Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kitabu cha Isaya

Sura

Muhtasari wa Yaliyomo

  • 1

    • Baba na wanawe waasi (1-9)

    • Yehova anachukia ibada ya kidesturi (10-17)

    • “Tunyooshe mambo kati yetu” (18-20)

    • Sayuni litakuwa jiji lenye uaminifu tena (21-31)

  • 2

    • Mlima wa Yehova wainuliwa (1-5)

      • Panga zitakuwa majembe ya plau (4)

    • Siku ya Yehova itawafedhehesha wenye majivuno (6-22)

  • 3

    • Viongozi wa Yuda wawapotosha watu (1-15)

    • Mabinti wa Sayuni wanaotongoza wahukumiwa (16-26)

  • 4

    • Wanawake saba kwa mwanamume mmoja (1)

    • Atakachochipusha Yehova kitakuwa chenye utukufu (2-6)

  • 5

    • Wimbo kuhusu shamba la Yehova la mizabibu (1-7)

    • Ole kwa shamba la Yehova la mizabibu (8-24)

    • Hasira ya Mungu dhidi ya watu wake (25-30)

  • 6

    • Maono ya Yehova katika hekalu lake (1-4)

      • “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova” (3)

    • Midomo ya Isaya yasafishwa (5-7)

    • Isaya atumwa (8-10)

      • “Mimi hapa! Nitume mimi!” (8)

    • “Ni mpaka lini, Ee Yehova?” (11-13)

  • 7

    • Ujumbe kwa Mfalme Ahazi (1-9)

      • Shear-yashubu (3)

    • Ishara ya Imanueli (10-17)

    • Matokeo ya kutokuwa waaminifu (18-25)

  • 8

    • Shambulizi linalokuja la Ashuru (1-8)

      • Maher-shalal-hash-bazi (1-4)

    • Usiogope⁠—“Mungu yuko pamoja nasi!” (9-17)

    • Isaya na watoto wake ni kama ishara (18)

    • Tafuteni habari katika sheria, si kwa roho waovu (19-22)

  • 9

    • Nuru kuu kwa ajili ya nchi ya Galilaya (1-7)

      • “Mkuu wa Amani” azaliwa (6-7)

    • Mkono wa Mungu dhidi ya Israeli (8-21)

  • 10

    • Mkono wa Mungu dhidi ya Israeli (1-4)

    • Ashuru⁠—​Fimbo ya hasira ya Mungu (5-11)

    • Ashuru kuadhibiwa (12-19)

    • Watu waliobaki wa Yakobo watarudi (20-27)

    • Mungu atahukumu Ashuru (28-34)

  • 11

    • Utawala wa uadilifu wa tawi la Yese (1-10)

      • Mbwamwitu na mwanakondoo watakaa pamoja (6)

      • Ujuzi kumhusu Yehova utajaa duniani (9)

    • Waliobaki watarudishwa (11-16)

  • 12

    • Wimbo wa shukrani (1-6)

      • “Yah Yehova ni nguvu zangu” (2)

  • 13

    • Tangazo dhidi ya Babiloni (1-22)

      • Siku ya Yehova iko karibu! (6)

      • Wamedi kuangusha Babiloni (17)

      • Babiloni halitakaliwa kamwe (20)

  • 14

    • Waisraeli wataishi katika nchi yao (1, 2)

    • Dhihaka dhidi ya mfalme wa Babiloni (3-23)

      • Anayeng’aa ataanguka kutoka mbinguni (12)

    • Mkono wa Yehova utamponda Mwashuru (24-27)

    • Tangazo dhidi ya Ufilisti (28-32)

  • 15

    • Tangazo dhidi ya Moabu (1-9)

  • 16

    • Ujumbe dhidi ya Moabu waendelea (1-14)

  • 17

    • Tangazo dhidi ya Damasko (1-11)

    • Mataifa yatakemewa na Yehova (12-14)

