milele. Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.   Yehova alituma neno dhidi ya Yakobo,Nalo limekuja dhidi ya Israeli.+   Na watu wote watalijua—Efraimu na wakaaji wa Samaria—Ambao wanasema kwa kiburi chao na mioyo yao yenye dharau: 10  “Matofali yameanguka,Lakini tutajenga kwa mawe yaliyochongwa.+ Mikuyu imekatwa,Lakini tutaweka mierezi badala yake.” 11  Yehova atawainua wapinzani wa Resini dhidi yakeNaye atawachochea maadui wake wachukue hatua, 12  Siria kutoka mashariki na Wafilisti kutoka magharibi,*+Watamnyafua Israeli kwa vinywa vilivyo wazi.+ Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.+ 13  Kwa maana watu hawajarudi kwa Yule anayewapiga;Hawajamtafuta Yehova wa majeshi.+ 14  Yehova atakata kabisa kutoka IsraeliKichwa na mkia, chipukizi na utete,* katika siku moja.+ 15  Mzee na anayeheshimiwa sana ndiye kichwa,Na nabii anayetoa mafundisho ya uwongo ndiye mkia.+ 16  Wale wanaowaongoza watu hawa wanawafanya watangetange;Na wale wanaoongozwa wamevurugika. 17  Ndiyo sababu Yehova hatawashangilia vijana wao,Naye hatawaonyesha rehema mayatima wao na wajane wao;Kwa sababu wote ni waasi imani na watenda maovu+Na kila kinywa kinasema kwa upumbavu. Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.+ 18  Kwa maana uovu unawaka kama moto,Ukiteketeza vichaka vya miiba na magugu. Utawasha moto vichaka vya msitu,Navyo vitapanda juu katika mawingu ya moshi. 19  Katika ghadhabu ya Yehova wa majeshiNchi imewashwa moto,Na watu watakuwa kuni kwa ajili ya huo moto. Hakuna yeyote atakayemhurumia hata ndugu yake. 20  Mtu atakata upande wa kuliaLakini bado atakuwa na njaa,Na mtu atakula upande wa kushotoLakini hatashiba. Kila mtu atainyafua nyama ya mkono wake mwenyewe, 21  Manase atamnyafua Efraimu,Na Efraimu atamnyafua Manase. Wote pamoja watapigana na Yuda.+ Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.+

Maelezo ya Chini

Au “serikali; utawala wa kifalme.”
Au “serikali yake; utawala wake wa kifalme.”
Tnn., “kutoka nyuma.”
Au labda, “tawi la mtende na tete.”