Isaya 20:1-6

  • Ishara dhidi ya Misri na Ethiopia (1-6)

20  Mwaka ambao Mfalme Sargoni wa Ashuru alimtuma Tartani* aende Ashdodi,+ alipigana na Ashdodi na kuliteka.+  Wakati huo Yehova alisema hivi kupitia Isaya+ mwana wa Amozi: “Nenda ukavue nguo ya magunia kutoka kiunoni mwako, na uvue viatu vilivyo miguuni mwako.” Naye akafanya hivyo, akatembea akiwa uchi* na bila viatu.  Kisha Yehova akasema: “Kama mtumishi wangu Isaya alivyotembea akiwa uchi na bila viatu kwa miaka mitatu ili kuwa ishara+ na dalili dhidi ya Misri+ na dhidi ya Ethiopia,+  hivyo ndivyo mfalme wa Ashuru atakavyowaongoza mateka wa Misri+ na wahamishwa wa Ethiopia, wavulana na wanaume wazee, wakiwa uchi na bila viatu na matako yakiwa wazi, uchi wa* Misri.  Nao wataogopa na kuona aibu kwa ajili ya Ethiopia tumaini lao na kwa ajili ya Misri fahari yao.*  Wakaaji wa eneo hili la pwani watasema siku hiyo, ‘Tazama kilicholipata tumaini letu, tulilolikimbilia ili kupata msaada na kuokolewa kutoka kwa mfalme wa Ashuru! Tutaokokaje sasa?’”

Maelezo ya Chini

Au “kamanda.”
Au “akiwa amevaa mavazi machache.”
Au “aibu ya.”
Au “Misri ambayo walivutiwa na urembo wake.”