  • 18

    • Ujumbe dhidi ya Ethiopia (1-7)

  • 19

    • Tangazo dhidi ya Misri (1-15)

    • Wamisri watamjua Yehova (16-25)

      • Madhabahu kwa ajili ya Yehova nchini Misri (19)

  • 20

    • Ishara dhidi ya Misri na Ethiopia (1-6)

  • 21

    • Tangazo dhidi ya nyika ya bahari (1-10)

      • Kulinda kwenye mnara wa mlinzi (8)

      • “Babiloni ameanguka!” (9)

    • Tangazo dhidi ya Duma na nchi tambarare ya jangwani (11-17)

      • “Mlinzi, kuna habari gani za usiku?” (11)

  • 22

    • Tangazo kuhusu Bonde la Maono (1-14)

    • Eliakimu awa msimamizi badala ya Shebna (15-25)

      • Kigingi cha mfano (23-25)

  • 23

    • Tangazo dhidi ya Tiro (1-18)

  • 24

    • Yehova ataifanya nchi kuwa tupu (1-23)

      • Yehova ni Mfalme katika Sayuni (23)

  • 25

    • Baraka nyingi kwa watu wa Mungu (1-12)

      • Karamu ya Yehova ya divai bora (6)

      • Kifo hakitakuwepo tena (8)

  • 26

    • Wimbo kuhusu tumaini na wokovu (1-21)

      • Yah Yehova, Mwamba wa milele (4)

      • Watu duniani watajifunza uadilifu (9)

      • “Wafu wako wataishi” (19)

      • Ingieni katika vyumba vya ndani mjifiche (20)

  • 27

    • Yehova amuua Lewiathani (1)

    • Wimbo kuhusu Israeli likiwa shamba la mizabibu (2-13)

  • 28

    • Ole kwa walevi wa Efraimu! (1-6)

    • Makuhani na manabii wa Yuda wapepesuka (7-13)

    • “Agano na Kifo” (14-22)

      • Jiwe la pembeni lenye thamani katika Sayuni (16)

      • Kazi ya Yehova isiyo ya kawaida (21)

    • Mfano kuhusu nidhamu ya Yehova yenye hekima (23-29)

  • 29

    • Ole kwa Arieli! (1-16)

      • Ibada ya midomo tu yashutumiwa (13)

    • Viziwi watasikia; na vipofu wataona (17-24)

  • 30

    • Msaada wa Misri ni bure kabisa (1-7)

    • Watu wakataa ujumbe wa kinabii (8-14)

    • Mtakuwa na nguvu mkiendelea kuwa na tumaini (15-17)

    • Yehova awaonyesha kibali watu wake (18-26)

      • Yehova, Mfundishaji Mkuu (20)

      • “Hii ndiyo njia” (21)

    • Yehova atatekeleza hukumu dhidi ya Ashuru (27-33)

  • 31

    • Msaada wa kweli unatoka kwa Mungu, hautoki kwa wanadamu (1-9)

      • Farasi wa Misri ni nyama tu (3)

  • 32

    • Mfalme na wakuu watatawala kwa haki ya kweli  (1-8)

    • Wanawake wanaopuuza mambo waonywa (9-14)

    • Kumiminwa kwa roho kwaleta baraka (15-20)

  • 33

    • Hukumu na tumaini kwa waadilifu (1-24)

      • Yehova ni Mwamuzi, Mpaji-sheria, na Mfalme (22)

      • Hakuna atakayesema: “Mimi ni mgonjwa” (24)

  • 34

    • Kisasi cha Yehova dhidi ya mataifa (1-8)

    • Edomu itafanywa ukiwa (9-17)

  • 35

    • Paradiso yarudishwa (1-7)

      • Vipofu wataona; viziwi watasikia (5)

    • Njia ya Utakatifu kwa ajili ya waliokombolewa (8-10)

  • 36

    • Senakeribu ashambulia Yuda (1-3)

    • Rabshake amdhihaki Yehova (4-22)

  • 37

    • Hezekia atafuta msaada wa Mungu kupitia Isaya (1-7)

    • Senakeribu atishia Yerusalemu (8-13)

    • Sala ya Hezekia (14-20)

    • Isaya apeleka jibu la Mungu (21-35)

    • Malaika awaua Waashuru 185,000 (36-38)

  • 38

    • Hezekia ashikwa na ugonjwa kisha apona (1-22)

      • Wimbo wa shukrani (10-20)

  • 39

    • Wajumbe kutoka Babiloni (1-8)

  • 40

    • Faraja kwa watu wa Mungu (1-11)

      • Sauti nyikani (3-5)

    • Ukuu wa Mungu (12-31)

      • Mataifa kama tone kutoka katika ndoo (15)

      • Mungu hukaa “juu ya duara ya dunia” (22)

      • Nyota zote huitwa kwa majina (26)

      • Mungu hachoki kamwe (28)

      • Wanaomtumaini Yehova watapata nguvu mpya (29-31)

  • 41

    • Mshindi kutoka mashariki (1-7)

    • Israeli achaguliwa kuwa mtumishi wa Mungu (8-20)

      • “Rafiki yangu Abrahamu” (8)

    • Miungu mingine yajaribiwa (21-29)

  • 42

    • Mtumishi wa Mungu na kazi yake (1-9)

      • ‘Jina langu ni Yehova’ (8)

    • Wimbo mpya wa kumsifu Yehova (10-17)

    • Israeli ni kipofu na kiziwi (18-25)

  • 43

    • Yehova awakusanya tena watu wake (1-7)

    • Miungu yashtakiwa (8-13)

      • “Ninyi ni mashahidi wangu” (10, 12)(10, 12)

    • Waachiliwa huru kutoka Babiloni (14-21)

    • “Tukutane ili tufanye kesi” (22-28)

  • 44

    • Baraka kwa watu waliochaguliwa na Mungu (1-5)

    • Hakuna Mungu ila Yehova (6-8)

    • Upumbavu wa sanamu zilizotengenezwa na wanadamu (9-20)

    • Yehova, Mkombozi wa Israeli (21-23)

    • Ukombozi kupitia Koreshi (24-28)

  • 45

    • Koreshi atiwa mafuta ili aliteke Babiloni (1-8)

    • Udongo haupaswi kushindana na Mfinyanzi (9-13)

    • Mataifa mengine yatambua Israeli (14-17)

    • Mungu anategemeka katika uumbaji na katika kufunua mambo (18-25)

      • Dunia iliumbwa ili ikaliwe (18)

  • 46

    • Sanamu za Babiloni dhidi ya Mungu wa Israeli (1-13)

      • Yehova atabiri mambo ya wakati ujao (10)

      • Ndege anayewinda anayetoka mashariki (11)

  • 47

    • Kuanguka kwa Babiloni (1-15)

      • Wanajimu wafunuliwa (13-15)

  • 48

    • Watu wa Israeli wakemewa na kusafishwa (1-11)

    • Yehova atachukua hatua dhidi ya Babiloni (12-16a)

    • Mafundisho ya Mungu ni yenye faida (16b-19)

    • “Tokeni Babiloni!” (20-22)

  • 49

    • Kazi ya mtumishi wa Yehova (1-12)

      • Nuru ya mataifa (6)

    • Faraja kwa Waisraeli (13-26)

  • 50

    • Dhambi za Waisraeli zasababisha matatizo (1-3)

    • Mtumishi mtiifu wa Yehova (4-11)

      • Ulimi na sikio la waliofundishwa (4)

  • 51

    • Sayuni larudishwa kuwa kama bustani ya Edeni (1-8)

    • Faraja kutoka kwa Muumba wa Sayuni mwenye nguvu (9-16)

    • Kikombe cha ghadhabu ya Yehova (17-23)

  • 52

    • Amka, Ee Sayuni! (1-12)

      • Miguu ya wale wanaoleta habari njema inapendeza (7)

      • Walinzi wa Sayuni wapaza sauti kwa pamoja (8)

      • Wale wanaobeba vyombo vya Yehova lazima wawe safi (11)

    • Mtumishi wa Yehova atakwezwa (13-15)

      • Sura iliyoharibika (14)

  • 53

    • Kuteseka, kufa, na kuzikwa kwa mtumishi wa Yehova (1-12)

      • Adharauliwa na kuepukwa (3)

      • Abeba magonjwa na maumivu (4)

      • “Kama kondoo machinjioni” (7)

      • Abeba dhambi za wengi (12)

  • 54

    • Sayuni aliye tasa atapata wana wengi (1-17)

      • Yehova ni mume wa Sayuni (5)

      • Wana wa Sayuni watafundishwa na Yehova (13)

      • Silaha dhidi ya Sayuni zitashindwa (17)

  • 55

    • Mwaliko wa kula na kunywa bure (1-5)

    • Mtafuteni Yehova na neno lake linalotegemeka (6-13)

      • Njia za Mungu ziko juu kuliko njia za mwanadamu (8, 9)

      • Neno la Mungu hakika litafanikiwa (10, 11)

  • 56

    • Baraka kwa wageni na matowashi (1-8)

      • Nyumba ya sala kwa ajili ya wote (7)

    • Walinzi vipofu, mbwa walio bubu (9-12)

  • 57

    • Mtu mwadilifu na watu washikamanifu waangamia (1, 2)

    • Ukahaba wa kiroho wa Israeli wafunuliwa (3-13)

    • Faraja kwa watu wa hali ya chini (14-21)

      • Waovu ni kama bahari iliyochafuka (20)

      • Hakuna amani kwa waovu (21)

  • 58

    • Kufunga kwa kweli na kwa uwongo (1-12)

    • Kushika Sabato kwa furaha (13, 14)

  • 59

    • Dhambi za Waisraeli zawatenga na Mungu (1-8)

    • Kuungama dhambi (9-15a)

    • Yehova huingilia kati kwa ajili ya wanaotubu (15b-21)

  • 60

    • Utukufu wa Mungu wang’aa juu ya Sayuni (1-22)

      • Kama njiwa kwenye viota vyao (8)

      • Dhahabu badala ya shaba (17)

      • Mdogo atakuwa elfu (22)

  • 61

    • Atiwa mafuta ili kutangaza habari njema (1-11)

      • “Mwaka wa nia njema ya Yehova” (2)

      • “Miti mikubwa ya uadilifu” (3)

      • Watu wa nchi nyingine watasaidia (5)

      • “Makuhani wa Yehova” (6)

  • 62

    • Jina jipya la Sayuni (1-12)

  • 63

    • Kisasi cha Yehova dhidi ya mataifa (1-6)

    • Upendo mshikamanifu wa Yehova nyakati za zamani (7-14)

    • Sala ya toba (15-19)

  • 64

    • Sala ya toba yaendelea (1-12)

      • Yehova “Mfinyanzi wetu” (8)

  • 65

    • Hukumu ya Yehova dhidi ya wanaoabudu sanamu (1-16)

      • Mungu wa Bahati Njema na Mungu wa Majaliwa (11)

      • “Watumishi wangu watakula” (13)

    • Mbingu mpya na dunia mpya (17-25)

      • Kujenga nyumba; kupanda mashamba ya mizabibu (21)

      • Hakuna atakayefanya kazi ngumu bure (23)

  • 66

    • Ibada ya kweli na ibada ya uwongo (1-6)

    • Sayuni na wanawe (7-17)

    • Watu wakusanyika Yerusalemu ili kuabudu (18-24)